Na Mwandishi wetu ,Dar es salaam 

KUTOKANA na uvunjifu wa amani na uharibifu wa miundombinu uliojitokeza kwa siku  nne hadi tano  zilizopita kwa baadhi ya maeneo hapa nchini ,wadau mbalimbali wamejitokeza na kulaani vikali vitendo hivyo.

Wamedai kwamba hali hiyo  haipaswi kujitokeza tena katika nchi  yetu nakwamba haikuzoeleka kwa wananchi na  kwenye macho ya watanzania  kwa miaka  mingi iliyopita.

wameeleza kwamba Tanzania ni kimbilio  la wengi na ni kisiwa Cha amani na  mataifa mbalimbali yana kimbilia  nchini kutokana  na   amani ambayo ipo tokea enzi na enzi na hii ni tunu kwa Taifa  letu 

" Mataifa ya bara la Afrika na hata mataifa ya nje  ya nchi ikiwemo Ulaya yamekuwa yakiitazama  Tanzania kama kioo  cha jamii katika suala zima la amani , utulivu,umoja na  mshikamano ndio Nguzo kubwa kwa watanzania",

Hata hivyo wamesema kilichojitokeza Oktoba 29 hadi Novemba 2,2025 hakipaswi kujirudia kabisa kwani ukiacha uharibifu uliojitokeza lakini baadhi ya watanzania wamepoteza maisha  jambo ambalo halijawahi kutokea wala kuzoeleka kwa wananchi kwani wamezoea kuona amani ikitawala nchini

Sambamba na hayo Miundombinu ambayo imejengwa kwa gharama kubwa zinazotokana na kodi ya watanzania imeharibiwa ,watu wamekatisha maisha yao kutokana na vurugu hizo lakini baadhi ya watanzania wamevunjiwa maduka yao,wameharibiwa mali zao kutokana na hali hiyo iliyojitokeza .

Kwa upande wake Mfanyabiashara mkubwa eneo la kariakooo, Shaban Kassimu lyomekyo  amezungumzia hali ya uvunjivu wa amani iliyojitokeza kwa baadhi ya makundi ya watu kufanya vitendo visivyo kubalika , yeye kwa nafasi yake kama mfanyabiashara analipongeza sana Jeshi la polisi kwa kazi kubwa iliyofanya.

Shaban amesema kuwa Jeshi la Polisi chini ya IGP Camirius Wambura linastahili kupongezwa sana kwa kusimama imara kuhakikisha watanzania wanabaki salama lakini kubwa zaidi eneo la kariakoo ambalo linakusanya maelfu ya wafanyabiashara linakuwa salama katika  kipindi chote Cha vurugu hizo.

Pia amesema unapozungumzia Jiji la Dar es Salaam ni lango la biashara maana yake unagusa moja kwa moja eneo la Kariakoo hivyo kitendo Cha Jeshi la Polisi kuimarisha Ulinzi katika kipindi chote Cha vurugu wanapaswa kupongezwa kwa nguvu zote 

Shaban amefafanua kuwa Jeshi hilo hususani Kanda Maalumu ya Dar es salaam iliyopo  chini ya Kamanda wa Polisi  SACP   Jumanne Murilo aliweza kupanga vijana wake kwa ustadi wa hali ya juu kiasi kwamba Kila lango la kuingia katika eneo la Kariakoo linakuwa na Ulinzi wa kutosha.

Amesisitiza kwamba eneo la Kariakoo ndio kitovu Cha biashara ambapo wafanya biashara wengi ndani na nje ya Dar es Salama wanakuja Kariakoo kufunga mizigo hivyo eneo hilo kama lingetikisika maana yake ni kwamba  hata uchumi wa nchi  ungetikisika  kwa kiasi kikubwa mno.

"Hapa nichukue fursa hii kulipongeza tena na tena  Jeshi letu la Polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya Ulinzi na Usalama wa nchi yetu kwa namna walivyojipanga na kuhakikisha Kariakoo inabaki salama na hivi sasa wafanyabiashara wanaendelea na shughuli zao kama kawaida ."amesema Shaban 

Angalia pale Kariakoo panabeba watu wangapi ,kwa maana ya wafanyabiashara wangapi alafu leo kama pangeharibiwa hali ingekuaje ?na ni kitu gani kingetokea?" ,amehoji ndugu Shaban .

Amesema Kariakoo ni lango kubwa mno la kibiashara ,wafanya biashara wakubwa wengi wapo  eneo hilo hivyo ndio maana anasema anapongeza sana Jeshi kwa namna lilivyojipanga kuhakikisha  eneo hilo linakuwa salama .

