*Aahidi kujenga viwanda vya kuongeza thamani ili kuongeza ajira kwa vijana


Na Said Mwishehe,Michuzi TV-Ruvuma


MGOMBEA Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)Dk. Samia Suluhu Hassan amesema katika Mkoa wa Ruvuma katika miaka mitano iliyopita Serikalini imetekeleza kwa kiasi kikubwa miradi ya maendeleo ya kijamii katika sekta za maji, elimu, afya na umeme serikali imetekeleza miradi hiyo kwa kasi kubwa.

Akizungumza na wananchi wq Songea Mjini katika Uwanja wa VETA mkoani Ruvuma Dk.Samia ameeleza hatua kwa hatua maendeleo ambayo yamepatikana ndani ya Mkoa huo kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita .

Kuhusu maji amesema kuna miradi mingi ambayo inaendelea kutekelezwa ndani ya mkoa huo na itakapokamilika itapita kiwango cha upatikanaji maji kilichoelekezwa na ilani ya uchaguzi (2020 - 2025).

"Kwa hiyo bado miradi inaendelea, maji yatapatikana niwaombe tuwe wastahimilivu ili wakandarasi wafanyekazi zao vizuri na maji yapatikane," alibainisha.

Kwa upande wa elimu Dk.Samia amesema kwamba ujenzi wa madarasa, shule mpya umefanyika huku serikali ikiendelea kutoa elimu bila malipo.

Pia, amegusia ujenzi wa Chuo Kikuu cha Uhasibu Arusha tawi la Songea ambapo ameeleza kwamba chuo hicho kitakamilika kitachukua wanafunzi 10,000 kwa mkupuo.

“Ni fursa nzuri kwa wananchi wa Mkoa wa Ruvuma kuhamasika kusoma fani mbalimbali zitakazotolewa chuoni hapo.Najua tutakuwa na Wahasibu wengi kutoka Ruvuma kutokana na uwepo wa Chuo hiki.”

Dk.Samia pia amesema serikali itatekeleza ujenzi wa chuo cha wenyeulemavu eneo la Liganga jimbo la Peramiho kitakachoweza kutoa mafunzo yaliyokusudiwa.

Kuhusu mkakati wa nishati safi, ameeleza kwamba Serikali imetekeleza mkakati huo zaidi ya ilivyotarajiwa katika ilani.

"Ilani ilituambia tukifika 2025 vijiji vyote viwe na umeme lakini serikali ipo katika vitongoji kuunganisha umeme. Takriban vitongoji nusu vya Tanzania tayari vimeshaunganishwa umeme.

"Lakini tunafanya hivyo kwa sababu tuliahidi kila wilaya kuwa na kongani za viwanda na tunataka tutakapoanza kuweka kongani za viwanda, umeme uwe umeshafika na ndiyo maana tunakwenda kwa kasi."

Ametoa mfano Mabada serikali itaweka viwanda vya kuongeza thamani zao la misitu ili kuongeza ajira na kukuza uchumi kwa vijana na Taifa.

Dk. Samia amesema uwepo wa umeme kutavutia wawekezaji wengi zaidi kuwekeza katika maeneo hayo.

Ameongeza kuwa serikali inakusudia kuweka viwanda vya kuongeza thamani zao la kahawa na parachichi.

"Kule Peramiho tumepata mwekezaji mkubwa wa kiwanda cha sukari na shamba kubwa la miwa. Hii pia ni fursa nyingine kutengeneza ajira kwa vijana wetu.

"Mkitupa ridhaa tutaendelea kuwekeza kwa kuongeza tija upatikanaji ruzuku ya mbolea na pembejeo za kilimo. Kama mnavyoona matokeo ya ruzuku na pembejeo za kilimo yameongekana.

Amesema Halmashauri ya Songea imeongeza uzalishaji mazao ya chakula kutoka tani 200,000 hadi tani 455,500.Pia uzalishaji mazao ya kilimo kwa Madaba umepanda kutoka tani 41.7 hadi tani 160,000.

