Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Julai 17, 2026 amekagua na kupokea taarifa ya maandalizi ya Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa yanayotarajiwa kufanyika Julai 25, 2026 katika Viwanja vya Mashujaa, Mtumba, jijini Dodoma.
Katika ukaguzi huo, Waziri Mkuu ameridhishwa na hatua zilizofikiwa na kuwataka wote wanaohusika kuendelea kukamilisha maandalizi yaliyobaki kwa wakati ili maadhimisho hayo yafanyike kwa utaratibu na hadhi inayostahili.
Maadhimisho hayo yataongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu.



.jpeg)



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...