Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kupitia Shamba la Miti Wino wamemaliza Bonanza la Michezo la TFS, lililowakutanisha timu nane kutoka kata tatu za Halmashauri ya Wilaya ya Madaba, kwa lengo la kuelimisha wananchi kuhusu uhifadhi wa misitu, madhara ya moto na kuwapa vijana nafasi ya kuonesha vipaji.

Katika mchezo wa fainali, TFS Wino walitwaa ubingwa baada ya kuifunga Magingo FC kwa mikwaju ya penalti, kufuatia sare tasa ndani ya dakika 90.

Akizungumza wakati wa hitimisho la bonanza hilo Jana Novemba 25,2025, Mkuu wa Wilaya ya Songea, Wilman Kapenjama, alisema mashindano hayo ni zaidi ya burudani kwa kuwa yanatumika kutoa elimu muhimu ya uhifadhi.

Alisema misitu ni mhimili wa uchumi wa kijani, akawataka wananchi kuachana na matumizi ya moto kwenye maandalizi ya mashamba hususan msimu huu wa kilimo, kwani husababisha uharibifu wa rasilimali na mazingira.

Kwa upande wake, Mhifadhi Muandamizi wa Shamba la Miti Wino, Glory Kasmir, alisema bonanza hilo ni njia shirikishi ya kuwaunganisha wananchi na TFS kupitia elimu ya ulinzi wa misitu, mbinu salama za maandalizi ya mashamba na udhibiti wa moto misituni, sambamba na kuinua vipaji vya michezo kwa vijana.

Baadhi ya wakazi na washiriki wa mashindano hayo walisema elimu waliyoipata itawasaidia kuimarika kiuchumi kupitia kilimo salama na shughuli rafiki kwa mazingira, huku wakiahidi kuwa mabalozi wa uhifadhi katika vijiji vyao kwa kutekeleza mafunzo ya TFS katika maisha ya kila siku.














Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...