Kwa upande wa Mbinga, uzalishaji kahawa umepanda ambapo pia ruzuku ya miche na pembejeo za kilimo zinatolewa na serikali.

“Uzalishaji kahawa umependa kutoka tani zaidi ya 100 hadi kufikia tani 300,”amesema na kubainisha aliwahi kutembelea shamba la mwekezaji ambalo limeajiri watu 3000 hali inayoonyesha mkoa huo kuwa kinara kwa kilimo.

"Tutajielekeza kujenga viwanda vya kuongeza thamani ili tuongeze ajira nyingi kwa vijana. Niwasisitize ndugu zangu wa Ruvuma mbolea hizi na pembejeo zinazotolewa kwa ruzuku naomba mtumie nyinyi na zisiuzwe.

"Kwa sababu ukiuza unawapa faida wengine wa jirani, mnawapa faida zaidi walime kwao kwa mbolea ya ruzuku, wewe hata ukipata pesa faida zaidi kwa mwenzako," amesema.

Amewashukuru wananchi wa mkoa huo kwa kuchangia vyema usalama wa chakula ndani ya nchi na mataifa jirani ambako mahindi yanapelekwa kuuzwa.

Aidha amesema Januari mwaka huu Tanzania ilikuwa mwenyeji wa mkutano wa nchi 25 za Afrika zinazozalisha kahawa.

Dk. Samia amesema katika mkutano huo liliwekwa lengo la ndani ya miaka 10 ijayo (2025 - 2035) asilimia 50 ya kahawa bora inayozalishwa Afrika iwe inasindikwa kabla ya kuuzwa nje ya Afrika.

“Hilo ndilo lengo la serikali kutekeleza azimio hilo ambapo CCM imeweka ahadi kuweka mitambo ya kukoboa kahawa kabla haijauzwa.

Pia amesema serikali imetekeleza mradi wa ujenzi maghala 28 ya kuhifadhia mazao mkoani Ruvuma ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Songea ina maghala 11, Mabada (tisa) Namtumbo (saba) na ghala moja kwa Manispaa ya Songea.

Mgombea Dk.Samia amesema katika Manispaa ya Songea serikali itakamilisha ujenzi wa soko la kisasa Manzese A na B."Soko hilo ambalo mmelisubiri kwa muda mrefu sasa linajengwa na hatujawasahau wanangu wamachinga mtakuwa na sehemu katika soko hilo.

"Niseme pia kwamba mkoa huu umebarikiwa kuwa na madini mengi kuanzia dhahabu, shaba, makaa ya mawe, madini ujenzi na vito hadi urani yanapatikana ndani ya mkoa huu," alisisitiza.

Dk. Samia alieleza kuwa endapo CCM ikipatiwa ridhaa, serikali yake itaanzisha na kuendeleza kongani za viwanda zinazohusiana na madini.

Alisema hatua hiyo itasaidia kuongeza thamani ya madini kabla ya kuuzwa huku kipaumbele kikiwa katika uchimbaji na wachimbaji wadogo."Tutakwenda kuboresha wachimbaji wadogo lakini pia tutawaelekeza uchimbaji ambao utatunusuru kwenye vifo.”

Alibainisha kuwa mwaka huu alifika wilayani Namtumbo kuzindua mradi wa madini ya urani pamoja na kuchimba madini hayo azma ya serikali yachakatwe, yasafirishwe kisha uwepo mtambo wa kuzalisha umeme nchini ili umeme wa uhakika upatikane.“Duniani madini hayo yanakubalika kama nishati safi kwa taifa kuyatumia.”












 Katibu Mtendaji wa THBUB, Patience Ntwina akizungumza wakati wa mafunzo maalum kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Septemba 22, 2025.

Picha ya Pamoja.

TUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imewataka waandishi wa habari nchini kuepuka vitendo vya rushwa, takrima na zawadi zinazoweza kuathiri weledi na uadilifu wao wakati wa kuripoti habari za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.

