Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro linamshikilia Charles Hirali Msangi (34) kwa tuhuma za kusababisha ajali iliyosababisha abiria 57 kunusurika kifo katika eneo la Mikumi, kando ya barabara kuu ya Mikumi–Ifakara.

Ajali hiyo ilitokea Aprili 16, 2026, ambapo basi lenye namba za usajili T 289 EAG lililokuwa likiendeshwa na mtuhumiwa huyo liliacha njia na kupinduka kutokana na mwendo wa hatari.

Basi hilo lilikuwa likitoka Ifakara kuelekea Dar es Salaam likiwa na jumla ya abiria 57.

Kutokana na ajali hiyo, abiria 13 walijeruhiwa na kupatiwa matibabu katika vituo vya afya vilivyo karibu.

Jeshi la Polisi limetoa wito kwa madereva wote kuzingatia sheria na kanuni za usalama barabarani ili kuzuia ajali zinazoweza kuepukika.

Imeandaliwa na Farida Mangube.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...