MAKAMU WA Rais Dkt Emmanuel Nchimbi amewataka waandishi waendesha ofisi kuongeza jitihada katika kutekeleza majukumu yao bila woga na kwamba Serikali inatambua mchango wao mkubwa kwa kazi wanayoifanya na ndio sababu Rais Dkt Samia amekubali kuwa mlezi wa chama hicho.
Aidha amewataka kutoa ushauri mzuri Kwa viongozi wao Kwa kutumia uzoefu waliokuwa nao pale yanapotokea mazingira ya kutoa ushauri katika taasisi hizo kwa kuwa itawajengea heshima na kufanya kuaminika.
Dkt Nchimbi akizungumza Leo Mei21, 2026 kwenye mkutano mkuu wa chama hicho unaendelea katika kituo cha Mikutano cha Tanzania Convention Center Ngurdoto Arusha, amesema waendesha ofisi ni watu muhimu na hawapaswi kubezwa Kwa namna yoyote Ile.
" Taasisi yenu inaaminika na ndio sababu Rais amekubali kuwa mlezi wenu, niwaombe tu kuendelea kuwa waaminifu na mfanye kazi Kwa uadilifu wakati wote wa utekelezajibwa majukumu yenu," amesema.
Akisoma risala ya chama hicho Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi waendesha ofisi Tanzania (TAPSEA),Bi.Zuhura Songambele Maganga amekemea tabia ya udhalilishaji inayoendelea kufanywa kupitia mitandao ya kijamii kuhusu kada ya Waandishi waendesha ofisi.
" Sisi kama waandishi waendesha ofisi maarufu kama Makatibu Muhtasi tunasikitishwa na tabia ya baadhi ya udhalilishaji inayoendelea huko mitandaoni, hii ni kada inayojiheshimu na watendaji wamekuwa na maadili na wanafuata miongozo ya Serikali," amesema.
Amesema kada hiyo ya waandishi waendesha ofisi isidhalilishwe kama inavyofanyika kwenye mitandao ya kijamii na majukwaani na kwamba ni taasisi inayoheshimika na miongoni mwao wako wake wa viongozi serikalini hivyo hawawezi kufanya mambo machafu ofisini kwao.
Amesema tangu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kukubali kuwa maezi wa chama hicho, wamekuwa na ujasiri wa kutekeleza majukumu yao na kujiamini.
Aidha Bi.Zuhura amemuomba Rais Samia kuwaongezea mshahara endapo uchumi utaruhusu kutokana na majukumu mengi ambayo wamekuwa wakiyatekeleza kama waandishi waendesha ofisi.
Waziri wa nchi ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa umma, Ridhiwani kikwete, amesema katika mwaka 2026/2027, Serikali imepanga kuongeza ajira mpya 45,000 ikiwemo kada ya Waandishi waendesha ofisi Ili kuboresha na kurahisisha utumishi wa umma nchini.


.jpeg)


.jpeg)



.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)



.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)










.jpeg)

.jpeg)






.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)



.jpeg)