Ameongeza kuwa Jeshi walifanikiwa kuweka vizuizi katika eneo la magomeni kwa maana ya barabara ya Morogoro lakini pia Tazara kuingia barabara ya Uhuru inayotokea Buguruni hadi kufika kariakoo na Mivunjeni kwa barabara ya Kilwa hakuna mtu kuingia mjini kwa maana ya Kariakoo.

"Nataka nisema kazi kubwa imefanyika ,unajua Kariakoo kama nilivyosema uchumi wa nchi unategemea hapo kwa asilimia kubwa ,Kariakoo Kuna maduka makubwa ya vipodozi ,Kuna maduka makubwa ya nguo ,pia katika eneo la Jangwani kule kuna wauzaji wakubwa wa vifaa vya pikipiki na eneo la Gerezani kuna maduka makubwa ya  vifaa vya umeme."amesisitiza 

Niseme nampongeza Kamanda Murilo na Jeshi lake kwa ujumla kwa kazi kubwa na nzuri waliofanya  kwa kipindi chote cha vurugu na hata Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt .Samia Suluhu Hassan aliposema shughuli za wananchi zirudi kama awali siku Ile ya Novemba,3 mwaka huu kama Kariakoo ingeharibiwa ingekuwa haijasaidia kutokana na uhalisia wa kibiashara eneo hilo.

Kariakoo inapokea wageni kutoka nchi jirani kama vile Malawi,Zambia ,Burundi ,Kenya ,Uganda ,Rwanda ,wote hao wanakuja Kariakoo kufungasha bidhaa kwa ajili ya kupeleka katika nchi zao hivyo Kwa kifupi hali ingekuwa mbaya sana sana kama eneo hilo lingeathiriwa.

Lakini licha ya hayo bidhaa zote zinazotoka Nchini china kwa asilimia kubwa Kariakoo ndio kutovu chake kwa maana zinafikia hapo ndio zinasafirishwa kwenda katika mataifa mbalimbali hasa katika nchi zile ambazo zinatumia bandari ya Dar es Salaam 

Shaban amesema kuwa licha ya uwepo wa wafanyabiashara wa kubwa lakini kundi kubwa la wamachinga wanaofanya shughuli zao katika Jiji la Dar es Salaam kwa asilimia kubwa wanategemea wafanyabiashara wakubwa kutoka Kariakoo hivyo kitendo Cha kuilinda Kariakoo Jeshi la Polisi na vyombo vingine vya Usalama ni jambo kubwa mno wamefanya.

Mfanyabiashara huyu ambaye kwa asilimia kubwa biashara zake anazifanyia Kariakoo pia anamshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tamko lake alilotoa baada ya kuapishwa kuwa Rais wa kipindi Cha pili Cha awamu ya sita kwani kama asingefanya hivyo hali ingekuwa ngumu mno katika jamiii yetu.

Gharama za maisha ndani ya siku chache za vurugu zilizojitokeza maisha yalipaa sana kiasi kwamba watanzania wengi walilaani vikali vurugu hizo  na waliosababisha vurugu hizo huku baadhi ya wananchi wakiomba watanzania kutochezea tena amani iliyopo na iliyodumu kwa miaka mingi 

Watanzania hao walisema waasisi wa Taifa la Tanzania kwa maana Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Mzee Aman Abeid Karume  walifanya kazi kubwa ya kuunganisha umoja ,mshakamano miongoni mwetu bila kubaguana kwa makabila ,rangi , wala jinsia ya mtu badala yake ni utanzania wetu tu.

Amesema pia viongozi hao waliotangulia mbele ya haki walisisitiza watanzania kuilinda amani na kwamba Tanzania ndio nchi yetu na wote wanaoizunguka ni jicho la utulivu wao na amani yao iko Tanzania na sio mahali pengine .

Hivyo nikiwa sehemu ya mtanzania niendelee kulipongeza Jeshi la Polisi na vyombo vingine vyote vya Ulinzi na Usalama katika nchi yetu kwa namna walivyorejesha amani ,Usalama katika Taifa  na niwaombe watanzania wenzangu kilichotokea kimetokea na kamwe kamwe tusiruhusu tena hali hiyo amesisitiza  Shaban 

Amemaliza kwa  kumshukuru Rais Dkt. Samia kwa kuendelea kuwa mlezi na mzazi namba moja wa Taifa letu tunamuombea Kila lenye heri katika safari yake mpya ya uongozi wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania .

