Na Mwandishi Wetu
KATIBU wa Halmashauri Kuu(NEC)ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Itikadi, Uenezi na Mafunzo Kenan Kihongosi amefanya kikao kazi na viongozi mbalimbali wa Chama hicho pamoja na wasanii wa Bendi ya TOT.
Kihongosi amefanya kikao kazi hicho leo katika Ofisi ndogo za Chama Cha Mapinduzi(CCM) zilizopo Lumumba jijini Dar es Salaam ambapo katika kikao hicho ametumia nafasi hiyo kuelezea mipango na mikakati mbalimbali yenye lengo la kuiimarisha Chama hicho.
Aidha Kenan amewahakikishia viongozi walioshiriki kikao kazi hicho kwamba anatambua kazi kubwa na nzuri ambayo wameifanya kipindi chote cha kampeni za Uchaguzi Mkuu 2025 napia kwa lengo la kukifanya Chama Cha Mapinduzi kuendelea kuwatumikia wananchi ambao wamekuwa na matumaini makubwa na Chama hicho chini ya Mwenyekiti wao Rais Dk.Samia Suluhu Hassan.








Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...