Rai hiyo imetolewa na Katibu Mtendaji wa THBUB, Patience Ntwina, wakati wa mafunzo maalum kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Septemba 22, 2025 alisisitiza kuwa wanahabari ni mhimili muhimu katika kulinda demokrasia na amani ya taifa kupitia kazi zao.

“Ninyi ni muhimili wa nne unaoheshimika nchini. Msiruhusu kalamu zenu zigeuke chombo cha kupandikiza chuki au kupotosha ukweli kwa ajili ya maslahi binafsi. Epukeni rushwa na zawadi zinazoweza kuwafanya muegeme upande wa chama au mgombea fulani,” alieleza

Aidha, mafunzo hayo yamelenga kuongeza uelewa wa kitaaluma na kimaadili kwa waandishi wa habari kuhusu haki na wajibu wao katika kipindi cha uchaguzi.

Waandishi walihimizwa kutumia mbinu za uhakiki wa taarifa (fact-checking) kabla ya kuchapisha au kutangaza habari ili kuepusha upotoshaji, lugha za uchochezi na taarifa zisizo na uthibitisho.

Ntwina, ameeleza kuwa jukumu la vyombo vya habari ni kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi kuhusu sera na ajenda za kisiasa, bila upendeleo, huku vikibaki kuwa daraja kati ya wagombea, vyama vya siasa, Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na wananchi.

Mafunzo yanasaidia kuimarisha uhusiano kati ya vyombo vya habari na mamlaka za dola, kukuza uhuru wa habari na kuimarisha misingi ya demokrasia nchini.
Na Said Mwishehe,Michuzi TV-Michuzi TV

MGOMBEA Mwenza wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, ameeleza kwamba hakuna eneo lolote nchini ambalo halijaguswa na maendeleo katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan.

Dk. Nchimbi ameeleza hayo alipohutubia maelfu ya wananchi katika mkutano wa kampeni za Mgombea Urais kupitia CCM Dk. Samia uliofanyika uwanja wa VETA mjini Songea jana.

“Kila Mtanzania ni shahidi kwa kasi ya maendeleo iliyofanyika nchini ikiwemo Mkoa wa Ruvuma. Umefanyakazi kubwa ya kuleta maendeleo katika maeneo yote nchi nzima. Hakuna sehemu haijaguswa na mkono wako wa maendeleo.

"Ndiyo maana leo sisi wasaidizi wako tunazunguka nchi nzima kifua mbele kunadi sera za CCM kwa sababu yapo mambo yametekelezwa chini ya uongozi wako," amesema.

Akieleza zaidi alipokuwa anawasilisha salamu za wananchi wa kabila la wasukuma ambao ni watani wa wangoni amesema wamedhamiria kuongoza kitaifa kwa kumpa Dk. Samia kura nyingi za ndiyo zikiambatana na wabunge na madiwani.

"Nimepita kwa watani wetu wasukuma wamesema wao kwa kazi alizozifanya Rais Dk. Samia wataongoza kitaifa kwa kura nyingi kwa Samia, wabunge na madiwani.

"Sasa ndugu zangu wa Ruvuma tusikubali kutaniwa na Wasukuma, tushindane na tuwashinde kwa kura nyingi. Wasukuma wamedhamiria kutushinda," amesema.

Aidha, Balozi Dk. Nchimbi alitoa msisitizo kwa Watanzania kutunza vitambulisho vyao vya kupigia kura na ifikapo Oktoba 29 mwaka huu wajitokeze kwa wingi kwenda kumpigakura Dk. Samia.








-Kutua mkoani Tanga Septemba 28 kwa ajili ya Kampeni kwa muda wa siku tatu.

-Wananchi watakiwa kujitokeza kwa wingi kumlaki.


Na Oscar Assenga, TANGA

MGOMBEA Urais wa Tanzania kupitia (CCM) Dkt Samia Suluhu anatarajiwa kuwasili Mkoani Tanga Septemba 28 mwaka huu na atapokelewa eneo la Mkata wilayani Handeni mkoani Tanga jioni na atakuwa na ziara ya kampeni ya siku tatu .

