
Dar es Salaam, 18 Julai 2025
Mwandishi wa vitabu vya kuelimisha watoto, Bi. Riziki Mohamed Juma, amezindua rasmi kitabu chake kipya kiitwacho “Saburi” katika hafla iliyofanyika katika Maktaba Kuu ya Taifa jijini Dar es Salaam.
Uzinduzi huu uliambatana na utambulisho wa vitabu vingine vya watoto, vikiwemo vya maandishi ya kawaida na vya nukta nundu kwa ajili ya watoto wenye mahitaji maalum.

Vitabu hivi vimetolewa kwa ushirikiano kati ya Mtalimbo Books na Dhahabu Publishers, na vinapatikana katika maduka ya vitabu na maktaba za jamii nchini.
Saburi ni hadithi ya kuvutia inayowasilisha ujumbe kuhusu athari za utoro shuleni kwa njia rahisi na ya kufundisha. Ni kitabu kinachofaa kwa watoto, wazazi, walezi na walimu.


Vitabu hivi vimetolewa kwa ushirikiano kati ya Mtalimbo Books na Dhahabu Publishers, na vinapatikana katika maduka ya vitabu na maktaba za jamii nchini.
Saburi ni hadithi ya kuvutia inayowasilisha ujumbe kuhusu athari za utoro shuleni kwa njia rahisi na ya kufundisha. Ni kitabu kinachofaa kwa watoto, wazazi, walezi na walimu.

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...