 Ibariki Tanzania Mungu wabariki Watanzania

 

CHAMA cha Mawakili wa Serikali kinatoa Pongezi za dhati kwa Mheshimiwa Hamza Saidi Johari kwa kuaminiwa na kuteuliwa kwa Mara ya pili mfululizo kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Kwa Sifa na Ubobevu alionao ni dhahiri anazo Sifa za kumfanya kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwani tukirejea Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ibara ya 59 inabainisha wazi kuhusu nafasi na sifa za Mwanasheria Mkuu wa Serikali kama ifuatavyo:

Ibara ya 59.- (1)

Kutakuwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano ambaye katika ibara zifuatazo za Katiba hii atatajwa tu kwa kifupi kama “Mwanasheria Mkuu” ambaye atateuliwa na Rais.

(2) Mwanasheria Mkuu atateuliwa kutoka miongoni mwa watumishi wa umma wenye sifa ya kufanya kazi za uwakili au watu wenye sifa ya kusajiliwa kuwa wakili, na ambaye amekuwa na sifa hizo mfululizo kwa muda usiopungua miaka kumi na tano.

Kwa mujibu wa kipengele hicho cha Katiba, ni wazi kwamba uteuzi wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali si wa kisiasa bali unatokana na uzoefu na sifa za kitaaluma. Hivyo basi, ni muhimu kwa kila mmoja wetu kutambua kuwa viongozi wa umma, hasa wale wanaoteuliwa kwa mujibu wa Katiba, hupitia taratibu za kisheria na kiutendaji kabla ya kuteuliwa.

Taarifa zozote zinazotolewa zisiso sahihi kuhusu viongozi hawa ni kitendo kinachoweza kuathiri heshima ya taasisi za umma na kupotosha jamii.

Ni wajibu wa kila Mtanzania kutafuta taarifa sahihi kutoka katika vyanzo rasmi kama vile Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali au tovuti rasmi za serikali kabla ya kueneza au kuamini taarifa mtandaoni.

Aidha Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza Saidi Johari ana uzoefu mkubwa na wa muda mrefu kwa zaidi ya miaka 20 kama mtumishi wa umma Mwandamizi aliyebobea katika eneo la majadiliano ya mikataba, Sheria za anga, Sheria ya Bahari na Sheria za udhibiti.

Zaidi ya hayo anazo Sifa stahiki za Kitaaluma, ikiwemo Shahada ya Kwanza ya Sheria (LL. B) na Shahada ya Uzamili ya Sheria (LL.M) katika Sheria ya Kimataifa kutoka Chuo Kikuu cha Kiev katika Jamhuri ya Ukraine na ana cheti cha Uongozi na Usimamizi kutoka Chuo cha Wafanyakazi wa Utawala cha India. Amehudhuria mafunzo mbalimbali ya kitaaluma na kuchapisha maandiko na vitini kadhaa katika

majadiliano ya Mikataba, Sheria ya Usafiri wa Anga na Sheria ya Bahari.

Vilevile amekuwa Mwenyekiti wa Shirika la Kimataifa la Huduma za Anga (CANSO) kwa Kanda ya Afrika na mjumbe wa Kamati Tendaji ya CANSO kwa miaka sita na Mwenyekiti wa Kamati ya Kisheria ya CANSO. Amewahi pia kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usafiri wa Anga ya SADC na Mwenyekiti wa Wakala wa Usalama wa Usafiri wa Anga wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (CASSOA).

Aidha, Mhe Hamza Johari ambaye ni mlezi wa Chama Cha Mawakili wa Serikali na ni Wakili namba moja kwa mujibu wa Sheria na ni Mjumbe wa Tume ya Utumishi wa Mahakama, Mwenyekiti wa Jopo la Ithibati ya Wasuluhishi, Wadadisi, Wasuluhishi na Waamuzi, Mwenyekiti wa Timu ya Wanasheria wa Serikali, Mjumbe wa Kamati ya Taifa ya Uendeshaji Uwekezaji na Mjumbe wa Kamati ya Mawakili (the Advocates Committee) . Pia aliwahi kuwa Mwanachama Mfadhili wa Taasisi ya Kimataifa ya Usafirishaji (CILT) iliyoanzishwa na Royal Charter 1929 (Uingereza), Mwanachama wa Maisha (lifetime), Chuo cha Wafanyakazi wa Utawala cha India na mwanachama wa Taasisi ya Wakurugenzi nchini Tanzania.