Akizungumza leo na waandishi wa habari Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga, Alhaj Rajab Abdurhaman kuhusu ujio wa Mgombea huyo ambapo alisema baada ya kupokelewa atawasalimia wananchi wa eneo hilo na baadae atakwenda Tanga mjini kwa ajili ya mapumziko na siku inayofuatia ataanzia wilaya ya Pangani kuzungumza na wananchi kupitia mkutano wa hadhara na Tanga mjini



Akizungumzia ujio wake Mwenyekiti huyo alisema ni vizuri wananchi katika maeneo mbalimbali atakayopita mgombea huyo kujitokeza kwa wingi kumlaki kwamba anayokuja kuwahutubia ni kupitia ilani ya uchaguzi 2025/2030 baada ya kuunda Serikali maendeleo yatakayokuja kwa ajili ya wananchi wote hiyo aliwaomba wana CCM wote popote walipoo kila mmoja wanawakaribisha kujitokeza kumlaki mgombea huyo.

“Niwaombe wananchi na wana CCM wote kila mmoja tunawakaribisha kumlaki na kumpokea Mgombea wa Urais kupitia CCM hatuna mgombea mwengine zaidi ya Dkt Samia tujitokeza kwa wingi na baada ya kumalizia Mkutano Tanga mjini atapita Muheza, Korogwe na ratiba katika maeneo hayo zitatolewa kwa nyakati tofauti”Alisema Mwenyekiti huyo.

Aidha alisema kwamba wana Tanga wanajiona watu wenye bahati kupata ugeni huo mkubwa kwa mara ya pili kwa mwaka huu mmoja amekuja kwa ziara ya kikazi miezi michache iliyopita mwaka huu na alikpokuja Tanga mambo mengi ya kimaendeleo ya Tanga yamefunguka na mambo yalikwenda vizuri na sasa anakuja kama Mgombea Urais.

Rajabu ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu (MCC) alisema kwamba wananchi kwenye mkoa wa Tanga wanategemea maendeleo zaidi kwa sababu kuna utofauti kati ya Mgombea wa CCM na wengine kutokana na kwamba wao walihaidi na wameshafanya kupitia ilani ya uchaguzi na aliyekuwa mtekelezaji ni Rais Dkt Samia Suluhu.

Alisema kwamba kutokana na mambo makubwa ya kimaendeleo yaliyokwisha kufanyika imani yao ni kwamba wananchi watakiunga mkono chama chao kwa sababu wana imani kwamba wakihaidi wanatekeleza kwa vitendo.

Hata hivyo alisema kwamba ni wana matumaini makubwa watu watampa kura nyingi Rais Dkt Samia Suluhu kwa sababu namna alivyojipambanua katika suala la kulinda amani ya nchi kwa kutumia busara na hekima na miradi mikubwa ya maendeleo.

Alisema kwamba Dkt Samia alipokuja katika ziara ya kikazi kabla ya kuja kuna miradi ilikuwa inasuasua lakini baada ya kuja ipi miradi imefunguka mfano barabara ya Tanga-Sadani -Bagamoto kasi ilivyoongezeka na Barabara ya Soni –Bumbuli mpaka Dindira na Korogwe kupitia kwa Meta wameona barabara hiyo wataalamu wanakwenda kuanza muda msio mrefu.

Aliongeza kwamba hiyo yote ni baada ya ujio wake hivyo wanaamini anapokuja anakwenda kuwaidi yale yaliyopo kwenye ilani mpya ya uchaguzi na miradi iliyobaki itakwenda kutiliwa mkazo itamalizika na miradi mipya iweze kuanzishwa .
MGOMBEA Udiwani Kata ya Kigamboni kwa tiketi ya CCM, Dotto Msawa, amewaomba wananchi wamchague ili kukamilisha kazi aliyoanza ya kuwaletea maendeleo.

