Farida Mangube, Morogoro

Zoezi la kuchukua fomu za kugombea nafasi ya Umeya na Naibu Meya wa Manispaa ya Morogoro kwa tiketi ya chama Cha Mapinduzi (Ccm) limefunguliwa leo huku mwandishi wa Habari wa Gazeti la Uhuru mkoa wa Morogoro Latifa Ganzeli akichukua fomu ya kuwania unaibu meya wa Manispaa ya Morogoro.

Akizungumzia zoezi hilo,Katibu wa Umoja wa Vijana(UVCCM)Wilaya ya Morogoro mjini Khalid Hossein King amesema kuwa zoezi Hilo linatarajiwa kukamilika Novemba 21 majira ya saa kumi jioni huku muitikio ukiwa mkubwa kwa wanachama waliojitokeza kuchukua fomu hizo.

Akizungumza mara baada ya kuchukua fomu ya kugombea Unaibu Meya wa Manispaa ya Morogoro,Diwani wa Viti maalumu ambaye pia ni mwandishi wa habari wa Gazeti la Uhuru,Latifa Ganzeli amesema kuwa baada ya kulitumikia baraza la Madiwani kwa muda wa miaka 10 ameona sasa ni wakati muafaka wa kugombea nafasi hiyo huku kipaumbele chake kikubwa kikiwa kwenda kuongeza vyanzo vipya vya mapato.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...