Wanachama wa TUGHE Zaidi ya 800 wamefanya utalii wa ndani kwa kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro siku ya Alhamisi tarehe 18 Septemba 2025 kwa lengo la kuunga mkono juhudi za kukuza utalii wa ndani na kutambua fursa za uwekezaji katika sekta ya utalii.

Katika ziara hiyo, wageni walipata nafasi ya kuona vivutio mbalimbali vikiwemo maporomoko ya maji, mimea ya kipekee na mandhari ya Mlima Kilimanjaro maarufu kama “Paa la Afrika”.

Katibu wa TUGHE, Hery Mkunda, alisema kuwa ziara hiyo imewapa uelewa mkubwa zaidi wa thamani na uzuri wa urithi wa dunia.

Naibu Kamishna wa Uhifadhi TANAPA, Steria Ndaga, aliwapongeza TUGHE kwa kuunga mkono utalii wa ndani, akibainisha kuwa kutembelea hifadhi kunasaidia kuongeza pato la taifa na ajira kwa vijana.

Naye Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi TANAPA, Jully Bede Lyimo, aliongeza kuwa utalii wa ndani una faida nyingi zikiwemo kuongeza mapato, kuchochea ajira, kukuza biashara ndogo ndogo na kujenga uzalendo wa taifa.

Kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Hifadhi ya Kilimanjaro, Amri Mtekanga, aliwakaribisha wageni hao na kuwaeleza vivutio pamoja na taratibu za kupanda Mlima Kilimanjaro.

Ziara hiyo ya TUGHE imedhihirisha mshikamano wa Watanzania katika kuunga mkono sekta ya utalii kuelekea maadhimisho ya Siku ya Utalii Duniani.








Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...