Na Ally Issa.

Mgombea wa jimbo la Rufiji anayetetea jimbo lake Mohamed Mchengerwa ameibuka kidedea katika kinyang'anyiro cha kura za maoni kwa kuzoa asilimia 99.19 ya kura zote zilizopigwa.

Akitangaza matokeo hayo Mkurugenzi wa Uchaguzi wa jimbo hilo Prudence Sempa. amesema Mchengerwa amepata kura 8, 465 kati ya kura 8 , 533 zilizopigwa sawa na asili 99.19

Aidha, Sempa amesema kura zote zilizopigwa zilikuwa 8, 534 ambapo idadi ya kura zilizoharibika ni asilimia 0.01 ya kura zote halali.

Wagombea wengine Salma Hamis ,Selemani Mhekela na Hamisa Kisoma waligawana asilimia iliyobaki.

Baada ya kutangaza matokeo hayo wagombea hao wamempongeza Mchengerwa na kuahidi kushirikiana na yeyote kati yao ambaye atachaguliwa na Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) miongoni mwao kupeperusha bendera katika uchaguzi mkuu.

Naye Mchengerwa amewashukuru wajumbe kwa kumpa kura za kishindo huku akisema kuwa ana deni kubwa la kuwalipa endapo Chama chake CCM kitampitisha.






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...