Mhe. Hamza Saidi Johari amefanya kazi kama Mkurugenzi Mkuu katika Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania kwa miaka tisa akitekeleza Sheria ya Usafiri wa Anga, Sura ya 80 ya Sheria. Amekuwa Mhadhiri mgeni katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Chuo Kikuu cha Mzumbe na Chuo Kikuu cha Alexandria (Misri) katika Sheria za Kimataifa za Bahari na Sheria za Kimataifa za Usafirishaji (Ardhi, Anga na Bahari).

Ameshiriki katika majadiliano ya miradi kadhaa ya Serikali kuhusu bandari za baharini, usafiri wa anga na migogoro ya kimataifa ya bweni kama Mwenyekiti wa Timu za Majadiliano za Serikali (GNT) na Mjumbe wa Kikosi Kazi mbalimbali cha Kitaifa na Kamati za Uongozi kama ifuatavyo:

1. Mjumbe wa Timu ya Kikosi Kazi cha Taifa kuhusu mgogoro wa Mpaka kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Malawi;

2. Mjumbe wa Timu ya Kikosi Kazi cha Taifa kuhusu mgogoro wa Mpaka kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Burundi;



3. Mjumbe wa Timu ya Kikosi Kazi cha Taifa kuhusu mgogoro wa Mpaka kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Uganda;



4. Kushirikishwa kama mtaalam wa maoni ya kisheria na Serikali ya Japani juu ya mzozo kati ya Japan na Uchina kuhusu Kisiwa cha Senkaku;



5. Mpatanishi Kiongozi wa Timu ya Serikali kuhusu Mikataba ya Huduma za Ndege baina ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Marekani, Canada, Uingereza, Ufaransa, Italia, Hispania, China, Russia, Falme za Kiarabu, Ujerumani, Uholanzi, Afrika Kusini, Oman, Korea Kusini, Morocco na Kenya;

6. Mwenyekiti wa Timu ya Majadiliano ya Serikali kuhusu marekebisho ya Mkataba wa Makubaliano kati ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania na Huduma za Makontena ya Kimataifa (TICTS);



7. Mwenyekiti wa Timu ya Majadiliano ya Serikali kuhusu marekebisho ya Mkataba wa Wanahisa na Miamala mingine ya Kibiashara kati ya Serikali na PUMA Energy;

8. Mwenyekiti wa Timu ya Majadiliano ya Serikali kuhusu marekebisho ya Makubaliano ya Wanahisa kati ya Serikali na TIPPER;

9. Mwenyekiti wa Timu ya Majadiliano ya Serikali kuhusu marekebisho ya Mkataba wa wenye Hisa kati ya Serikali na Progress Rail ya Marekani kwa ajili ya ununuzi wa Locomotives kwa Shirika la Reli Tanzania;

10. Mwenyekiti wa Timu ya Majadiliano ya Serikali kuhusu kusitisha Mkataba wa Makubaliano kati ya Mamlaka ya Bandari Tanzania na Huduma za Kimataifa za Makontena Tanzania (TICTS);



11. Mpatanishi Kiongozi wa Timu ya Majadiliano ya Serikali ya Ubia na kuendeleza Makubaliano ya Kiserikali (IGA) kwa ajili ya kuendeleza Bandari ya Dar es Salaam kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Emirate ya Dubai;

12. Mpatanishi Kiongozi wa Timu ya Majadiliano ya Serikali kwa ajili ya majadiliano ya Mkataba wa Serikali Mwenyeji (HGA) kati ya Serikali na DP World ya U.A.E;

13. Mpatanishi Kiongozi wa Timu ya Majadiliano ya Serikali kwa ajili ya majadiliano ya Mkataba wa Makubaliano kati ya Serikali na DP World ya U.A.E;

14. Mpatanishi Kiongozi wa Timu ya Majadiliano ya Serikali kwa ajili ya Mkataba wa Ukodishaji kati ya Serikali na DP World ya U.A.E kwa ajili ya kukodisha ardhi katika Bandari ya Dar es Salaam;

15. Mpatanishi Kiongozi wa Timu ya Majadiliano ya Serikali kwa ajili ya majadiliano ya Mkataba wa Makubaliano kati ya Serikali na Bandari ya Adani ya India kwa ajili ya huduma za makontena katika Bandari ya Dar es Salaam;

16. Mpatanishi Kiongozi wa Timu ya Majadiliano ya Serikali ya majadiliano ya Mkataba wa Ukodishaji kati ya Serikali na Bandari ya Adani ya India kwa ajili ya ukodishaji wa ardhi katika Bandari ya Dar es Salaam.

