Na Munir Shemweta, WANMM MTWARA
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo leo tarehe 22 Desemba 2025 amekutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Sawala.
Mhe. Dkt Akwilapo ambaye yuko ziarani mkoani Mtwara amemueleza Kanali Sawala juhudi za wizara yake katika kushughulikia changamoto za sekta ya ardhi nchini.
"Sisi kama wizara tutazifanyia kazi changamoto zote za sekta ya ardhi na hapa Mtwara tayari tumeshaanza kuzifanyia kazi, lengo ni kutaka kuwaacha wananchi wetu wawe na furaha". Amesema
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Sawala amempongeza Mhe. Dkt Akwilapo kwa kuaminiwa na Rais Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kuteuliwa kuwa Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi wizara aliyoieleza kuwa ni nyeti kutokana na kugusa maisha ya kila mtu.
"Nikuahidi Mhe. Waziri sisi kama mkoa tutajitahidi kukusemea kwa yale yote mazuri unayofanya katika mkoa wetu". Amesema Kanali Sawala.

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo (kushoto) akisisitiza jambo wakati akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Patrick Sawala alipomtembelea ofisini kwake mkoani Mtwara tarehe 22 Desemba 2025.

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo (kushoto) akimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Patrick Sawala alipomtembelea ofisini kwake mkoani Mtwara tarehe 22 Desemba 2025.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo (Kulia) akioongozana na mwenyeji wake Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Patrick Sawala mara baada ya mazungumzo yao alipomtembelea ofisini kwake mkoani Mtwara tarehe 22 Desemba 2025.




Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...