Benki ya NMB imedhamini na kushiriki kwenye Kikao kazi cha wenyeviti wa Bodi na watendaji wakuu wa taasisi za umma (CEOs Forum
2025) kinachoendelea katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano Arusha (Arusha International Conference Centre).
Ujumbe wa NMB umeongozwa na David Nchimbi - Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi pamoja na Juma Kimori - Afisa Mkuu wa Fedha na Kaimu Afisa Mtendaji mkuu.
Kikao kazi hicho cha Siku tatu kinawashirikisha Viongozi zaidi ya Mia Sita Hamsini kutoka Taasisi, Mashirika na Wakala wa Serikali. Kauli mbiu ya Kikao hicho ni “Kujenga Ushirikiano Endelevu katika Mazingira ya Ushindani wa Kimataifa – Wajibu wa Mashirika ya Umma.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...