Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) limeshiriki maonesho ya Nane ya Teknolojia ya Madini yanayofanyika katika viwanja vya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan vilivyopo mkoani Geita kuanzia tarehe 18 hadi 28 Septemba, 2025.
Wadau mbalimbali wametembelea banda la TASAC na kupata elimu ya ugomboaji wa bidhaa ikiwemo makinikia, vilipuzi na madawa yanayotumika kwenye migodi ya uchumbaji wa madini, elimu ya usalama, ulinzi wa vyombo vya usafiri majini na utunzaji wa mazingira ambamo vyombo vinafanyakazi imetolewa
TASAC imekuwa ikitumia fursa ya maonesho hayo kutoa elimu ya umuhimu wa huduma za usafirishaji majini, usalama wa vyombo vya usafiri majini, pamoja na fursa za biashara zinazopatikana kupitia sekta ya usafiri kwa njia ya maji
Aidha, Wadau waliotembelea banda hilo wamepongeza jitihada za Shirika katika kuelimisha Umma na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa kupitia usafirishaji wa majini.





Wadau mbalimbali wametembelea banda la TASAC na kupata elimu ya ugomboaji wa bidhaa ikiwemo makinikia, vilipuzi na madawa yanayotumika kwenye migodi ya uchumbaji wa madini, elimu ya usalama, ulinzi wa vyombo vya usafiri majini na utunzaji wa mazingira ambamo vyombo vinafanyakazi imetolewa
TASAC imekuwa ikitumia fursa ya maonesho hayo kutoa elimu ya umuhimu wa huduma za usafirishaji majini, usalama wa vyombo vya usafiri majini, pamoja na fursa za biashara zinazopatikana kupitia sekta ya usafiri kwa njia ya maji
Aidha, Wadau waliotembelea banda hilo wamepongeza jitihada za Shirika katika kuelimisha Umma na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa kupitia usafirishaji wa majini.





Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...