Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amezitaka nchi wanachama wa Harakati za Nchi Zisizofungamana na Upande Wowote (NAM) kuunganisha sauti na misimamo yao ili kuongeza ushawishi katika maamuzi ya kimataifa na kutetea maslahi ya mataifa yanayoendelea.
Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo, tarehe 01 Septemba 2026, jijini Belgrade, Jamhuri ya Serbia, alipowasilisha hotuba kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika Mkutano Maalum wa Ngazi ya Juu wa Kumbukumbu ya Miaka 65 tangu kufanyika kwa Mkutano wa Kwanza wa Wakuu wa Nchi wa NAM.
Amesema misingi ya NAM iliyoasisiwa mwaka 1961 bado ina umuhimu katika dunia ya sasa, huku akisisitiza kuwa kutofungamana na upande wowote hakumaanishi kutokuwa na msimamo, bali ni uhuru wa mataifa kufanya maamuzi kwa kuzingatia maslahi yao na kulinda uhuru na mamlaka yao.
Rais Dkt. Mwinyi amesisitiza umuhimu wa kutatua migogoro kupitia mazungumzo, upatanishi na kujenga kuaminiana, pamoja na kushughulikia vyanzo vya migogoro vinavyotokana na ukosefu wa haki, usawa na ujumuishi.
Aidha, ametoa wito wa kufanyika kwa mageuzi katika mfumo wa Umoja wa Mataifa, ikiwemo Baraza la Usalama, pamoja na taasisi za fedha za kimataifa, ili kuongeza uwakilishi, uwazi na kuzingatia mahitaji ya nchi zinazoendelea. Amesema Afrika inastahili uwakilishi mkubwa na wa haki zaidi katika maamuzi ya kimataifa.
Vilevile, Rais Dkt. Mwinyi amesisitiza umuhimu wa kuimarisha Ushirikiano wa Kusini pamoja na ushirikiano kati ya NAM na BRICS, hususan katika fedha za maendeleo na mageuzi ya mfumo wa utawala wa kimataifa, bila kuathiri misingi na utambulisho wa NAM.
Amesema Tanzania itaendelea kuunga mkono NAM yenye umoja na yenye uwezo wa kukabiliana na changamoto za dunia ya sasa, kwa kuhimiza amani, haki ya maendeleo, ushirikiano wa Kusini na mfumo wa dunia wenye usawa na uwakilishi wa haki.
Mkutano huo wenye kaulimbiu “Urithi wa Kutofungamana na Upande Wowote: Mafunzo kwa Dunia ya Leo” umefunguliwa na Rais wa Jamhuri ya Serbia, Mhe. Aleksandar Vučić, na kuhudhuriwa na Viongozi Wakuu wa Serikali pamoja na Wakuu wa Ujumbe kutoka mataifa 34.
Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo, tarehe 01 Septemba 2026, jijini Belgrade, Jamhuri ya Serbia, alipowasilisha hotuba kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika Mkutano Maalum wa Ngazi ya Juu wa Kumbukumbu ya Miaka 65 tangu kufanyika kwa Mkutano wa Kwanza wa Wakuu wa Nchi wa NAM.
Amesema misingi ya NAM iliyoasisiwa mwaka 1961 bado ina umuhimu katika dunia ya sasa, huku akisisitiza kuwa kutofungamana na upande wowote hakumaanishi kutokuwa na msimamo, bali ni uhuru wa mataifa kufanya maamuzi kwa kuzingatia maslahi yao na kulinda uhuru na mamlaka yao.
Rais Dkt. Mwinyi amesisitiza umuhimu wa kutatua migogoro kupitia mazungumzo, upatanishi na kujenga kuaminiana, pamoja na kushughulikia vyanzo vya migogoro vinavyotokana na ukosefu wa haki, usawa na ujumuishi.
Aidha, ametoa wito wa kufanyika kwa mageuzi katika mfumo wa Umoja wa Mataifa, ikiwemo Baraza la Usalama, pamoja na taasisi za fedha za kimataifa, ili kuongeza uwakilishi, uwazi na kuzingatia mahitaji ya nchi zinazoendelea. Amesema Afrika inastahili uwakilishi mkubwa na wa haki zaidi katika maamuzi ya kimataifa.
Vilevile, Rais Dkt. Mwinyi amesisitiza umuhimu wa kuimarisha Ushirikiano wa Kusini pamoja na ushirikiano kati ya NAM na BRICS, hususan katika fedha za maendeleo na mageuzi ya mfumo wa utawala wa kimataifa, bila kuathiri misingi na utambulisho wa NAM.
Amesema Tanzania itaendelea kuunga mkono NAM yenye umoja na yenye uwezo wa kukabiliana na changamoto za dunia ya sasa, kwa kuhimiza amani, haki ya maendeleo, ushirikiano wa Kusini na mfumo wa dunia wenye usawa na uwakilishi wa haki.
Mkutano huo wenye kaulimbiu “Urithi wa Kutofungamana na Upande Wowote: Mafunzo kwa Dunia ya Leo” umefunguliwa na Rais wa Jamhuri ya Serbia, Mhe. Aleksandar Vučić, na kuhudhuriwa na Viongozi Wakuu wa Serikali pamoja na Wakuu wa Ujumbe kutoka mataifa 34.




.jpeg)
.jpeg)





.jpeg)


.jpeg)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...