Serikali imesema udanganyifu katika mitihani ya kitaifa umepungua kwa kiasi kikubwa kutokana na kuimarishwa kwa usimamizi wa mitihani nchini.

Kauli hiyo imetolewa Septemba 7, 2026 mkoani Ruvuma na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu Prof. Carolyne Nombo, alipofika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma na kuazungumzia utekelezaji wa masuala mbalimbali ya elimu ikiwemo maandalizi ya mtihani wa Taifa wa darasa la saba unaotrajia kufanyika nchini kote Septemba 9 na 10, 2026.

Ameeleza kuwa mitihani ya kitaifa ni suala nyeti linalohitaji usimamizi madhubuti, hivyo viongozi wa elimu katika ngazi zote wanapaswa kuhakikisha taratibu zote za mitihani zinafuatwa.

“Udanganyifu umepungua kwa kiasi kikubwa, nawasihi wanafunzi wa darasa la saba manaotarajia kufanya mitihani yenu kutojiingiza katika udanganyifu wowote wa mitihani, tuzingatie taratibu zote za mitihani,” amesisitiza Prof. Nombo

Aidha, amezitaka kamati za mitihani za mikoa na viongozi wa elimu kuendelea kushirikiana katika kusimamia mitihani, huku akiwapongeza kwa hatua ambazo tayari zimechukuliwa katika kupunguza udanganyifu.

Amebainisha kuwa, Serikali itaendelea kuchukua hatua pale inapobaini vitendo vya udanganyifu, hasa vile vinavyohusisha kupanga kwa pamoja kati ya wanafunzi, walimu au wasimamizi wa mitihani.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Songea Mhe. Wilman Kapenjama amesema mkoa umejiandaa vema katika kusimamia mtihani huo kwa hali ya usalama bila changamoto yoyote.
Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...