Na. Joseph Mahumi, WF, Dodoma
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-Maamry Mwamba, amekutana na kufanya mazungumzo na Naibu Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia masuala ya Watoto (UNICEF) anayehusika na Programu, Bi. Patricia Safi Lombo, ambapo wamejadili kuhusu namna ya kuendeleza ushirikiano kati ya Serikali na Shirikika hilo hususan maendeleo ya huduma za jamii.
Dkt. Mwamba alisisitiza dhamira ya Serikali ya kuendelea kushirikiana na UNICEF katika kutekeleza miradi inayolenga kuinua ustawi wa jamii na kukuza maendeleo ya kiuchumi nchini.
Kwa upande wake, Bi. Patricia Safi Lombo, aliyefika kujitambulisha, Treasury Square jijini Dodoma, aliipongeza Serikali ya Tanzania kwa hatua kubwa ilizopiga katika kusimamia sekta za kijamii, na kuahidi kuendeleza ushirikiano wa karibu zaidi katika utekelezaji wa programu za maendeleo zenye tija kwa Watoto.
Mazungumzo hayo yalihitimishwa kwa pande zote mbili kueleza nia ya kuimarisha zaidi uhusiano uliopo, kupitia mipango bunifu inayochochea ustawi wa watoto, vijana na jamii kwa ujumla, sambamba na malengo ya maendeleo endelevu (SDGs).
Dkt. Mwamba alisisitiza dhamira ya Serikali ya kuendelea kushirikiana na UNICEF katika kutekeleza miradi inayolenga kuinua ustawi wa jamii na kukuza maendeleo ya kiuchumi nchini.
Kwa upande wake, Bi. Patricia Safi Lombo, aliyefika kujitambulisha, Treasury Square jijini Dodoma, aliipongeza Serikali ya Tanzania kwa hatua kubwa ilizopiga katika kusimamia sekta za kijamii, na kuahidi kuendeleza ushirikiano wa karibu zaidi katika utekelezaji wa programu za maendeleo zenye tija kwa Watoto.
Mazungumzo hayo yalihitimishwa kwa pande zote mbili kueleza nia ya kuimarisha zaidi uhusiano uliopo, kupitia mipango bunifu inayochochea ustawi wa watoto, vijana na jamii kwa ujumla, sambamba na malengo ya maendeleo endelevu (SDGs).
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-Maamry Mwamba, akizungumza jambo wakati alipokutana na Naibu Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Watoto (UNICEF) anayehusika na Programu, Bi. Patricia Safi Lombo (hayupo pichani), ofisini kwake, Treasury Square, jijini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-Maamry Mwamba (Watatu kulia) na Naibu Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Watoto (UNICEF) anayehusika na Programu, Bi. Patricia Safi Lombo (wa nne kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja na maafisa waandamizi wa Wizara ya Fedha pamoja na UNICEF, baada ya kukutana na kufanya mazungumzo, Ofisi za Wizara ya Fedha, jijini Dodoma.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Dodoma)







Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...