KUTOKA VUNJO.
KATIKA kuhakikisha kuwa wananchi wa Jimbo la Vunjo wanakabiliana na tatizo la uhaba wa ajira kwa kujiajiri wenyewe, Mbunge wa jimbo hilo Enock Koola amekuja kampeni maalum ya kuwafundisha wananchi ufugaji wa ng'ombe wa maziwa pamoja na samaki.
Mafunzo hayo yanayotarajiwa kutolewa kesho Juni 13 mwaka huu katika ukumbi wa shule ya viziwi kata ya njia panda.
Mafunzo hayo yatawasidia wananchi kujiajiri kupitia ufugaji wenye faida na kuwawezesha vijana kupata fursa ya ajira.
Hili ni mwendelezo wa juhudi za Mbunge Enock Koola ya kuhakikisha anainua uchumi wa wananchi wa jimbo hilo ambapo hapo awali alikuja na mkakati wa kufufua zao la kahawa kwa kuleta miche bora na ya kisasa kwa maeneo yanayolima zao hilo.
Katika kampeni ya miche bora ya miparachichi jumla ya vijana 60 walinufaika katika jimbo hilo, elimu ya ufugaji nyuki vijana 80 walinufaika, huku upande wa uvuvi na ufugaji ng'ombe vijana 80 watanufaika kutoka kila kata ili kwenda kutoa elimu kwa wananchi na vijana wengine.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...