Na Farida Mangube Morogoro 

Kemikali inayodaiwa kuwa ni sulphur imemwagika  baada ya gari yenye namba za usajili T196 EMU  mali ya kampuni ya Alhushum  lililokuwa libeba kemikali hiyo kuacha kuacha njia na kugonga miti barabara kuu ya Morogoro–Iringa, karibu kabisa na Bwawa la Mindu.

Michuzi Tv imefika eneo la tukio na kushuhudia jitihada  za dharura zikifanyika kuzuia kemikali hiyo isiingie kwenye bwawa la Mindu iwapo Mvua ikinyesha na kuhatarisha maisha ya wakazi wa Manispaa ya Morogoro ambao asilimia 75 wanategemea maji safi na Salama kutoka kwenye bwawa hilo.

Mamlaka mbalimbali nimefika Katika eneo hilo zikiwemo NEMC, Bonde la Wami-Ruvu, MORUWASA na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji zikiratibu operesheni ya kudhibiti hali hiyo. Hata hivyo, wataalamu kutoka mamlaka hizo wamekataa kuzungumzia tukio hilo kwa kina wakieleza kuwa kipaumbele chao kwa sasa ni kuokoa hali.

Kwa upande wa Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali Kanda ya Kati imesema wataalamu wake wako njiani kutoka Dodoma na watazungumzia tukio hilo baada ya kufika eneo husika.

Hadi majira ya saa Moja na nusu  usiku mwandishi wa michuzi Tv anaondoka Katika eneo la tukio Bado jitihada za kuzuia kemikali hiyo isiingie kwenye mitaro inayotiririsha maji kuelekea bwawani zilikuwa zinaendelea, awali zikihusisha nguvu kazi ya watu kabla ya kuwasili kwa mitambo mizito kusaidia kazi hiyo.






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...