Kampuni ya Startimes imezindua kampeni mpya iitwayo Zote Ndani, ikiwapa watazamaji ofa maalum kupitia vipindi mbalimbali vya burudani, michezo, tamthilia na vipindi vya watoto.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi, Meneja Masoko wa Startimes, David Malisa, alisema kampeni hiyo inaleta vipindi vya kipekee sambamba na michezo ya kimataifa itakayorushwa kupitia kisimbuzi cha Startimes.

“Tumejipanga kuonesha mechi kali kutoka Ligi Kuu ya England, La Liga na Bundesliga kupitia kisimbuzi chetu cha familia,” amesema Malisa.

Mbali na michezo, Startimes pia imetambulisha tamthilia mbili kubwa kutoka Uturuki ambazo zimetafsiriwa kwa Kiswahili, ikiwemo Shadel T na Sagado Hadel Queen.

Kwa upande wake, Godfrey Lugalabamu maarufu kama ‘Mc Gara B’, amesema msimu mpya wa Hello Mr. Right utarejea na maudhui mapya yenye msisimko.

“Nimekuwa sehemu ya Hello Mr. Right tangu msimu wa kwanza. Baada ya kupumzika msimu wa sita, mashabiki walitaka nirejee—na sasa natangaza rasmi kwamba nimerudi kwa ajili ya kuzalisha mahusiano mapya. Msimu huu wa saba utakuwa na mambo mengi ya kushangaza,” amesema Mc Gara B.

Naye, Maimartha Jesse, mmoja wa watangazaji wa kipindi hicho, alisisitiza umuhimu wa washiriki kuwa wazi kwa familia zao kabla ya kushiriki.

“Washiriki wanapokuja Hello Mr. Right tunawahimiza wazungumze na wazazi wao mapema, kwani nia ya shindano hili ni kuona watu wakikutana, kupendana na hatimaye kufunga ndoa. Pia tunahakikisha wanapima afya kabla ya kuingia kwenye mahusiano ya ndoa,” amesema Maimartha.

Kwa upande wa vipindi vya watoto, Startimes imetangaza kuonesha katuni mpya kupitia ist Kids, ikiwemo Mbabe, sambamba na ofa mbalimbali na punguzo la bei kwa kisimbuzi cha familia.

Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...