Dar es Salaam, 4 Septemba 2025 – Kampuni ya michezo ya kubashiri PigaBet leo imetangaza kwa shangwe majina ya washindi wa promosheni zake kubwa mbili – SHINDA NDINGA na JISMATISHE, katika droo iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Mshindi wa promosheni ya SHINDA NDINGA ni Musa Nicodemus
kutoka mkoa wa Mwanza, ambaye ameibuka na zawadi ya smartphone ya kisasa kupitia
kampeni hiyo ya kipekee.
Washindi wa JISMATISHE
Hamis Kassim kutoka Tegeta, Dar es Salaam – amejinyakulia
Smart TV aina ya Hisense yenye ukubwa wa inch 55.
Innocent Sanga kutoka Arusha – ameibuka mshindi wa
smartphone ya kisasa aina ya Samsung.
Akizungumza baada ya kutangazwa kwa washindi, Meneja
Mawasiliano wa PigaBet, Hemed Jaafary Msonge, alisema:
“Tunafurahi kuona wateja wetu wakiendelea kufurahia promosheni zetu na kushinda zawadi kubwa. Hii ni njia yetu ya kurudisha shukrani kwa wachezaji wote wanaotuamini kila siku.”
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...