NA MWANDISHI WETU
BARAZA la Wadhamini la Chama Cha Mapinduzi (CCM) limeeleza kuridhishwa na utekelezaji wa miradi inayotekelelezwa kwa ubia baina ya Chama, jumuiya zake na wadau .
Hayo yameelezwa na wajumbe wa baraza hilo katika ziara ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Dar es salaam leo, inayotekelezwa na CCM, Jumuiya ya Wazazi na Umoja wa wanawake Tanzania (UWT) .
Akizungumza baada ya ziara hiyo ,Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini la CCM, Vuai Ali Vua, amesema CCM ni Chama cha siasa kinacho taka kujitegemea hivyo ili kufikia azama hiyo kinafanya shughuli za kisiasa na kiuchumi.
"Hivyo wito kwa watendaji wetu wa Chama kuanzia ngazi za shina, tawi kata, wilaya mkoa na taifa ni kutumia fursa zilizopo katika taifa letu kupromoti miradi ya CCM kuongeza pato la Chama,"alisema Vuai.
Ameeleza ni wajibu wa watendaji wa CCM na jumuiya zake kuwa wabunifu wa kiuchumi na kisiasa kwani ndiyo aina ya watendaji ambao chama kintegemea kuwa nao katika kipindi hiki.
Akizungumzia a mradi wa jengo la kitega uchumi la Jumiuya ya Wazazi Tanzania katika eneo la Ilala Mchikichini Kiwanja 2C na 2B wenye thamani ya sh. bilioni 2.3, Vuai amesema baraza limeridhishwa na utekelezaji wa mradi huo ambao umesuasua kwa miaka mingi sasa.
Ameshauri Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania, Ally Hapi, kukaa na Kampuni ya MCL ambaye ni mwekezaji wa mradi huo wa ghorofa moja unaohusisha , nyumba za makazi na ofisi kuongeza ghorofa zaidi kutoka ghorofa moja iliyopo.
Awali Mjumbe wa Bodi hiyo, Kapten mstaafu John Chiligati, alishauri kwa kuwa mradi huo ulikusudiwa kujenga ghorofa 20 ambapo msingi wake unaweza kubeba ghorofa hizo ni vyema utekelezaji ukaendelea.
Pia, Mjumbe wa Bodi hiyo, Andrew Chenge, ameshauri Jumuiya ya Wazazi kukaa vyema na wawekezaji Kampuni ya MCL kuhakikisha uwekezaji huo unakuwa endelevu na haushii hapo ili ulete tija zaidi.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania, Fadhili Maganya, amesema kukamilika kwa jengo hilo kumechukua muda mrefu kutokana na migogoro 'mazonge' mbalimbali ambayo hata hivyo ilitatuliwa na utekelezaji kufanyika hatimaye jengo kukamilika.
Katibu wa Jumuiya hiyo, Ally Hapi, amesema amepokea ushauri na maelekezo ya baraza hilo hususan kukaa na Kampuni ya Uwekezaji ya MCL kwaajili ya kuendeleza ujenzi wa jengo hilo kujengwa kwa zaidi ya ghorofa moja .
Bodi hiyo pia ilikagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la kitega uchumi la UWT linalojengwa katika eneo la SUWATA, jijini Dar es Salaam kwa gharama ya sh. bilioni 6 na kupongeza umoja huo kwa hatua hiyo kubwa.
.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...