Waziri Mkuu mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mizengo Pinda ametaka Utaalamu wa Kisanyansi uzingatiwe katika mnyororo mzima wa thamani wa sekta ya Kilimo ikiwa ni pamoja na kuzingatia ufafanuzi wa Kisanyansi katika chapa za bidhaa mbalimbali za Kilimo zilizoongezewa thamani ili kuonesha tija inayopatikana kwa mtumiaji wa bidhaa hizo.

Mheshimiwa Pinda amesema hayo Leo Agosti 07,2025 alipokuwa katika Banda la Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) kwenye Maonesho ya kimataifa ya Kilimo Maarufu kama Nanenane yanayoendelea viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma ambapo TARI inashiriki ikiwa na Teknolojia mbalimbali za Kilimo.

Akitolea mfano wa Korosho iliyoongezewa thamani na TARI Mheshimiwa Pinda ameeleza kufuraishwa na ufafanuzi wa kitaalamu uliopo katika mfuko wa Korosho hizo unaotoa maelezo ya Kisanyansi kumtosheleza mtumiaji kutambua tija anayopata kutokana na matumizi ya bidhaa hiyo zaidi ya kuishia kusema ni tamu yenye ladha nzuri kitu ambacho amesema kinanyima fursa zaidi kwa mtumiaji kuelewa.

Akiwa katika Banda la TARI, Waziri Mkuu huyo mstaafu amepata maelezo kuhusu Teknolojia mbalimbali za Kilimo zilizofanyiwa Utafiti na TARI ambazo amewasihi wadau wa Kilimo kuzitumia ili kujiongezea tija.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...