Vijana wa Kikundi cha Kigamboni Vijana Unity wamepata fursa mpya ya kujiajiri baada ya Benki ya NMB kukabidhi bajaji tano zenye thamani ya Sh60 milioni, huku ikisisitiza kuwa nidhamu ya marejesho ndiyo itakayofungua milango ya mikopo kwa maelfu ya vijana wengine nchini.

Akikabidhi bajaji hizo jijini Dodoma Ijumaa, Juni 12, 2026, Kaimu Meneja wa NMB Kanda ya Kati, Amos Mubusi, alisema mikopo hiyo imetolewa kupitia ushirikiano kati ya benki na Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa vikundi vilivyochaguliwa, kupatiwa mafunzo na kuthibitishwa kukidhi vigezo. Alisema NMB imekwishatoa zaidi ya Sh3 bilioni kwa vikundi 304 nchini, huku Sh228 milioni zikitolewa kwa vikundi 19 katika Jiji la Dodoma.

Mwenyekiti wa kikundi hicho, Antery Nestory, alisema wanachama wamejipanga kuhakikisha fursa hiyo haipotei baada ya kuwezeshwa bila kuweka dhamana ya mali. “Safari yetu ya kujenga maisha bora imeanza. Tutalindwa na nidhamu, utii wa masharti ya mkopo na usimamizi mzuri wa mapato,” alisema. Dodoma ni miongoni mwa halmashauri 10 zinazotekeleza awamu ya majaribio ya mikopo ya asilimia 10 kwa vikundi vya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu.

Dodoma ni miongoni mwa halmashauri 10 zinazotekeleza awamu ya majaribio ya mikopo ya asilimia 10 kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu.







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...