NA VICTOR MASANGU,KIBAHA 

Mbunge mteule wa Jimbo la Kibaha mjini kupitia tiketi ya Chama cha mapinduzi (CCM) Silvestry Koka ameahidi kuboresha sekta ya afya,elimu na maji pindi atakapopewa ridhaa ya kuwaongoza  wananchi.

 Koka ameyasema hayo wakati wa ufunguzi rasmi wa kampeni za CCM kata ya Kibaha na kusema kuwa lengo lake kubwa ni kuendelea kushirikiana na serikali katika kuwaletea wananchi maendeleo.

Koka amebainisha kwamba  anatambua wananchi wa kata ya Kibaha wanahitaji  kwa kiasi kikubwa huduma mbali mbali ikiwemo suala la   upatikanaji wa maji safi na salama.

"Kitu kikubwa ambacho ninawaomba kwa dhati  wananchi wa kata ya Kibaha ni kuniamini pamoja na kunipa kura ili niweze kuendelea kuwapatia maendeleo katika nyanja mbali mbali,"amesema Koka.

Kadhalika Koka amebainisha kuwa ataweka mipango madhubuti ya kuweza kuhakikisha anatengeneza na kuboresha miundombinu ya barabara.

Kwa upande wake Diwani mteule wa kata ya Kibaha Omary Bula  amesema kwamba dhumuni lake ni kusikiliza kero na kutatua changamoto za wananchi.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha mapinduzi (CCM) Mwalimu Mwajuma Nyamka amewaomba wanachama wa CCM pamoja na wananchi kumchagua kwa kura nyingi  za  kishindo  nafasi ya Rais Dkt.Samia,Ubunge pamoja na udiwani.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...