Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Mhe. Mariam Abdallah Ibrahim, ameendelea na ziara yake katika Mkoa wa Morogoro, Wilaya ya Mvomero.


Akiwa Wilayani Mvomero, Mhe. Mariam amewashukuru wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na wananchi kwa kukiamini chama na kukipa ushindi mkubwa katika Uchaguzi Mkuu.

Katika ziara hiyo, amesisitiza umuhimu wa kuimarisha uhai wa jumuiya kwa kufanya vikao mbalimbali, kuhamasisha ushiriki wa wanawake katika shughuli za chama, pamoja na kuwahimiza wanawake kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya chama.

Aidha, Mhe. Mariam amekagua vikundi vilivyopatiwa mikopo kupitia Halmashauri na kuangalia maendeleo ya miradi yao. Pia amekagua ujenzi wa nyumba ya mtumishi wa UWT na kuchangia kiasi cha Shilingi Milioni Tano (5,000,000) kwa ajili ya kuunga mkono ujenzi huo.

“Tunaendelea kuimarisha jumuiya, kuwawezesha wanawake na kuhakikisha maendeleo yanafika kwa wananchi.”

Mhe. Mariam Abdallah Ibrahim
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya UWT Taifa






 

Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...