Na Said Mwishehe,Michuzi TV-Kilimanjaro 

MGOMBEA Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) Rais Dk.Samia Suluhu Hassan amesema katika miaka mitano ijayo Serikali itaendelea kuongeza makusanyo ya mapato ndani ya nchi yetu ili kuepuka manyanyaso yanayotokana na mikopo na misaada. 

Akizungumza mbele ya maelfu ya wananchi wa Wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro katika mkutano wa kampeni kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba 29 mwaka huu Dk.Samia amesema kıla ambacho wameahidi kwa wananchi kupitia Ilani ya Uchaguzi Mkuu 2025-2030 CCM inajua fedha itapatikana wapi.

“Kila tulichokiweka mule katika Ilani ya Uchaguzi Mkuu tunajua fedha yake ya utekelezaji inatoka wapi lakini nataka niwaambie lingine tumeongeza makusanyo ya mapato. 

“Tunajua hakika fedha zinatoka wapi. Tutakopa ndiyo lakini mikopo ambayo itaheshimu uhuru wa nchi yetu ndiyo tutakayokopa.”

Pamoja na hayo Dk.Samia Suluhu Hassan ametumia nafasi hiyo kuelezea faraja yake kwa wananchi wa Wilaya Mwanga ambayo inatokana na kutimiza mradi ambao marehemu Waziri Mkuu mstaafu na Makamu wa Rais mstaafu Cleopa David Msuya ulikuwa mradi wake wa kufa na kupona.

“Alinifuata na akaniomba miradi miwili mradi mmoja maji safi Mwanga - Korogwe na mradi wa pili wa barabara ya Msuya bypass.

“Faraja yangu ni kwamba miradi yote miwili nimeweza kuifanya ameiona kabla ya Mungu hajamchukua kwa hiyo nawashukuru wanamwanga. Niseme kwamba kwenye maji tumeweza kupandisha asilimia ya upatikanaji maji kutoa 77.5 mwaka 2023 hadi 81.9 mwaka jana.

“Miradi 26 imefanyika hapa kwa bilioni 54.2 na mradi wa Same Mwanga Korogwe peke yake una bilioni 304 kwa hiyo ni mradi mkubwa sana. 

“Tumetekeleza mradi huu kwa awamu ya kwanza ambayo tayari maji yameanza kupatikana. Na awamu ya pili ni kwenye maenwo yaliyobaki Same baadhi na kule Korogwe.

“Kama nilivyomuahidi marehemu Mzee Msuya tutakwenda kuukamilisha mradi huu sambamba na ile barabara ya Msuya bypass.”

Wakati huo huo mgombea Urais Dk.Samia amesema Serikali imejenga minara sita ya simu ili kuimarisha mawasiliano ya simu na kuwawezesha wananchi kufanya shughuli zao za kiuchumi.

“Sasa hivi mambo yote kwenye simu, kununua kwenye simu kutangaza biashara kwenye simu lazima tuhakikishwa network inapatikana kila mahali. “








Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...