Wananchi wa Kata ya Mpandangindo katika Jimbo la Peramiho wanatarajia kunufaika na ujenzi wa barabara ya Mpandangindo kupitia Parangu hadi Peramiho, baada ya Serikali kutenga zaidi ya shilingi milioni 250 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo.

Akizungumza na wananchi, Mbunge wa Jimbo la Peramiho, Mhe. Dkt. Lazaro Komba Bunungu, amewahakikishia kuwa ujenzi wa barabara hiyo utaanza, akieleza kuwa mradi huo ni sehemu ya jitihada za Serikali kuboresha miundombinu na kurahisisha shughuli za kijamii na kiuchumi.

Mhe. Dkt. Bunungu amesema barabara hiyo imekuwa kero kwa muda mrefu kutokana na hali yake kutokuwa nzuri, jambo ambalo limekuwa likikwamisha usafiri na usafirishaji wa mazao pamoja na shughuli nyingine za maendeleo kwa wananchi.

Kwa upande wake, Mhandisi wa TARURA, Simon Binamu, amesema tayari bajeti ya zaidi ya shilingi milioni 250 imetengwa kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo, na kwamba kwa sasa mradi upo katika hatua za utekelezaji.

Ujenzi wa barabara hiyo unatarajiwa kuboresha mawasiliano kati ya Mpandangindo, Parangu na Peramiho, kurahisisha usafiri wa wananchi, kuongeza fursa za biashara na kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika maeneo hayo.

Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...