Pia amemshukuru mgombea Urais Dk. Samia Suluhu Hassam, kuwapa fedha nyingi za utekelezaji wa miradi mbalimbali ya mendeleo katika kata hiyo.

Dotto alisema hayo, juzi katika mkutano wa uzinduzi wa kampeni katika kata hiyo, viwanja vya Shababu, Dar es Salaam,

Alisema kazi kubwa ameanza awamu iliyopita na sasa wamchague akakamilishe katika huduma za afya, barabara, elimu na ujenzi wa Soko la kisasa Magengeni kwa Urasa.

"Wananchi naomba kura zenu za ndiyo, nikamalize kazi niliyoanza awamu iliyopita, mliniamini na nikafanya makubwa katika utekelezaji wa Ilani ya CCM iliyopita, sasa naimba nikamalizie yale niliyoanza", alisema.

Dotto alisema atahakikisha barabara zote zenye mahitaji ya kiwango cha lami zitakamilika muda siyo mlefu kuanzia sasa na zitawekwa taa za barabarani zaidi ya 5,000, pia itawekwa mifereji ya kutoa maji katika makazi ya waanchi.

Alisema kata hiyo imefanikiwa kupata Shule ya Sekondari Paul Makonda, ambapo inaendelea kuboreshwa kwa upande wa ujenzi wa maabara, kuongeza vyumba vya madarasa pamoja ujenzi wa nyumba za walimu, pia amepeleka maombi serikalini kwaajili ya ujenzi shule ya sekondari kidato cha tano na sita.

Alisema shule nyingi za msingi Kigamboni zina majengo ya chini, hivyo ataanza kuijenga Shule ya Msingi Raha Leo iwe ya ghorofa, fedha za kuanzia zipo.

Pia Dotto alisema kwa upande wa afya, wakati anaingia madarakani alikuta kata ina zahanati, kwa juhudi zake na serikali inayoongozwa na mgombea urais Dk. Samia amefanikiwa kujenga Kituo cha Afya Kigamboni chenye hadhi ya nyota tatu, ambapo huduma zote za afya muhimu zinapatikana.

"Wananchi wenzangu wa Kigamboni mama Samia anatupenda sana, ameleta maendeleo kwa haraka sana alipoingia madarakani na ametoa fedha nyingi za miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo afya, elimu na miundombinu ya barabara, kwahiyo tumlipe kwa kumpa kura nyingi za ndiyo, pia tunamshuuru sana", alisema.

Dotto alisema Kigamboni hakuna soko la kisasa, atakapomchagua tena atakwenda kujenga soko kubwa la kisasa katika eneo la magengeni kwa Urasa.






Jengo refu linawaka moto katika Mtaa wa Nyamwezi na Narung’ombe, karibu na geti la kuingilia Shimoni Kariakoo.

Jitihada za kuuzima unaendelea huku chanzo cha moto huo bado hakijafahamika, kaa karibu na Michuzi Media kukujuza zaidi


Na Augusta Njoji, Handeni TC

MKUU wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, amewataka Maofisa Mifugo wa Halmashauri ya Mji Handeni kutumia vishikwambi walivyokabidhiwa na serikali kwa kazi za kiofisi pekee na si kwa matumizi binafsi.

Akizungumza Septemba 22, 2025 wakati wa ugawaji wa vifaa hivyo mjini Handeni, Nyamwese amesema vishikwambi hivyo vimetolewa ili kuongeza ufanisi katika utendaji kazi na kusaidia harakati za utambuzi wa mifugo.

“Tusije tukasikia vinaingia kwenye matumizi ya mitandao ya kijamii kama ku stream live, kuingia youtube, instagram, facebook. Vishikwambi hivi vitumike kutekeleza majukumu yaliyokusudiwa,” amesema.

Ameongeza kuwa vifaa hivyo vitunzwe na changamoto zozote ziwasilishwe Kitengo cha TEHAMA cha Halmashauri badala ya kupelekwa kwa mafundi wa mtaani.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Gerald Kauki, amesema hatua hiyo itawaongezea maofisa ufanisi katika kutoa huduma kwa wafugaji.

