Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Dalmia Mikaya Septemba 26,2025 amepokea vifaa tiba viivyotolewa na benki ya NMB ikiwa ni sehemu ya benki hiyo kurudisha sehemu ya faida yake katika Jamii.
DC Dalmia amesema vifaa vilivyotolewa ni pamoja na vitanda vya Wanawake kujifungulia na vitanda vya uchunguzi 20 pamoja na mashine 20 za kusaidia kupumulia kwa Watoto wadogo wenye changamoto.
DC Dalmia ameishukuru benki ya NMB kwa kutoa msaada huo ukiwa na lengo la kusaidia mahitaji mbalimbali ya upatikanaji wa vifaa tiba na kuiunga mkono Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa ya iliyofanya ya ujenzi wa Hospitali ambayo imekua msaada mkubwa kwa Jamii.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...