Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), imetembelewa na Kamati ya Bunge ya Miundombunu na kupongezwa kwa jitihada zake za kuisimamia na kuiendeleza sekta ya usafiri wa anga nchini.

Kamati hiyo ya Bunge ya Miundombinu ilifanya ziara hiyo mnamo Februari 16, 2026 katika Makao Makuu ya TCAA yaliyopo Banana-Ukonga jijini Dar es Salaam.

Ziara hiyo iliongozwa na Kaimu Mwenyekiti wa Kamati na Mbunge wa Jimbo la Bukoba Mjini, Mhandisi Johnston Mutasingwa, kwa niaba ya Mwenyekiti Selemani Kakoso.

Ziara hiyo ya kikazi ilikuwa na lengo la kujua shughuli zinazofanywa na Mamlaka katika utekelezaji wa majukumu yake ya ki udhibiti .

Kamati hiyo iliihimiza TCAA kuendelea kumsimamia kikamilifu mkandarasi anayetekeleza Mradi wa ujenzi wa Majengo ya Kisasa ya Chuo cha Usafiri wa Anga (CATC) ili kuhakikisha ujenzi huo unakamilika kwa wakati na kwa viwango vilivyokubalika.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Uchukuzi, Mhe. David Kihenzile aliyeongozana na kamati hiyo, alibainisha kuwa Serikali ya Awamu ya Sita imejikita katika kuboresha sekta ya usafiri wa anga kupitia ujenzi, ukarabati na upanuzi wa miundombinu ya anga pamoja na kuimarisha mifumo ya usimamizi. Alisema jitihada hizo zinategemea nguvu kazi yenye ujuzi mkubwa, na kwamba CATC, kwa kushirikiana na TCAA, ni nguzo muhimu katika kuzalisha wataalamu watakaoiwezesha sekta ya usafiri wa anga kukua kwa kasi na kwa usalama.

Kwa upande wa TCAA kamati hiyo ilipokewa na Mwenyekiti wa Bodi wa TCAA Dkt. Hamisi Mwinyimvua na kisha kupokea taarifa ya utendaji kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa TCAA Bw. Salim Msangi.
Kaimu Mwenyekiti wa Kamati na Mbunge wa Jimbo la Bukoba Mjini, Mhandisi Johnston Mutasingwa akizungumza akizungumza na menejimenti na watumishi wakati wa ziara ya kamati hiyo ilipotembelea Makao Makuu ya TCAA yaliyopo Banana-Ukonga jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Uchukuzi, Mhe. David Kihenzile akizungumza kuhusu Serikali ya Awamu ya Sita imejikita katika kuboresha sekta ya usafiri wa anga wakati wa ziara ya Kamati ya Bunge ya Miundombunu aliyotembelea Makao Makuu ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) yaliyopo Banana-Ukonga jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi wa TCAA Dkt. Hamisi Mwinyimvua akizungumza jambo wakatiwa  ziara ya Kamati ya Bunge ya Miundombunu aliyotembelea Makao Makuu ya TCAA.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Salim Msangi akitoa taarifa kuhusu kazi mbalimbali zinazofanywa na Mamlaka hiyo kwa  Kamati ya Bunge ya Miundombunu ilipotembelea Makao Makuu ya TCAA yaliyopo Banana-Ukonga jijini Dar Es Salaam.
Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu wakiuliza maswali pamoja na kuchangia hoja mara baada ya kuwasilisha taarifa ya kazi zinazofanywa na TCAA


Wajumbe wa kamati ya Bunge ya Miundombinu, menejimenti na watumishi wa TCAA wakiwa kwenye kikao kilichofanyika  Makao Makuu ya TCAA yaliyopo Banana-Ukonga.
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Bi. Mtumwa Khatib Ameir akitoa neno la shukrani kwa Kamati ya Bunge ya Miundombinu ilipotembelea ofisi za TCAA zilizopo Banana-Ukonga. jijini Dar es Salaam.
Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...