Benki ya NMB imeendelea kuonyesha nafasi yake katika kukuza sekta ya kilimo kwa kutoa suluhisho za kifedha kwa wadau waliopo kwenye mnyororo wa thamani wa kilimo, wakiwemo wakulima, wanunuzi wa mazao, wachakataji, wasafirishaji na waagizaji wa pembejeo.
Akizungumza katika Banda la NMB kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam, Mkuu wa Idara ya Kilimo kwa Wateja Wakubwa wa Benki ya NMB, Christopher Mwalugenge, alisema benki hiyo inatoa mikopo inayowawezesha wateja kununua mazao kutoka kwa wakulima, kuyachakata na kuyapeleka sokoni.
Mwalugenge alisema huduma hizo ni muhimu hasa katika msimu wa mavuno ya mazao kama kahawa, tumbaku, ufuta na pamba, ambapo mahitaji ya mitaji kwa wanunuzi na wafanyabiashara wa mazao huwa makubwa. Alisema mikopo hiyo huandaliwa kulingana na aina ya biashara ya mteja na mzunguko wake wa mapato.
Alisema NMB itaendelea kuunga mkono juhudi za kuongeza thamani ya mazao ya ndani, kupanua masoko ya wakulima na kuchochea ukuaji wa uchumi kupitia sekta ya kilimo, ambayo inaendelea kuwa mhimili muhimu wa maisha na biashara kwa Watanzania wengi.
Akizungumza katika Banda la NMB kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam, Mkuu wa Idara ya Kilimo kwa Wateja Wakubwa wa Benki ya NMB, Christopher Mwalugenge, alisema benki hiyo inatoa mikopo inayowawezesha wateja kununua mazao kutoka kwa wakulima, kuyachakata na kuyapeleka sokoni.
Mwalugenge alisema huduma hizo ni muhimu hasa katika msimu wa mavuno ya mazao kama kahawa, tumbaku, ufuta na pamba, ambapo mahitaji ya mitaji kwa wanunuzi na wafanyabiashara wa mazao huwa makubwa. Alisema mikopo hiyo huandaliwa kulingana na aina ya biashara ya mteja na mzunguko wake wa mapato.
Alisema NMB itaendelea kuunga mkono juhudi za kuongeza thamani ya mazao ya ndani, kupanua masoko ya wakulima na kuchochea ukuaji wa uchumi kupitia sekta ya kilimo, ambayo inaendelea kuwa mhimili muhimu wa maisha na biashara kwa Watanzania wengi.




.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...