Na Mwandishi Wetu

KATIBU wa Halmashauri Kuu(NEC)ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Itikadi, Uenezi na Mafunzo Kenan Kihongosi amefanya kikao kazi na viongozi mbalimbali wa Chama hicho pamoja na wasanii wa Bendi ya TOT.

Kihongosi amefanya kikao kazi hicho leo katika Ofisi ndogo za Chama Cha Mapinduzi(CCM) zilizopo Lumumba jijini Dar es Salaam ambapo katika kikao hicho ametumia nafasi hiyo kuelezea mipango na mikakati mbalimbali yenye lengo la kuiimarisha Chama hicho.

Aidha Kenan amewahakikishia viongozi walioshiriki kikao kazi hicho kwamba anatambua kazi kubwa na nzuri ambayo wameifanya kipindi chote cha kampeni za Uchaguzi Mkuu 2025 napia kwa lengo la kukifanya Chama Cha Mapinduzi kuendelea kuwatumikia wananchi ambao wamekuwa na matumaini makubwa na Chama hicho chini ya Mwenyekiti wao Rais Dk.Samia Suluhu Hassan.








Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...