MAMLAKA ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) imewatangazia waingizaji wa mizigo mikubwa ya forodha ya bidhaa za Dawa, Vifaa Tiba na Vitendanishi nchini, kuwa mifumo ya TANCIS-TRA na RIMS-TMDA imeunganishwa ili kuongeza ufanisi katika kuingiza na kutoa shehena za bidhaa hizo nchini kwa njia ya kielektroniki.  

Kwa mujibu wa taarifa kwa Umma iliyotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa TMDA, Dk. Adam Fimbo ameeleza kuwa, Lengo kuu la muunganiko huo ni kurahisisha michakato ya uombaji vibali kuwa na sehemu moja ya kuingiza taarifa, pamoja na kuboresha ufuatiliaji na shughuli za udhibiti wa maombi ya kuingiza na kutoa bidhaa nchini.

"Mnajulishwa rasmi kuwa kuanzia tarehe 1 Mei, 2026 maombi yote yaliyokuwa yanapitia TMDA-RIMS na TRA-Forodha kwa ajili ya kutolea taarifa (declaration) yatafanyika moja kwa moja katika mfumo wa TANCIS.  

Ili kuepusha Hoja zisizo za lazima na kurahisisha huduma za upatikanaji wa vibali, mnakumbushwa kuzingatia; Usahihi wa taarifa za bidhaa zinazosimamiwa na TMDA (ikijuimuisha namba za usajili za bidhaa na majengo); na Wadau wote watatakiwa kushirikiana na Wakala wa Forodha kwa ukaribu ili kuthibitisha usahihi wa taarifa za kitaalam na nyaraka hitajika." Imeeleza taarifa hiyo kwa Umma.

Aidha, TMDA imewataka kuzingatia kuwa, tangazo hilo  linawahusu waingizaji wa mizigo mikubwa ya forodha, na si waingizaji kwa matumizi binafsi (personal use).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...