NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV
KIKUNDI cha Vision Vikoba ambacho ni kikundi mama cha vikundi 13) kimeadhimisha miaka 10 tangu kuanzishwa kwake, ambapo mshikamano na mshikamanifu wa kijamii umetajwa kuwa siri ya mafanikio yaliyowezesha kuendelea kwao hadi leo.
Akizungumza katika hafla ya maadhimisho hayo jijini Dar es Salaam, Mwanzilishi wa Vision Vikoba, Bi. Sharifa Mohamed, alisema walipoanza walikuwa na ndoto ya kuunda eneo la mshikamano na kusaidiana, lakini sasa ndoto hiyo imezaa matunda makubwa.
“Kikundi chetu mama kilikuwa kama mbegu, na vikundi 13 vilivyochipuka leo hii ni kama miti yenye matunda mema. Hii ndiyo maan a ya mshikamano na mshikamanifu wa kijamii,” alisema.
Kwa mujibu wake, kikundi kina jumla ya wanachama 314, ambapo asilimia 80 ni wanawake na asilimia 20 ni wanaume, huku dira ikiwa ni kukua zaidi na kugeuka kuwa vyama vya ushirika, taasisi za kifedha na hata kushiriki katika miradi ya kijamii.
Aidha, ameiomba Serikali kuendelea kuweka mazingira rafiki ya uwekezaji kwa wajasiriamali wadogo, akisema vikoba vimekuwa darasa la kujitegemea kiuchumi na kusaidia familia nyingi.
Akihutubia katika maadhimisho hayo, Katibu Tawala wa Wilaya ya Kinondoni, Bi. Warda Abdallah, amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika ofisi za wakuu wa wilaya ili kuchangamkia mikopo nafuu ya asilimia 10 inayotolewa na Serikali.
Amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imetoa fedha nyingi kwa wananchi ili kuwawezesha kujikomboa kutoka katika umaskini.
“Mkiwa mnajuana kitabia ni rahisi kuepusha migogoro. Changamkieni fursa hizi ili muondokane na umaskini,” alisema Bi. Warda.
Mwenyekiti wa Smart Vikoba Endelevu, Bi. Dainess Kalinga, amesema kupitia vikoba ameweza kununua ardhi, pikipiki na kuendesha biashara zake huku akisisitiza upendo na heshima kama nguzo ya kikundi.
Mdau kutoka Bakhresa Food Products, Bi. Rehema Salim, amesisitiza nidhamu ya fedha na mshikamano kama silaha ya vikoba endelevu.
Kwa upande wake, mwanachama Shedrack Sheria alitoa rai kwa umma kuachana na dhana kwamba vikoba ni kwa ajili ya wanawake pekee, akisema ni kwa watu wote wenye maono ya kuinuana kiuchumi.

















KIKUNDI cha Vision Vikoba ambacho ni kikundi mama cha vikundi 13) kimeadhimisha miaka 10 tangu kuanzishwa kwake, ambapo mshikamano na mshikamanifu wa kijamii umetajwa kuwa siri ya mafanikio yaliyowezesha kuendelea kwao hadi leo.
Akizungumza katika hafla ya maadhimisho hayo jijini Dar es Salaam, Mwanzilishi wa Vision Vikoba, Bi. Sharifa Mohamed, alisema walipoanza walikuwa na ndoto ya kuunda eneo la mshikamano na kusaidiana, lakini sasa ndoto hiyo imezaa matunda makubwa.
“Kikundi chetu mama kilikuwa kama mbegu, na vikundi 13 vilivyochipuka leo hii ni kama miti yenye matunda mema. Hii ndiyo maan a ya mshikamano na mshikamanifu wa kijamii,” alisema.
Kwa mujibu wake, kikundi kina jumla ya wanachama 314, ambapo asilimia 80 ni wanawake na asilimia 20 ni wanaume, huku dira ikiwa ni kukua zaidi na kugeuka kuwa vyama vya ushirika, taasisi za kifedha na hata kushiriki katika miradi ya kijamii.
Aidha, ameiomba Serikali kuendelea kuweka mazingira rafiki ya uwekezaji kwa wajasiriamali wadogo, akisema vikoba vimekuwa darasa la kujitegemea kiuchumi na kusaidia familia nyingi.
Akihutubia katika maadhimisho hayo, Katibu Tawala wa Wilaya ya Kinondoni, Bi. Warda Abdallah, amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika ofisi za wakuu wa wilaya ili kuchangamkia mikopo nafuu ya asilimia 10 inayotolewa na Serikali.
Amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imetoa fedha nyingi kwa wananchi ili kuwawezesha kujikomboa kutoka katika umaskini.
“Mkiwa mnajuana kitabia ni rahisi kuepusha migogoro. Changamkieni fursa hizi ili muondokane na umaskini,” alisema Bi. Warda.
Mwenyekiti wa Smart Vikoba Endelevu, Bi. Dainess Kalinga, amesema kupitia vikoba ameweza kununua ardhi, pikipiki na kuendesha biashara zake huku akisisitiza upendo na heshima kama nguzo ya kikundi.
Mdau kutoka Bakhresa Food Products, Bi. Rehema Salim, amesisitiza nidhamu ya fedha na mshikamano kama silaha ya vikoba endelevu.
Kwa upande wake, mwanachama Shedrack Sheria alitoa rai kwa umma kuachana na dhana kwamba vikoba ni kwa ajili ya wanawake pekee, akisema ni kwa watu wote wenye maono ya kuinuana kiuchumi.


















Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...