Naye, Mkuu wa Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi wa Halmashauri hiyo, Aldegunda Matunda, amesema Halmashauri ina maofisa mifugo 27 wanaohudumia wafugaji 34,484 wenye mifugo zaidi ya 148,000.

Amefafanua kuwa katika mpango wa chanjo ya mifugo, Halmashauri imepokea vishikwambi 25 kutoka serikalini ambapo awali walikuwa na vishikwambi viwili pekee katika utambuzi wa mifugo.

“Utambuzi wa ng’ombe umefikia asilimia 58 na mbuzi asilimia 17. Tunaamini vifaa hivi vitachochea kasi ya utekelezaji wa mpango huo,” amesema.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele leo Septemba 21, 2025 ametembelea Halmashauri ya Mji wa Mafinga Wilayani Mufindi Mkoani Iringa ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kukagua maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 ambapo pamoja na mambo mengine alipokea taarifa ya Mji huo kutoka kwa wasimamizi wa Uchaguzi wa Halmashauri kuhusu maandalizi ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani wa Mwaka 2025 na kisha kukagua vifaa ambavyo tayari vimepokelewa katika Halmashauri hiyo.


Jaji Mwambegele yupo Mkoani Iringa kukagua maandalizi hayo na kutazama kampeni za wagombea katika majimbo ya Mkoa wa Iringa



kwa mujibu wa ratiba iliyotangazwa na Tume,Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 unatarajiwa kufanyika Oktoba 29, mwaka huu.

"Kura Yako Haki Yako Jitokeze Kupiga Kura"
Mratibu wa Uchaguzi Mkoa wa Iringa Bi. Nuru Sovella akizungumza jambo wakati wa utoaji wa taarifa maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 kwa Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele
Msimamizi Jimbo la Mafinga Mjini Mwalimu Doroth Kobelo akiwasilisha taarifa ya maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 kwa Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele (katikati) kulia ni Mratibu wa Uchaguzi Mkoa wa Iringa, Bi. Nuru Sovella.


Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza na wasimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Mafinga Mjini ambapo aliwasisitiza kutekeleza majukumu yao kwa weledi na ufanisi.


Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza na wasimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Mafinga Mjini ambapo aliwasisitiza kutekeleza majukumu yao kwa weledi na ufanisi.

Mratibu wa Uchaguzi Mkoa wa Iringa, Bi. Nuru Sovella akisikiliza kwa umakini


Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akiangalia sehemu ya vifaa vya uchagzi ambavyo vimeshapokelewa.

 
Na Mwandishi wetu, Michuzi Tv

MAMLAKA za Mapato za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) zimekutana jijini Dar es Salaam kujadili namna ya kuboresha mifumo ya kodi ili kuchochea ukuaji wa biashara ndani ya Jumuiya hiyo.

Akizungumza katika hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa mia moja wa Kamati ya Kiufundi ya Mamlaka hizo leo Septemba 22, 2025 jijini Dar es Salaam, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Yusuph Mwenda, alisema nchi wanachama zinapaswa kuwa na suluhu za pamoja kuondoa vikwazo vinavyokwamisha urahisi wa kufanya biashara.

“Tunapaswa kuona namna tunavyoimarisha biashara katika ukanda wa EAC. Ni muhimu watanzania waweze kwenda Uganda, Kenya, Rwanda, Burundi na kwingine kufanya shughuli zao bila changamoto yeyote inayotokana na vikwazo vya kikodi. Sisi Tanzania tutaviondoa, na tunatarajia na wao pia wafanye hivyo ili kuhamasisha biashara za kikanda,” amesema Mwenda.

Amebainisha kuwa tatizo la magendo bado ni changamoto kubwa nalinachochewa na tofauti za viwango vya kodi baina ya nchi wanachama.

