Na Mwandishi Wetu, Handeni

Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, amewataka wawekezaji wa migodi ya madini kuhakikisha wanazingatia kikamilifu kanuni na miongozo ya usalama ili kuepusha ajali zinazoweza kuzuilika.

Akizungumza wakati wa ziara ya kutembelea mgodi wa dhahabu wa GSB uliopo Kilima Mzinga, Halmashauri ya Wilaya ya Handeni, Mhe. Nyamwese amesema ni jukumu la kila mwekezaji kulinda maisha ya watu pamoja na mazingira ya maeneo wanayofanyia kazi.

Amesema Wilaya ya Handeni ina hazina kubwa ya fursa za maendeleo na kwamba mshikamano wa wananchi, wawekezaji na serikali unaweza kuigeuza kuwa kitovu cha uzalishaji, ajira na ustawi wa jamii.

Katika hatua nyingine, Mhe. Nyamwese amempongeza mwekezaji huyo kwa uamuzi wa kuwekeza Handeni, akibainisha kuwa hatua hiyo itafungua milango ya ajira na kuchochea maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi.

Aidha, ameahidi kuendelea kushirikiana kwa karibu na wawekezaji ili kuhakikisha changamoto za miundombinu, hususan upatikanaji wa umeme wa uhakika na maji, zinapatiwa suluhisho la kudumu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...