MGOMBEA mwenza wa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi akimsikiliza Mlemavu wa Miguu,Amos Kalungula.
Dk.Nchimbi yuko mkoani Kagera ambako amewasili tangu jana na leo Septemba 7 ameendelea na mikutano ya kampeni ya kuomba kura za Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba 29,2025.
Akiwa katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika Uwanja wa Shule ya Msingi Kashai Bukoba Mjini baada ya kuwahutubia wananchi,alimfuata Kalungula ambaye ni mlemavu wa miguu aliyekuwa ameshika bahasha yenye rangi ya kaki na kisha kumkabidhi Dk.Nchimbi.
Hata hivyo bahasha hiyo aliyokabidhiwa Dk.Nchimbi haijafahamika ilikuwa imebeba ujumbe gani .Hata hivyo mkazi huyo alionekana kufurahishwa na upendo ulioneshwa na Dk.Nchimbi aliyeamua kumfuata kumsikiliza na kupokea barua hiyo.


Dk.Nchimbi yuko mkoani Kagera ambako amewasili tangu jana na leo Septemba 7 ameendelea na mikutano ya kampeni ya kuomba kura za Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba 29,2025.
Akiwa katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika Uwanja wa Shule ya Msingi Kashai Bukoba Mjini baada ya kuwahutubia wananchi,alimfuata Kalungula ambaye ni mlemavu wa miguu aliyekuwa ameshika bahasha yenye rangi ya kaki na kisha kumkabidhi Dk.Nchimbi.
Hata hivyo bahasha hiyo aliyokabidhiwa Dk.Nchimbi haijafahamika ilikuwa imebeba ujumbe gani .Hata hivyo mkazi huyo alionekana kufurahishwa na upendo ulioneshwa na Dk.Nchimbi aliyeamua kumfuata kumsikiliza na kupokea barua hiyo.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...