Amesema Kamati hiyo itajadili mbinu za kudhibiti hali hiyo, ikiwemo kuchukua hatua kali za kisheria dhidi ya wahusika na kutumia teknolojia za kisasa kama akili mnemba (AI) kuwabaini na kuzuia vitendo hivyo.

Mwenda ameongeza kuwa majadiliano hayo pia yatajikita katika kukuza biashara za ndani na kupunguza kodi za ndani ili wafanyabiashara wa ukanda huo waweze kushindana ipasavyo katika masoko ya nje.

“Tunataka kujenga taswira nzuri ya taasisi zetu kwa kuondoa rushwa na kuweka utawala unaomsaidia mlipakodi badala ya kumwonea. Ni lazima tufanye mageuzi yanayoendeshwa na teknolojia, kutumia uchambuzi wa takwimu, kuoanisha mifumo yetu na viwango vya kimataifa, na kuimarisha uwazi,” alisema.

Amesisitiza kuwa sera ya kodi itajadiliwa ili kuona namna ya kufanana kwa viwango vya ndani (tax rates), ili wafanyabiashara wanaofanya biashara katika nchi tofauti za EAC wasikumbane na changamoto kutozwa kodi kubwa au utofauti wa kodi.

“Kwa mfano, wapo wanaozalisha bidhaa kama vigae wanapopeleka katika nchi jirani wanatozwa kodi kubwa. Tunapaswa kuondoa vikwazo hivyo na kurahisisha mifumo ya kodi iwe rahisi, inayoeleweka na ya kutabirika,” alifafanua

Aidha, amesema wigo wa kodi bado ni finyu, hivyo kuna haja ya kurasimisha sekta isiyo rasmi, ikiwemo biashara ndogo ndogo na sekta ya dawa, ili kupanua msingi wa mapato.

Mwenyekiti wa mkutano huo, Beatus Nchota amesema wamejipanga kutoa matokeo yenye viwango vya juu vitakavyosaidia ukuaji na ustahimilivu wa uchumi wa kikanda.

“Kadri ukanda wa Afrika Mashariki unavyokua, ni lazima mifumo yetu ya kodi ibadilike kuendana na mabadiliko ya uchumi wa bidhaa. Tunapaswa kubaki na suluhisho la pamoja, mawazo bunifu, mikakati na mbinu mpya zitakazotusogeza mbele kwa malengo ya pamoja,” amesema Nchota.

Ameeleza kuwa Kamati hiyo imelenga mikakati ya kuoanisha ubunifu na teknolojia katika ukanda huo ili kusaidia viwanda vidogo pamoja na usimamizi wa mizigo mikubwa mipakani, ikiwemo madini, gesi na shughuli za usafirishaji.

Vilevile, amesema watajadili mpango wa biashara ya kukodisha (GOS) kwa kujifunza kutoka migogoro ya zamani ya kodi na mitandao mingine ya kikanda kama 'African Tax Administration Forum '(ATAF)

“Tutathmini matumizi ya biashara yenye ufanisi katika kuboresha huduma za usimamizi wa mapato, tutatafuta mbinu za kurahisisha kodi kwenye sekta isiyo rasmi, na kufanya utafiti wa kulinganisha mifumo ya 'Relevant Contracts Tax' ( RCT) katika nchi wanachama ili kubaini njia bora za pamoja,” amesema.

Ameongeza kuwa watajadili pia mikakati ya mafunzo na maendeleo ya taaluma kwa lengo la kuongeza uwezo na kubakiza vipaji ndani ya mamlaka za kikanda.

Naye Mwakilishi kutoka Rwanda, Densi Mukama amesema wamejifunza kutoka Tanzania kuhusu matumizi ya risiti wakati wa manunuzi, akibainisha kuwa utaratibu huo unarahisisha utunzaji wa kumbukumbu.

“Njia hii tutaianza kwetu. Mteja anapokuwa na risiti anapata uthibitisho wa manunuzi, jambo ambalo sisi hatukuwa na utamaduni nalo,” amesema.









Top News