Huyo ndiye Hamza Saidi Johari Wakili namba moja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mmakonde mzaliwa wa wilaya ya Mtwara Vijijini, Tarafa ya Ziwani kata ya Nalingu.
Imetolewa na CHAMA CHA MAWAKILI WA SERIKALI TANZANIA

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mhe. Sergei Kiriyenko, Mjumbe Maalum wa Rais wa Jamhuri ya Shirikisho la Urusi Mhe. Vladimir Putin mara baada ya kuwasili Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 06 Novemba, 2025.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mhe. Sergei Kiriyenko, Mjumbe Maalum wa Rais wa Jamhuri ya Shirikisho la Urusi Mhe. Vladimir Putin, Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 06 Novemba, 2025.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Ujumbe Maalum kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Shirikisho la Urusi Mhe. Vladimir Putin uliowasilishwa kwake na Mhe. Sergei Kiriyenko, Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 06 Novemba, 2025.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Mjumbe Maalum wa Rais wa Jamhuri ya Shirikisho la Urusi Mhe. Vladimir Putin, Mhe. Sergei Kiriyenko, Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 06 Novemba, 2025.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amemuapisha Dkt. Mwinyi Talib Haji kuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar.

Hafla ya uapisho imefanyika leo Novemba 6, 2025, Ikulu, Zanzibar.

Dkt. Mwinyi Talib Haji ameteuliwa tena kushika nafasi hiyo baada ya kuitumikia katika kipindi kilichopita.

Hafla hiyo imehudhuriwa na Jaji Mkuu wa Zanzibar, Mhe. Khamis Ramadhan Abdalla, Mhandisi, Zena Ahmed Said, Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi, Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama, pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali, Chama Cha Mapinduzi na Dini.






JUKWAA la Wahariri Tanzania (TEF) linafuatilia kwa karibu na limepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za vifo vya Watanzania wenzetu, wakiwamo wanahabari na wengine waliojeruhiwa.

Siku ya tukio tulipokea taarifa za vifo vya vijana na askari polisi. Baadhi ya wananchi waliwasiliana nasi wahariri, kuomba msaada wa kuulizia walipo ndugu zao.

Jukwaa linatoa pole kwa Watanzania waliopoteza ndugu, jamaa na marafiki katika vurugu zilizotokea wakati na baada ya uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025, katika kilichoanza kama maandamano ya amani, lakini kuishia kwenye uchomaji wa magari, vituo vya mafuta, nyumba, kadhia zingine za kiafya kwa waliopiga kura na hatimaye mauaji ya raia na askari.

TEF inawakumbuka kwa heshima wanahabari na Watanzania waliouawa katika vurugu hizi, kwani wameacha pengo kubwa katika tasnia ya habari, kazini na familia zao. Pia tunawapa pole wote waliojeruhiwa katika matukio hayo.

Jukwaa limerejea utamaduni wa Taifa letu wa amani na utulivu na kuakisi yaliyotokea yakazaa maafa haya. Tunafahamu yapo maumivu makubwa kila upande, ila tunaomba sasa tusimame pamoja kama taifa, tuzungumze na kujisahihisha, ili kamwe haya yasitokee tena katika ardhi ya Tanzania.

Jukwaa linatoa mwito kwa Mamlaka kufanya uchunguzi wa kina na kuhakikisha haki inatendeka. Tunaisihi Serikali kuanzisha mchakato wa maridhiano haraka, ili kuponya majeraha kwa pande zote. Tunaomba kila upande mchakato ukianza uwe tayari kushiriki kama nchi tumalize kadhia hii milele.

Tumeshuhudia madhara ya amani kupotea na tulikofika, tujizuie kama nchi isitokee tena. Mungu awape uponyaji wa haraka walioumia, azilaze mahali pema peponi roho za waliopoteza uhai, na atupe nguvu ya kusimama kama nchi tujisahihishe. Mungu ibariki Tanzania.

Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF)
Deodatus Balile Mwenyekiti Novemba 6,




Na Mwandishi Wetu, Lindi
HIFADHI ya Urithi wa Utamaduni wa Dunia ya Magofu ya Kale ya Kilwa Kisiwani na Songo Mnara wilayani Kilwa imeendelea kuwa kivutio kikubwa kwa watalii kutoka ndani na nje ya nchi, ambapo tarehe 31 Oktoba 2025 ilipokea jumla ya watalii 147 kutoka mataifa mbalimbali duniani waliowasili hifadhini humo kwa kutumia meli ya kifahari iitwayo SH Diana, kwa lengo la kutalii na kujionea vivutio vya kihistoria vilivyopo katika eneo hilo.

