Serikali imeombwa kupunguza gharama za usajili wa vyombo vya habari mtandaoni (Online Media) ili kutoa fursa kwa vijana wengi zaidi kujiajiri.

Ombi hilo limetolewa na Jumamosi Januari 24, 2026 na Mkurugenzi wa BMG Media, George Binagi wakati wa hafla fupi ya kupokea tuzo maalum kutoka YouTube baada ya chombo hicho cha mtandaoni kufikisha wafuasi (Subscribers) laki moja.

Binagi amesema licha ya Serikali kupunguza gharama za usajili wa online media kutoka shilingi milioni moja hadi laki tano, bado watengeneza maudhui mtandaoni wanaomba gharama hizo kupungua hadi laki moja hatua itakayosaidia vijana wengi wakiwemo wahitimu wa vyuo vya uandishi wa habari kujiajiri na kuajiri wenzao.

Pia Binagi amebainisha kuwa kuanzia mwaka huu 2026 watengeneza maudhui mtandaoni wameanza kukatwa asilimia tano ya mapatano wanayopata mtandaoni na kuwasilishwa serikalini wakati huo huo wakilipa kodi jambo ambalo limewaongezea mzigo wa kulipa kodi mara mbili na hivyo kuomba changamoto hiyo kutatuliwa.

Katika hatua nyingine, Binagi amewashukuru wadau, wasomaji na wafuasi (subscribers) wa BMG Media kwa mchango wao uliofanikisha kupata tuzo hiyo na kuahidi kuendelea kutengeneza maudhui yenye weledi unaokidhi mahitaji yao

Akizungumza kwenye hafla hiyo, Mwenyekiti wa MISATAN na MPC, Edwin Soko amesema mitandao ya kijamii kwa sasa ni fursa kwa vijana kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa ajira nchini, hivyo amehimiza matumizi sahihi ya mitandao hiyo.

