Na Mwandishi Wetu, Bagamoyo.

Mgombea Ubunge wa Viti Maalum Mkoa wa Pwani kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mariam Ibrahim, amewataka wananchi wa Wilaya ya Bagamoyo kujitokeza kwa wingi siku ya uchaguzi na kumpigia kura Rais Dk. Samia Suluhu Hassan pamoja na wagombea wengine wa chama hicho.

Akizungumza katika uzinduzi wa kampeni uliofanyika wilayani humo jana Septemba 17, 2025, Mariam alipiga magoti mbele ya wananchi akisisitiza mshikamano na mshikikano wa kisiasa kwa ajili ya maendeleo ya taifa.

Mariam alisema ni muhimu Rais Samia, Mgombea Ubunge wa Bagamoyo Subira Mgalu, na madiwani wa CCM katika kata mbalimbali wakapewa kura nyingi ili kuendeleza miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali.

Aidha, aliwahimiza wanawake kushirikiana kikamilifu katika kampeni na kuhamasisha jamii nzima kujitokeza kwa wingi siku ya uchaguzi, akibainisha kuwa ushiriki wao ni nyenzo muhimu ya kuendeleza maendeleo ya Bagamoyo na taifa kwa ujumla.



















 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...