Na Mwandishi Wetu
MGOMBEA mwenza wa Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Emmanuel John Nchimbi amehitimisha mikutano yake ya hadhara ya kampeni katika Mkoa wa Tabora huku akiacha ujumbe kuwa ifikapo Oktoba 29 mwaka huu wananchi wa mkoa huo wampigie kura mgombea urais wa Chama hicho Dk.Samia
Suluhu Hassan.
Dk.Nchimbi amehitisha ziara leo Oktoba 6, 2025 katika Mkoa wa Tabora ambapo katika mikutano ya kampeni mbali ya kumuombea kura mgombea urais Dk.Samia Suluhu Hassan, wabunge na madiwani pia ametumia mikutano hiyo kunadi sera na Ilani ya uchaguzi mkuu ambayo imelenga kuleta maendeleo ya watanzaniaL
Akiwa katika mkutano wa kampeni Dk.Nchimbi kabla ya kuanza kuwahutubia Wananchi amesimikwa kuwa msaidizi wa Mtemi, kimila akiitwa 'MTONGI' baada ya mkubwa wake Chifu Hangaya ambaye ni Raisi Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Dkt. Nchimbi amesimikwa na viongozi wa kimila wa Unyanyembe (Tabora) kwenye mkutano wake wa mwisho wa kampeni mkoani humo,katika kata ya Kigwa jimbo la Igalula, wilaya ya Uyui nakupewa jina la "NYUNGU YA MAWE".
Pamoja na mambo mengine,Dkt.Nchimbi aliwanadi wagombea Ubunge wa mkoa huo akiwemo mgombea Ubunge wa jimbo la Igalula, Ndugu Juma Ramadhan Mustafa [KAWAMBA) pamoja na Madiwani.
Aidha Dkt.Nchimbi pia alitumia nafasi hiyo kuwaomba wampigie kura za ushindi wa kishindo Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani,Dkt.Samia Suluhu Hassan,Wagombea Ubunge na Madiwani kwa ujumla.
Balozi Nchimbi anafikia mkoa wa 18 sasa tangu kuzinduliwa kwa kampeni hizo Oktoba 28,2025 jijini Dar es Salaam,akiendelea kusaka kura za ushindi wa kishindo za Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan,Wabunge na Madiwani.











MGOMBEA mwenza wa Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Emmanuel John Nchimbi amehitimisha mikutano yake ya hadhara ya kampeni katika Mkoa wa Tabora huku akiacha ujumbe kuwa ifikapo Oktoba 29 mwaka huu wananchi wa mkoa huo wampigie kura mgombea urais wa Chama hicho Dk.Samia
Suluhu Hassan.
Dk.Nchimbi amehitisha ziara leo Oktoba 6, 2025 katika Mkoa wa Tabora ambapo katika mikutano ya kampeni mbali ya kumuombea kura mgombea urais Dk.Samia Suluhu Hassan, wabunge na madiwani pia ametumia mikutano hiyo kunadi sera na Ilani ya uchaguzi mkuu ambayo imelenga kuleta maendeleo ya watanzaniaL
Akiwa katika mkutano wa kampeni Dk.Nchimbi kabla ya kuanza kuwahutubia Wananchi amesimikwa kuwa msaidizi wa Mtemi, kimila akiitwa 'MTONGI' baada ya mkubwa wake Chifu Hangaya ambaye ni Raisi Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Dkt. Nchimbi amesimikwa na viongozi wa kimila wa Unyanyembe (Tabora) kwenye mkutano wake wa mwisho wa kampeni mkoani humo,katika kata ya Kigwa jimbo la Igalula, wilaya ya Uyui nakupewa jina la "NYUNGU YA MAWE".
Pamoja na mambo mengine,Dkt.Nchimbi aliwanadi wagombea Ubunge wa mkoa huo akiwemo mgombea Ubunge wa jimbo la Igalula, Ndugu Juma Ramadhan Mustafa [KAWAMBA) pamoja na Madiwani.
Aidha Dkt.Nchimbi pia alitumia nafasi hiyo kuwaomba wampigie kura za ushindi wa kishindo Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani,Dkt.Samia Suluhu Hassan,Wagombea Ubunge na Madiwani kwa ujumla.
Balozi Nchimbi anafikia mkoa wa 18 sasa tangu kuzinduliwa kwa kampeni hizo Oktoba 28,2025 jijini Dar es Salaam,akiendelea kusaka kura za ushindi wa kishindo za Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan,Wabunge na Madiwani.











Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...