Kuhusu gharama za usajili na kodi mbalimbali, Soko ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye hafla hiyo, amesema atafikisha suala hilo kwa mamlaka husika kupitia vikao mbalimbali vya wadau wa habari ambavyo vimekuwa vikifanyika kwa lengo la kuboresha sekta hiyo.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Maabara yaMkemia Mkuu wa Serikali, Christopher Kadio, akiongea wakatiakifunga Mkutano wa Jukwaa la Kitaifa la Wadau wa Kemikalilililofanyika katika Ukumbi wa Cate Hoteli, jijini Morogoro January 23, 2026.
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Maabara ya MkemiaMkuu wa Serikali na Mwenyekiti wa Kamati ya Bodi ya Usimamizi na Udhibiti waKemikali Prof. Edda Vuhahula, akiongea wakati wa mkutano wa Jukwaa la kitaifala Wadau wa Kemikali, Januari 23, 2026.
Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko, akiongea kabla yakumkaribisha Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Maabara yaMkemia Mkuu wa Serikali, Christopher Kadio (hayupo pichani) kufunga Mkutanowa Jukwaa la kitaifa la Wadau wa Kemikali, Januari 23, 2026.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaalam ya Kemikali, Dkt. Clarence Mgina, akiwasalimuwadau wa Jukwaa la kitaifa la Wadau wa Kemikali lililofanyika mkoani Morogoro, Januari 23, 2026.
Mkurugenzi wa Huduma za Udhibiti, Daniel Ndiyo, akitoa ufafanuzi wa maswalimbalimbali yaliyoulizwa na washiriki wa Jukwaa la Kitaifa la Wadau wa Kemikalikwa mwaka 2026 ambalo lilihitimishwa katika Hoteli ya Cate, Morogoro, Januari23, 2026.
Wadau wa Kemikali, Hussein Dewji, kutoka Simba Supply Chain Solutions Ltd, naEng. Harryson Rwehumbora kutoka ATZ Group Ltd. Arusha, (picha ya chini) wakitoa wasilisho fupi kuhusu namna wanatekeleza majukumu yao kwakushirikiana na Mamlaka katika siku ya pili ya Jukwaa la Kitaifa la Wadau waKemikali lililofanyika Morogoro, Januari 23, 2026.
Wadau wa Kemikali, Nyakolema Magige, kutoka Waja General Co. Ltd. (picha yajuu) na Shukuru Swaleh kutoka Usangu Logistics (picha ya chini) wakitoawasilisho fupi kuhusu utekelezaji wa majukumu yao kwa kuzingatia Sheria yaUsimamizi na Udhibiti wa Kemikali katika Jukwaa la Kitaifa la Wadau wa Kemikali, Januari 23, 2026.
Washirikia wa Mkutano wa Jukwaa la Kitaifa la Wadau wa kemikali wakifuatiliamada mbali mbali zilizowasilishwa na wataalam kwenye mkutano wa Jukwaa la Kitaifa la Wadau wa Kemikali lililohitimishwa Morogoro, Januari 23, 2026.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu waSerikali, Christopher Kadio (katikati) akiwa na viongozi wengine wa Mamlaka(mstari wa mbele) pamoja na wadau wa kemikali ambao waliwasilisha madakuhusu majukumu yao (waliosimama nyuma) wakati wa mkutano wa Jukwaa la Kitaifa la Wadau wa Kemikali Januari 23, 2026.
Mwakilishi wa Wadau wa mkutano wa Jukwaa la Kitaifa la Wadau wa Kemikali, Happyness Shumbusho, akitoa neno la shukrani kwa niaba wa washiriki wenginewa mkutano wakati wa siku ya pili ya mkutano huo uliofanyika Cate HoteliMorogoro.
Mratibu wa mkutano wa Jukwaa la Kitaifa la Wadau wa Kemikali, AnastaziaRugaba, akiwasilisha maazimio ya mkutano wa Jukwaal a Kitaifa la Wadau waKemikali kabla ya kufungwa kwa mkutano huo uliofanyika Morogoro, Januari23,2026.

Na Mwandishi Wetu

MKURUGENZI Mkuu wa Bodi ya Utalii Tanzania(TTB) Ephraim Mafuru amesema kuzinduliwa kwa meli mpya kubwa na ya kisasa ya MV New Mwanza kunakwenda kufungua fursa katika sekta ya utalii ambapo sasa watalii watazunguka nchi za Afrika Mashariki kwa kutumia usafiri wa meli hiyo ambayo ni rahisi na nafuu.

Mafuru ametoa kauli hiyo leo alipokuwa akizungumza baada ya Tanzania kuandika  historia kubwa katika uwekezaji ya miundombinu ya usafiri, usafirishaji na utalii katika Bara la Afrika.

“Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imewekeza  Sh.bilioni 120 katika meli hii. Watanzania wenzangu na Waafrika kwa ujumla Bodi ya Utalii Tanzania tunatoa mwito tutumie meli hii kuendeleza biashara zetu zinazozunguka katika  Afrika Mashariki kwasababu Ziwa Victoria ndio ziwa kubwa kuliko maziwa yote katika  Afrika

“Inauwezo wa kubeba mizigo mingi na kusafirisha abiria lakini pia kuleta watalii. Kwawale mlioko sekta ya utalii mtakubaliana nami ya kwamba watalii wanaozunguka katika Afrika Mashariki kutoka Kenya tunawageni  240,000 , na kutoka Uganda ni wageni kama 60,000 na wengi wanatumia barabara ,wengi wanatumia safari za anga 

“Leo hii Serikali ya Awamu ya Sita imeidhihirishia dunia ya kwamba watalii sasa wanaweza kuzunguka Afrika Mashariki kwa kutumia usafiri rahisi na nafuu kupitia meli hii ya Mv New Mwanza,”amesema Mafuru kuhusu kuzinduliwa kwa meli hiyo sambamba na fursa ambazo zitapatikana katika kukuza utalii.

