Na Mwandishi Wetu


MAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, imewahukumu kifungo cha maisha jela Suleiman Thabit Ngulangwa na Farid Hamis Said baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la biashara haramu ya dawa za kulevya aina ya heroin yenye uzito wa kilo 15.19.

Katika hukumu iliyotolewa Juni 1, 2026, Jaji S.E. Kisanya alisema ushahidi wa upande wa mashtaka ulithibitisha pasipo shaka kuwa washtakiwa hao walikuwa na umiliki wa dawa hizo.

Mchambuzi wa Serikali kutoka Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA), Leonida Daniel Michael, aliithibitishia mahakama kuwa pakiti 16 zilizokamatwa zilikuwa na heroin yenye uzito wa kilo 15.19 baada ya kufanyiwa uchunguzi wa kisayansi.

Mahakama ilibaini kuwa utetezi wa washtakiwa haukuweza kuibua shaka dhidi ya ushahidi wa mashahidi na vielelezo vilivyowasilishwa.

Mshtakiwa wa pili, Sharifa Selemani Bakari, aliachiliwa huru baada ya mahakama kubaini kuwa upande wa mashtaka haukuthibitisha ushiriki wake katika kosa hilo.

Mbali na kifungo hicho, mahakama imeagiza heroin yote iliyokamatwa pamoja na vifaa vya kufungashia kuteketezwa kwa mujibu wa sheria.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...