Na Mwandishi Wetu, Barcelona – Hispania

Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro (NCAA) na Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) wameendeleza jitihada za kuitangaza Tanzania kimataifa kupitia ushiriki wao katika maonesho ya utalii (Tourism Road Show) yanayofanyika nchini Hispania.

Onesho hilo lililoandaliwa na kampuni ya usimamizi wa safari (DMC) yenye makao makuu yake nchini Tanzania, (Tanganyika Expeditors) na kufanyika jijini Barecelona Oktoba 06, 2025 , limewaleta pamoja wadau mbalimbali wa sekta ya utalii wakiwemo mawakala wa safari za kitalii pamoja na wawekezaji kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya jiji hilo. 

Kupitia ushiriki huo, NGORONGORO na TANAPA zimepata fursa kutoa taarifa muhimu za kuwasaidia mawakala wa usafiri kuandaa safari kwa wageni wanaotaka kutembelea Tanzania kujionea vivutio mbalimbali vinavyopatikana hifadhi ya  Ngorongoro na Hifadhi za taifa kama vile Serengeti, Manyara, Tarangire na maeneo mengine ya kipekee yanayosimamiwa na taasisi hizo.

Mbali na NCAA na TANAPA, washiriki wengine kutoka Tanzania ni pamoja na Miracle Experience -Tanzania, Auram Treks, Karafuu Beach Resort and Spa na Malia Hotels International.

Maonesho hayo ya Tourism Road Show yaliyoanza leo tarehe 6 Oktoba yataendelea kufanyika katika majiji mengine ya Hispania, ikiwemo Madrid na Seville ambapo yanatajiwa kuhitimishwa tarehe 8 Oktoba, 2025.







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...