Awali wakati anazungumza meli hiyo Mafuru amesema ndani ya wiki mbili zilizopita yameshuhudiwa makubwa katika historia ya nchi yetu na leo katika Jiji la Mwanza Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Mwigulu Nchemba ameongoza viongozi mbalimbali wa Serikali na Chama na wawekezaji walioko ndani ya Tanzania kushuhudia uzinduzi wa meli hiyo kubwa ya MV New Mwanza 

“Kwamara ya kwanza katika bara la Afrika yaani  vyombo vinavyotumika katika maji baridi katika maziwa Tanzania inakuwa nchi ya kwanza kwa ujenzi na uzinduzi wa meli kubwa MV New Mwanza ambayo leo imezinduliwa jijini Mwanza ikiwa na uwezo wa kubeba abiria 1200 kwa wakati mmoja,magari madogo 20 na magari makubwa matatu 

“Sasa unaweza kujiuliza tani 400 za mizigo zina uwezo wa kubebwa na meli hii, kwa Watanzania wenzangu ambao tunaweza kupiga picha tani 400 maana yake nini ? Ukichukua yale magari makubwa semitraila tani 400 ni magari 13.

Hebu  piga hesabu msururu wa yale magari ,urefu wa hii meli ni karibu uwanja mmoja wa mpira kwani uwanja wa mmoja wa mpira una mita 92.”








 Na WANDISHI WETU

MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi  ya Chama Cha  Mapinduzi (CCM)  Wilaya ya Temeke, Hamis Slim, amewakata  viongozi  wa  mabaraza, kamati za utekelezaji za kata na matawi  za jumuiya hiyo kuvunja makundi  yaliyotokana na uchaguzi mkuu wa Oktoba 29 , 2029 na kufanyakazi kwa ushirikiano.

Ameyasema hayo  Dar es Salaam, leo katika ziara ya Kamati ya Utekelezaji ya  Jumuiya hiyo Wilaya ya Temeke katika Kata za Kiburugwa na Kibondemaji inayo lenga kuwashukuru   wanachama wa jumuiya hiyo kwa ushindi mkubwa wa  CCM na kuimarisha uhai wa jumuiya.

Slim, amesema  uchaguzi umekwisha  hivyo ni wakati muafaka wa kuvunja makundi, kusameheana, kupendana na  kuhudumia jumuiya kwa  ufanisi na weledi.

“Tunawapongeza  Jumuiya ya Wazazi mmeafanya kazi nzuri  katika uchaguzi mkuu na kuipatia  ushindi wa kishindo  CCM na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan. Sasa ni wakati wa kuleta maendeleo. Tuzike tofauti zetu zilizotokana na uchaguzi. Mwiba ulipoingia ndipo unapotokea,”amesema Slimu.

Pia amewataka kuishi kwa hofu ya Mungu, kuheshimu katiba ya CCM, kanuni na  viongozi na wanachama.

“Binadamu  anahamika kwa mambo matatu, Jambo la kwanza ni jinsi anavyo jifahamu mwenyewe. Jambo la pili ni namna  watu wengine wanavyo mfahamu na jambo la tatu ni nama anavyo fahamika na Mungu. Tusidharauliane kwa sababu mamlaka  hata za dunia na viongozi wake  zimetoka kwa Mungu,”amesema Slim.

Aidha  Slim,  ametumia ziara hiyo kutoa pole kwa wanachama wa jumuiya hiyo, CCM na  wananchi wote kwa ujumla kwa matukio yaliyojitokeza Oktoba 29, 2025 katika uchaguzi mkuu na kuwakumbusha umuhimu wa kutunza amani  ya taifa.

