Na Mwandishi Wetu
Serikali
ya Kenya imezindua rasmi kampeni ya kugombea nafasi ya Jaji wa
International Criminal Court kwa kipindi cha mwaka 2027 hadi 2036 kwa
Justice Njoki Ndung’u, hatua inayolenga kuiwakilisha nchi hiyo katika
taasisi ya kimataifa ya utoaji haki.
Akiwa mmoja wa majaji wanaoheshimika nchini Kenya, Jaji Njoki amewahi kuhudumu katika Bunge la Kenya, Bunge la Afrika pamoja na taasisi za United Nations, jambo lililompa uzoefu mpana katika masuala ya sheria ya kimataifa, haki za binadamu na mfumo wa haki ya jinai.
Aidha, ameelezwa kuwa ameonyesha uwezo mkubwa wa kitaaluma katika sheria, uhuru wa kiakili, ujasiri katika kufanya maamuzi na kujitolea katika kusimamia haki na uwajibikaji katika majukumu yake ya kitaifa na kimataifa.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa wakati wa uzinduzi huo, Jaji Njoki anatajwa kuwa na mchanganyiko wa sifa muhimu ikiwemo mamlaka ya kimahakama, uadilifu, uzoefu wa kutunga sheria pamoja na uelewa wa masuala ya kimataifa unaoendana na mahitaji ya ICC katika juhudi zake za kupambana na ukwepaji wa haki duniani.
Hatua hiyo
inatajwa kuwa sehemu ya juhudi za Kenya kuendelea kushiriki katika
kuimarisha taasisi za sheria na haki katika ngazi ya kimataifa.














Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...