Na Mwandishi wetu- Arusha

Mwenyekiti wa bodi ya wadhamini MOI Dkt. Marina Njelekela ameipongeza menejimenti ya MOI kwa uamuzi wake wa kushiriki na kutoa huduma kwa washiriki wa mkutano wa wenyeviti wa bodi na wakuu wa Taasisi unaofanyika katika ukumbi wa AICC Arusha.

Dkt. Njelekela ametoa pongezi hizo Leo 25/08/2025 alipotembelea eneo la kutolea huduma la MOI katika ukumbi wa AICC

“Nawapongeza menejimenti nzima ya MOI ikiongozwa na Mhe. Balozi Dkt. Mpoki Ukisubisya kwa uamuzi huu mzuri wenye tija wa kuja kutoa huduma kwa ashiriki wa mkutano huu mkubwa na muhimu, hongereni sana “ Alisema Dkt. Njelekela

Pia , Dkt Njelekela amepongeza ushirikiano kati ya Taasisi ya MOI, Taasisi ya Moyo JKCI na Hospitali ya AICC katika kuwahudumia washiriki wa mkutano huo.

Awali, Mkurugenzi mtendaji wa MOI Mhe. Balozi Dkt. Mpoki Ulisubisya alimuarifu Dkt. Njelekela kwamba MOI imeleta madaktari bingwa wa mifupa, Ubongo, Mgongo, viungo na mishipa ya fahamu ili watoe huduma za ushauri (Consultation) kwa washiriki wa mkutano huo ambapo wale watakaohitaji uchunguzi zaidi watapewa rufaa kwenda MOI

Taasisi ya MOI imeanza kutoa huduma kwenye kikao kazi cha Wenyeviti wa bodi na wakuu wa Taasisi za umma 2025 jijini Arusha kuanzia Agosti 23, 2025 na kutamati Agosti 26, 2025.






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...