Na Pamela Mollel,Longido

Wilaya ya Longido imeendelea kupiga hatua kubwa za maendeleo katika sekta mbalimbali chini ya uongozi wa aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo, Steven Kiruswa kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Agosti 26, 2025, Kiruswa alichukua fomu ya kugombea tena ubunge katika Halmashauri ya Longido, akipokelewa kwa shamrashamra na wafuasi wa CCM

Akizungumza baada ya kuchukua fomu, Kiruswa alisema ameendelea kushirikiana na serikali, halmashauri na wadau wa maendeleo katika utekelezaji wa Ilani ya CCM, ikiwemo kuboresha huduma muhimu za kijamii.

Katika sekta ya elimu, amefanikisha ujenzi wa madarasa, mabweni na kuongeza walimu, jambo lililowezesha shule za msingi kufika kila kijiji na sekondari kila kata

Katika sekta ya afya, amesimamia ujenzi wa vituo vya afya pamoja na kuboresha hospitali ya wilaya kwa vifaa tiba na madaktari

Pia amesimamia miradi ya maji kupitia visima na miundombinu ya usambazaji maji safi, sambamba na uboreshaji wa barabara, umeme vijijini na mawasiliano ya simu.

Kiruswa aliwashukuru viongozi wa CCM kwa kumuamini kuendelea kupeperusha bendera ya chama hicho, akiahidi kuendeleza miradi yote ya maendeleo pale aliposhia.

Aidha, aliwataka wafuasi wa CCM kuhakikisha chama hicho kinashinda kwa kishindo katika uchaguzi Mkuu

“Naomba wananchi wa Longido tumchague Rais kwa asilimia 100, Mbunge kwa asilimia 100 na madiwani kwa asilimia 100 ili tuendelee kuipa CCM ushindi wa kishindo,” alisema Kiruswa huku akishangiliwa na umati wa wafuasi wake.






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...