Na Nasra Ismail
Wizara ya Mifugo na Uvuvi leo imezindua chanjo ya homa ya mapafu kwa ngombe mkoani Geita pamoja na kuzindua zoezi la uvikwaji wa hereni kwa ngombe na kuachana na utaratibu wa kuwagonga mihuri ya moto kwenye ngozi.
Zoezi hilo la uzinduzi limefanyika katika halmashauri ya wilaya ya Chato pamoja na wilaya ya Bukombe huku lengo likiwa ni kupandisha thamani ya mifugo nchini pamoja na kupunguza upotevu wa mifugo.
Kupitia hereni hizi za ng'ombe wataweza kusajiriwa kupitia jina la mmiliki Pamoja na kuwa na uwezo wa kufatiliwa wakiibiwa kupitia hereni hizi.
Waziri wa ufugaji na uvuvi Dkt Ashatu Kijaji ametoa wito kwa wafugaji kujitokeza kupeleka mifugo yao kupata chanjo ili mifugo hiyo iwe na thamani na kuweza kuuzwa nje.
Aliongeza kuwa uchanjaji wa mifugo hii utakuwa ni bure ambapo chanjo zinazotolewa ni pamoja na homa ya mapafu, sotoka kwa mbuzi na kondoo pamoja na chanjo ya kideli kwa ajili ya kuku na bata.
Mkoa wa Geita una takribani ng'ombe milion 1 ambapo katika wilaya ya Chato jumla ya ng'ombe 600 watapata chanjo hizi.

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...