NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) kwa kushirikiana na Tume ya Ushindani (FCC) wamekutana na wadau wa bidhaa za pombe nchini kwa lengo la kuwajengea uelewa juu ya matakwa ya sheria, kanuni na viwango vinavyosimamia sekta hiyo.

Kikao hicho kilichofanyika leo Machi 27, 2026 jijini Dar es Salaam, pia kimelenga kujadiliana na kubaini changamoto zinazowakabili wadau katika kukidhi matakwa ya kisheria pamoja na masuala ya ushindani, ili kupata ufumbuzi wake.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao hicho, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Mhandisi Yona Afrika, amesema kumekuwa na malalamiko yanayopokelewa na taasisi hizo kuhusu uwepo wa pombe duni na bandia katika soko, hali inayochangiwa na baadhi ya wafanyabiashara wasio waaminifu.

“Bidhaa hizi zisipozingatia matakwa yaliyowekwa, zinaweza kuhatarisha afya na usalama wa walaji,” amesema Afrika.

Ameongeza kuwa TBS kwa kushirikiana na FCC zitaendelea kuimarisha usimamizi wa viwango ili kudhibiti ubora wa bidhaa pamoja na kuhakikisha ushindani wa haki katika soko.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi.Roberta Feruzi, amesema uwepo wa pombe duni na bandia si tu unaharibu ushindani wa haki bali pia husababisha malalamiko kutoka kwa walaji kuhusu thamani ya fedha wanazolipa na athari za kiafya.

Amebainisha kuwa hali hiyo pia hudhoofisha biashara halali na kuvuruga mazingira ya ushindani sawa kwa wafanyabiashara wanaofuata sheria.







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...