MAMIA ya wananchi wamejitokeza kuchangia damu katika kambi maalumu iliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Ukonga, Bakari Shingo, viwanja vya Pugu Kajiungeni, wilayani Ilala, jijini Dar es Salaam, leo.
Kambi hiyo ilianza kwa matembezi ya hisani ya kilometa tano yaliyoanzia Mombasa hadi viwanja vya Pugu yakiongozwa na mbunge huyo na kushiriki, wananchi, vikundi vya jogging na makundi mbalimbali.
Akizungumza katika kambi hiyo, Mbunge Shingo, amesema dhamira ni kuchangisha damu ili kuokoa maisha ya watu hususan wanawake wanao jifungua, waliopata ajali, wagonjwa wa kawaida na wananchi wote wenye matatizo ya kuhitaji damu hospitalini.
Shingo amesema kuchangia damu ni ibada hivyo kuwataka wananchi kuendeleza utamaduni huo bila kujali itikadi zao za kidini na kisiasa.
“Damu hii tunayo change itakwenda kuokoa wananchi wote bila kujali dini zao wala itikadi za kisiasa. Ofisi ya Mbunge Jimbo la Ukonga tunawashukuru wananchi waliojitokeza leo kujitoleaa damu,”amesema Shingo.
Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo, ambaye ni Katibu Tarafa ya Ilala, Kheri William, amempongeza Mbunge Shingo kwa kuandaa kambi hiyo na kuomba utaratibu huo uendelezwe.
“Tunaomba mbunge huu utaratibu ulioanzisha wa kuandaa matembezi na uchangiaji damu uendelee. Angalau kila baada ya miezi sita tuandae kambi hii,”alisema Katibu tarafa huyo.
Alisema katika matibabu damu haina mbadala kwani haitengenezwi kwa namna yoyote ispo kuwa kwa wananchi kujitolea damu yao na kuokoa maisha ya wahitaji.
Zoezi la utoaji damu lilisimamia na maofisa wa Mpango wa Taifa wa Damu Salamaa, kutoka Hospitali ya Rufani ya Amana, ambao wamempongeza Mbunge Shingo na wananchi wote walio fika kujitolea damu kwa kuzingatia umuhimu wa uchangiaji huo


.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...