Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Elimu kutoka Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Bw. Atupele Mwambene amesema serikali kupitia miradi mbalimbali imeboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia kwa kuyafanya yawe salama, yanavutia na rafiki kwa walimu na wanafunzi kufundisha na kujifunza ili kuendelea kuboresha Sekta ya elimu kote Nchini.

Bw. Mwambene ameyesema hayo wakati wa akifunga mafunzo ya Walimu wa ushauri, unasihi na ulinzi wa Watoto wa shule za Msingi Nchini, kupitia mpango wa shule salama unaotekelezwa kupitia mradi BOOST, yaliofanyika katika Chuo Cha Ualimu mkoani Tabora.



Amesema, Serikali imewezesha kujengwa kwa shule mpya 2,441 zikiwemo za msingi 1,399 na za sekondari 1,042 katika maeneo ya vijijini ambayo hayakuwa na shule na yenye msongamano mkubwa wa wanafunzi, na jumla shule kongwe 906 zilikarabatiwa na miundombinu mingine kama vile; vyumba vya madarasa, matundu ya vyoo, nyumba za walimu, mabweni, mabwalo, maabara na maktaba imejengwa na kukarabatiwa.

“Ofisi ya Rais – TAMISEMI katika kipindi cha mwaka 2022/23 hadi 2024/25 ilipeleka jumla ya shilingi bilioni 539.6 shuleni na kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya 656 za awali na msingi, lengo la msingi la uwekezaji huu ni kuhakikisha sisi kama Taifa, Wazazi na Walezi tunatoa fursa sawa ya Watoto kupata elimu” Mwambene.



Aidha, amewataka kwenda kuimarisha mifumo na taratibu za kushughulikia malalamiko ya wanafunzi kwa kuweka masanduku ya maoni, mabaraza ya watoto pamoja na madawati ya ulinzi na usalama wa mtoto shuleni kwa kufuata miongozo na kuweka mikakati ya kutatua changamoto zitakazowasilishwa na wanafunzi.

Vile vile, Bw. Mwambene amewaelekeza walimu kote Nchini kuhakikisha wananazingatia nidhamu, maadili na miiko ya ualimu ili kuhakikisha wanafunzi wanatendewa haki na kuondoa kabisa vitendo vya ukatili ambavyo vinaweza kufanywa na walimu dhidi ya Wanafunzi kwa sababu ya kutozingatia maadili ya ualimu.

Akitoa neno la utangulizi, Mratibu wa Mradi wa BOOST kutoka Ofisi ya Rais – TAMISEMI Mwal. Ally Swalehe amesema mradi huo ulianzisha ukiwa na malengo ya kupambana na changamoto ya uhaba na uchakavu wa miundombinu, baadhi ya wanafunzi wa darasa la pili kushindwa kumudu stadi za kusoma, kuhesabu na kuandika na baadhi ya wanafunzi kushindwa kuendelea na elimu ya sekondari.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...