SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) Kanda ya Kati, Dodoma, limeteketeza jumla ya tani 1.53 za bidhaa za chakula ambazo hazijakidhi matakwa ya viwango, zikiwemo zilizokwisha muda wa matumizi.
Akizungumza wakati wa zoezi hilo lililofanyika Oktoba 11, 2025, Afisa Udhibiti Ubora wa TBS Kanda ya Kati, Daniel Marwa, alisema bidhaa hizo zenye thamani ya shilingi milioni 8.11 zilikamatwa katika ukaguzi mbalimbali uliofanyika kati ya Julai hadi Oktoba 2025 katika mikoa ya Dodoma, Singida na Iringa.
Marwa alisema hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za TBS kulinda afya za watumiaji na kuhakikisha bidhaa zote zinazouzwa sokoni zinakidhi viwango vilivyowekwa kisheria.



Akizungumza wakati wa zoezi hilo lililofanyika Oktoba 11, 2025, Afisa Udhibiti Ubora wa TBS Kanda ya Kati, Daniel Marwa, alisema bidhaa hizo zenye thamani ya shilingi milioni 8.11 zilikamatwa katika ukaguzi mbalimbali uliofanyika kati ya Julai hadi Oktoba 2025 katika mikoa ya Dodoma, Singida na Iringa.
Marwa alisema hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za TBS kulinda afya za watumiaji na kuhakikisha bidhaa zote zinazouzwa sokoni zinakidhi viwango vilivyowekwa kisheria.




Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...