Watalii hao walitoka katika nchi 13 zikiwemo Ufaransa, Australia, Ubelgiji, Canada, Uingereza, Uswisi, Ujerumani, Cyprus, New Zealand, Marekani, Urusi, Uturuki na Ukraine. Ziara hiyo iliratibiwa na kampuni za Savannah Tours Ltd kwa kushirikiana na Black Willow Safaris.

Akizungumza wakati wa mapokezi ya watalii hao, Kamanda wa Hifadhi hiyo, Mhifadhi Mwandamizi Kelvin Stanslaus, alisema ujio wa wageni hao ni ishara njema kwa ukuaji wa utalii wa urithi nchini, hasa ikizingatiwa umuhimu wa Kilwa Kisiwani na Songo Mnara kama maeneo yaliyosajiliwa na UNESCO kuwa Urithi wa Dunia tangu mwaka 1981.

“Tunayo furaha kubwa kuona wageni kutoka pande mbalimbali za dunia wakija kujionea historia adhimu ya Kilwa, ambayo ni alama muhimu ya biashara ya kimataifa ya karne za kati kati ya Afrika Mashariki na Dunia,” alisema Afisa huyo.

Aidha, wageni hao walipata fursa ya kutembelea majengo ya kihistoria ikiwemo Msikiti Mkongwe, na Kasri la Sultani, ambapo walivutiwa na usanifu wa majengo ya mawe pamoja na simulizi za kihistoria zinazoambatana na maeneo hayo kutoka Kwa Maofisa wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania - TAWA waliobobea na kutopea katika masuala ya malikale.

Kwa mujibu wa TAWA ambayo ndiyo wasimamizi wa hifadhi hiyo, ujio wa meli hiyo ni sehemu ya mwendelezo wa jitihada za Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii katika kuimarisha utalii wa urithi, hususan katika maeneo ya bahari, malikale na visiwa vyenye thamani ya kihistoria.

MERIDIANBET, jukwaa linaloongoza kwa michezo ya kubashiri nchini Tanzania, linawapa wachezaji fursa ya kipekee ya kuingia kwenye burudani ya mchezo wa kasino mtandaoni wa Super Heli na kujishindia simu nne za kisasa za Samsung A26.

Hii sio tu mchezo wa kufurahisha, bali ni nafasi ya kweli ya kubeba zawadi ya gharama kubwa bila juhudi za ziada. Kila Jumatatu, mshindi mmoja atatangazwa, wakiwapa wachezaji fursa za kushinda simu za kisasa wiki baada ya wiki mwezi huu.

Kwenye Super Heli, unaweka dau lako, na helikopta inaanza kupaa, huku odds zikiongezeka kwa kasi na ushindi wako ukikua. Siri ya kushinda ni rahisi, toa pesa kabla helikopta haijalipuka, kwani ukichelewa, unaweza kupoteza dau lako.

Ukijisajili Meridianbet unapewa bonasi ya mizunguko ya bure kucheza michezo ya kasino mtandaoni lakini pia una machaguo ya kutosha ukiwa unabashiri na Meridianbet, kila chaguo lina odds kubwa. Jisajili kwa kupiga *149*10# au tovuti www.meridianbet.co.tz

Ili kujiunga na promosheni hii ya kipekee, unahitaji tu akaunti halali ya Meridianbet, ambayo unaweza kufungua kwa urahisi kupitia tovuti ya meridianbet.co.tz au kwa kupakua app ya Meridianbet. Mara tu unapojisajili, anza kucheza Super Heli, na kadri unavyocheza mara nyingi, ndivyo nafasi zako za kuwa mmoja wa washindi wanne wa simu hizi zinavyoongezeka.

Promosheni hii ni fursa ya kipekee ya kufurahia mchezo wa Super Heli huku ukiwa na nafasi ya kujizawadia simu ya kisasa pamoja na ushindi wa pesa taslimu kulingana na dau lako na ustadi wako.
Usipitwe na nafasi hii ya kushinda, ingia sasa meridianbet.co.tz, fungua akaunti yako, cheza Super Heli mara nyingi, na uwe miongoni mwa mabingwa watakao tembea na simu mpya za Samsung A26.


KWA dau dogo tuu leo hii unaweza kubadilisha maisha yako kwani ODDS KUBWA zipo Meridianbet. Mechi nyingi za Europa leo zipo kwaajili yako. Unangoja nini?. Suka jamvi lako hapa.

OGC Nice atakuwa mwenyeji wa Freiburg ya Ufaransa huku nafasi ya kuondoka na ushindi akipewa yoyote kwani Odds za kibabe zipo kwenye mechi hii. Je nani kuondoka na ushindi kati yao. Bashiri na Meridianbet sasa.

