Na Mwandishi Wetu

JUBILEE Insurance (Jubilee Life na Jubilee Health) leo Novemba  17,2025 wamezindua rasmi ofisi yao mpya iliyopo ghorofa ya tatu jengo la Faykat Tower. 

Uzinduzi wa ofisi hiyo mpya ni muendelezo wa ahadi yao ya kuendelea kutoa huduma bora za bima ya Afya na bima ya Maisha kwa Watanzania.

Taarifa yake kwa vyombo vya habari iliyotolewa leo imesema kwamba Jubilee Insurance inawakaribisha mawakala na wateja wake kutembelea ofisi hizo kwa msaada zaidi kuhusu maswala ya bima.

Katika uzinduzi huo mbali ya kuhudhuriwa na waalikwa mbalimbali pia alikuwepo Ofisa Mtendaji Mkuu wa Jubilee Health Insurance Dk.Harold Adamson pamoja na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Jubilee Life Insurance Bi. Helena Mzena.

Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...