WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Jumamosi (Mei 9, 2026) ameweka jiwe la msingi la ufunguzi wa soko la mazao Kibakwe, katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa, Mkoa wa Dodoma.

Ujenzi wa soko hilo umelenga kuwawezesha wakulima na wafanyabiashara kupata maeneo rasmi, salama na yenye miundombinu stahiki kwa ajili ya biashara ya mazao yao.

Akizungumza na wananchi baada ya uzinduzi wa soko hilo, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amejitambulisha kuwa kiongozi wa matokeo kwa kutekeleza miradi mbalimbali inayogusa moja kwa moja maisha ya Watanzania

“Mheshimiwa Dkt. Samia ni  mtendaji. Ambaye akisema jambo, anatekeleza. Na haya yanadhihirishwa kwa kazi kubwa ambayo imefanyika”

Mheshimiwa Waziri Mkuu amesema kuwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia amefanya kazi kubwa inayowapa heshima Watanzania wote. “Nchi inapopiga hatua, kwa kazi kubwa inayofanywa Rais wetu, inalinda heshima ya uhuru wa nchi”.







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...