Nae Celtic Glasgow atakuwa ugenini dhidi ya FC Midtylland ya kule Denmark ambao leo hii kushinda mechi hii wana ODDS 3.40 kwa 2.10. Mara ya mwisho kukutana ilikuwa ni 2022 ambapo mgeni aliondoka na ushindi. Je leo nani kushinda?. Tandika jamvi hapa.

Pia SK Sturm Graz watakuwa wenyeji wa Nottingham Forest ya kule Uingereza ambao mechi yao iliyopita walishinda. Wenyeji wao walipoteza hivyo ushindi wa leo ni muhimu sana. Mechi hii ina machaguo zaidi ya 1000 Meridianbet. Jisajili hapa.

Michezo ya kasino kukutajirisha leo cheza Keno, Aviator, Poker, Roullette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

FC Utrecht watawaleta kwao FC Porto ya kule Ureno huku akiwa ndiye anayepewa nafasi nzuri ya kushinda mechi hii kwa ODDS 1.75 kwa 4.50. Mwenyeji anahitaji kushinda siku ya leo. Je wewe beti yako unaiweka kwa nani siku ya leo?. Beti hapa.

Kwa upande wa Bologna wao wataumana dhidi ya SK Brann huku Meridianbet wakimpa nafasi kubwa ya kushinda mwenyeji. Wewe una nafasi pia ya kuondoka na mshindo wa maana leo. Ingia na utengeneza mkwanja mrefu leo.

AS Roma atakuwa ugenini dhidi Glasgow Rangers ya kule Scotland. Tofauti ya pointi kati yao hadi sasa ni 3 pekee kwani mwenyeji yeye mpaka sasa hajashinda mechi yoyote. Nafasi ya kushinda na Meridianbet zaidi ya Mamilioni ipo hapa. Tengeneza pesa yako kubwa sasa.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Bw. Hamza Said Johari kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 05 Novemba, 2025.
Wageni mbalimbali waliohudhuria hafla ya uapisho wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Bw. Hamza Said
Johari, Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 05 Novemba, 2025.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emanuel Nchimbi katika picha ya pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Bw. Hamza Said Johari, mara baada ya tukio la uapisho, Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 05 Novemba, 2025.
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndugu. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongoza Kikao Maalumu cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa iliyoketi jijini Dodoma, leo Jumatano, Novemba 5, 2025.

Kikao hicho pamoja na Mambo mengine kimefanya uteuzi wa wagombea wa nafasi za Spika na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na nafasi ya Spika na Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar.




 


BAADA ya jana kushuhudia mitanange ya maana siku ya jana, leo hii tena kitawaka sana ambapo nafasi ya kuondoka na mpunga ipo nje kabisa. Tandika jamvi lako la ushindi na Meridianbet.

Vijana wa Enzo Maresca Chelsea leo hii watakuwa ugenini kusaka ushindi dhidi ya Qarabag FK ambao mechi iliyopita walipoteza. The Blues wao walishinda wakiwa nyumbani. Je leo hii wanaweza kuendeleza ushindi wao?. Bashiri hapa.

Pia kule Uholanzi Ajax baada ya kupoteza mechi iliyopita, leo hii atakuwa kibaruani dhidi ya Galatasaray ambao walishinda. Hivyo leo hii ushindi ni muhimu sana kwa wmenyeji kwani mpaka sasa kwenye mechi 3 ambazo amecheza hajashinda hata moja. ODDS KUBWA zipo mechi hii. Jisajili sasa.

Nao Club Brugge watamenyana dhidi ya FC Barcelona ambapo tofauti ya pointi kati yao ni 3 pekee. Kila timu inataka ushindi siku ya leo huku wakali wa ubashiri Tanzania Meridianbet wakimpa nafasi kubwa ya kushinda Barca wakiwa na ODDS 1.55 kwa 5.20. Tandika jamvi hapa.

Piga pesa kwenye michezo ya kasino kama vile Keno, Aviator, Poker, Roullette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Bashiri mechi ya Benfica vs Leverkusen huku mwenyeji yeye akiwa hana pointi yoyote mpaka sasa. Kwa upande wa Mjerumani yeye ana pointi 2 pekee hadi sasa. Unaweza ukatengeneza mkwanja wako kupitia mechi hii sasa. Ingia na usuke jamvi hapa.

