wanenguaji wa twanga wakila sebene usiku wa mwaka mpya hoteli ya landmark. watu wengi walilalamika na wengine kuondoka pale menejimenti ya hoteli na bendi walipopandisha bei ghafla tok 5,000/- hadi 7,000/- ambapo wengi walijiendea fm academia ambako wao ilikuwa ile ile 5,000/- na walizidi kudhihirisha kuwa ni tishio kwa bendi za bongo kwa kuwa katika chati...
nilipomuuliza dada asha baraka kisa cha kufanya tamaa, akaruka kimanga na kudai kwamba huo haukuwa uamuzi wa twanga pepeta, ila wa menejomenti ya hoteli. aliungama kwamba kitendo kama hicho ni hatari kwa biashara hasa ikizingatiwa kuna mpinzani wa kweli pembeni akingoja makosa kama hayo anufaike - kama alivyonufaika usiku wa kuamkia leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. Baaab kubwa naona ombi letu wamelisikia, sasa matambala meusi hukuna tena!

    ReplyDelete
  2. Haya twanga kazi wanayo......tama jamani.....michuzi ebu tuwekee na chipolopolo au ndo wameisha???? FM naona wanakula vichwa tu

    ReplyDelete
  3. Twanga wameishiwa, hata kiongozi wao kachoka ndio maana watu sasa wanakimbilia kwenye muziki wa uhakika Wazee wa ngwasuma!!Kama una akili timamu 5,000 yako peleka FM Academia inalipa kuliko kuipotezea Twanga palipojaa wachovu na wagonjwa kibaooooo!!!!

    ReplyDelete
  4. kama kutwanga na kupepeta kwenyewe ni hivi ninavyoona kwenye picha.Wadau naomba ruhusa niondoke Twanga pepeta nirudi kijijini kulima.

    ReplyDelete
  5. HAWANA MPANGO HAWA TWANGA PEPETA.
    NDIO WAMEZIDI KUJIHARIBIA KWA TAMAA YA PESA NA KUWAGILIBU WATU, MIE NI MMOJA WA WATU WALIOFIKA MLANGONI GAFULA KIINGILIO KIMEPANDA TOKA ELFU 5, MPAKA ELFU 7, AKA MWENZANGU MIE NA KUNDI LA WASHKAJI WANGU 9 TUKAONDOKA TUKAENDA -FM ACADEMIA WANA NGWASUMA. NA TULIINJOY SANA, TENA SANA,
    ACHANENI NAO HAWA. MNATAKA KUWA-WIN WANANCHI TENA ILI MPATE WATEJA WENGI, MSIFANYE MAMBO YA UTAPELI KAMA HIVI. KWA MIE NA WENZANGU MMESHAPOTEZA CUSTOMERS KWANI KAMWE HATUTAKUJA KWENYE SHOW ZENU TENA, KAMWE.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...