Na Mwandishi Wetu

KIONGOZI Mkuu wa Kanisa la Ngurumo ya Upako Jijini Arusha, Nabii Mkuu GeorDavie Moses, ameteuliwa kuwa Mwakilishi na Balozi wa Amani wa Afrika Mashariki kupitia Shirika la Mabalozi wa Amani la Umoja wa Mataifa (UN-PAF) lenye makao yake makuu Jijini New York, Marekani.

Taarifa kutoka Marekani zinaeleza kuwa uteuzi huo ulifanywa rasmi na Mwenyekiti wa Dunia wa UN-PAF, Balozi Kingsley Ossai, ambaye ametuma barua maalumu za utambulisho kwa Serikali ya Tanzania, United Nations Chapter ya Tanzania pamoja na Ubalozi wa Marekani nchini, kwa lengo la kumtambulisha Nabii GeorDavie katika wadhifa wake mpya.

“Tunatambua mchango wa Nabii GeorDavie katika kueneza amani na maendeleo ya kijamii. Tunaamini kama Balozi wa Amani Duniani, ataziwakilisha vema nchi za Afrika Mashariki kupitia Shirika letu,” imeeleza sehemu ya barua hiyo.

Nabii Mkuu GeorDavie, ambaye pia ni mlezi wa JMAT Taifa, amekuwa akihusishwa kwa muda mrefu na shughuli za kijami.




Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...