Vijana wa Pep Guardiola, Manchester City watakuwa Etihad kusaka ushindi dhidi ya Borussia Dortmund ambapo mara ya mwisho kukutana ilikuwa 2022 na hakuna ambaye alikuwa mbabe kati yao. Machaguo zaidi ya 1000 yapo kwenye mechi hii. Suka jamvi hapa.

ODDS KUBWA zipo mechi hii ya Marseille vs Atalanta ambapo mara ya mwisho kwenyeji yeye alifungwa huku mgeni yeye akitoa suluhu. Pointi 3 ni muhimu kwa hawa wote siku ya leo. Je nani kuondoka kifua mbele?. Beti sasa.

Newcastle United ya Eddie Howe watakuwa nyumbani pia kusaka pointi tatu dhidi ya Athletic Bilbao ambapo mara ya mwisho kukutana ilikuwa ni 2022 kwenye mechi ya kirafiki ambao The Magpies walishinda. Je leo hii Bilbao kulipa kisasi?. Beti hapa.
The Open University of Tanzania (OUT), under the UNESCO Chair in Teacher Education and Curriculum, has launched a new training module titled “Competency-Based Digital Skills Training for STEM Teachers.” The initiative aims to empower Science and Mathematics teachers with digital tools and innovative teaching approaches to enhance learning outcomes.

Held online via Zoom on October 15, 2025, the launch brought together 30 STEM teachers from nine secondary schools in Iringa District Council, along with officials from Ministry of Education, Science and Technology, the President’s Office - Regional Administration and Local Government (PO-RALG), Iringa District Education Office and participating school head teachers.

Project Leader, Dr. Edephonce Nfuka said the training supported by the Global Partnership for Education - Knowledge and Innovation Exchange (GPE-KIX) through the International Development Research Centre (IDRC) Canada, in collaboration with partner institutions from Nigeria, Bhutan and India. He noted that the module builds on the earlier Connected Learning for STEM (CL4STEM) project (2021-2024) and now focuses on competency-based digital skills, responsible AI use and sustainability through a Training of Trainers (ToT) approach.

Prof. Elifas Bisanda, Chairperson of the UNESCO Chair, commended the OUT team’s leadership and urged teachers to embrace innovative teaching methods. Mr. Ohadi Nosa, Head of Nyerere High School, announced plans to extend the training to all 53 district schools by 2026, citing positive outcomes from earlier projects.

Representing MoEST, Mr. Musa Mnyeti and Mr. Sitta Peter Ndamayape (on behalf of the District Education Officer) applauded the initiative, affirming government support and highlighting its alignment with national education and digital strategies.

The launch marks a major milestone toward strengthening teacher professionalism and advancing Tanzania’s vision of inclusive, technology-driven education.


Na Mwandishi wetu, Ngorongoro.

Wageni kutoka mataifa mbalimbali wanaotembelea eneo la Hifadhi ya Ngorongoro wameendelea kufanya shughuli za utalii kwa amani, usalama na utulivu na kufurahia vivutio mbalimbali vya utalii vilivyoko hifadhi ya Ngorongoro  

Akizungumzia katika geti kuu la kuingia hifadhi ya Ngorongoro Afisa Uhifadhi Mkuu Idara ya huduma za Utalii na Masoko Ngorongoro Bw. Peter Makutian amesema kuwa katika kipindi chote cha uchaguzi mkuu wa Tanzaia hadi kufikia tarehe 5 novemba, 2025 wageni takribani 1200 kutoka mataifa mbalimbali wameendelea kutembelea hifadhi hiyo na kufanya utalii.

 “Ngorongoro  tunaendelea kupokea wageni  katika kipindi hiki cha msimu wa wastani na tuna Imani kuelekea kipindi cha sikukuuu za mwisho wa mwaka watalii watakuwa wengi zaidi .” alisema Makutian.

Mmoja wa wageni  kutoka Nchini Colombia Isabella Jerónimol  ameeleza kuwa ametembeleaa Tanzania akiwa na familia ya watu 26 ambapo chaguo lao  ni kuona hifadhi ya Ngorongoro kutokana na hali ya utulivu, amani, ukarimu pamoja na utajiri wa vivutio vya utalii vilivyopo.

Bw. Dunstan Sospeter kutoka Dar es Salaam akiwa katika hifadhi ya Ngorongoro na Familia yake ameelezea kufurahishwa na hali ya usalama na kushuhudia utalii wa wanyamapori, uhifadhi endelevu, Wanyama mbalimbali ambao wanaweza kuonekana kwa pamoja katika muda ambapo pia ametumia fursa hiyo  na familia yake kutembelea  Bonde la Olduvai, mchanga unaohama na kreta ya Ngorongoro.













Top News