Naye Katibu wa Jumuiya ya Wazazi  Wilaya ya Temeke, Emmanuel  Itatiro,  amewataka  viongozi wa jumuiya hiyo katika ngazi za mashina, matawi na kata, kutekeleza wajibu wao kwa kufuata Katiba ya CCM na jumuiya hiyo, kanuni na miongozo.

Pia, amewahimiza kuwajibika  ipasanyo hususan kuitisha vikao vya kikatiba na kushughulikia  changamoto za  wananchi, hususa katika sekta za elimu, afya, malezi  na mazingira.

Ziara hiyo ya Kamati ya Utekelezaji ya  Jumuiya ya Wazazi   Wilaya ya Temeke, itapita katika kata zote za wilaya hiyo.






WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika ibada ya kumuaga aliyekuwa Gavana wa kwanza wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Mzee Edwin Mtei, akimtaja kuwa kiongozi mahiri, mzalendo na nguzo muhimu katika historia ya uchumi na demokrasia ya Tanzania.

Akizungumza katika ibada hiyo ya mazishi iliyofanyika nyumbani kwa marehemu Tengeru, Dkt. Nchemba alisema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anatambua mchango mkubwa wa marehemu kwa Taifa na Serikali mara zote itaenzi  mchango wake mkubwa katika uchumi na demokrasia nchini.

Waziri Mkuu alisema Mzee Mtei alikuwa miongoni mwa Watanzania wachache waliobahatika kuhudumu katika nyadhifa zote kuu za sekta ya fedha, ikiwemo kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Waziri wa Fedha na mwakilishi wa Tanzania katika taasisi za fedha za kimataifa, mchango uliompa heshima ya kipekee kitaifa na kimataifa.

Alisema katika maisha yake ya utumishi wa umma, marehemu alitambulika kwa kusimamia misingi ya uadilifu, uaminifu, uzalendo, bidii na kumcha Mungu na kwamba mchango wake uliweka msingi imara wa taasisi za kifedha na nidhamu ya uchumi wa Taifa.

Dkt. Nchemba alibainisha kuwa Mzee Mtei pia alikuwa miongoni mwa waasisi wa demokrasia ya vyama vingi nchini, akiwa mwanzilishi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), hatua iliyochangia kwa kiasi kikubwa kuimarisha mfumo wa kisiasa na uhuru wa mawazo nchini.

Katika kuenzi mchango wa marehemu kwa vitendo, Waziri Mkuu alitoa maelekezo mahsusi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo, akisisitiza kuwa hatua hizo ni sehemu ya kudumisha misingi ya maendeleo, haki na uzalendo aliyoyaishi marehemu.

Kuhusu miundombinu ya barabara, Waziri Mkuu alielekeza ukamilishwaji wa taratibu za manunuzi na kuanza mara moja kwa ujenzi wa barabara ya njia nne katika kipande cha Tengeru hadi Usa River, akieleza kuwa mkandarasi anatakiwa kuingia eneo la kazi bila kuchelewa.

Aidha, kwa kipande cha Usa River hadi Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) chenye urefu wa kilomita 28, Waziri Mkuu alisema usanifu wa mradi ulikuwa umefikia takribani asilimia 80, na akaelekeza Wizara ya Ujenzi kwa kushirikiana na TANROADS kukamilisha haraka usanifu uliobaki na kutangaza zabuni mara moja, akisisitiza kuwa fedha za utekelezaji wa mradi huo tayari zipo.

Katika hatua nyingine, aliagiza ukamilishwaji wa barabara na madaraja katika maeneo korofi kati ya Kilimanjaro na Arusha ifikapo Februari 20, 2026, akielekeza Wizara ya Ujenzi na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha kuhakikisha barabara hiyo inafunguliwa na kuanza kutumika kwa lengo la kuondoa adha kwa wananchi.

Kuhusu mgogoro wa ardhi katika eneo la Mringa Estate, Waziri Mkuu alielekeza marekebisho yafanyike ndani ya mwezi mmoja kwa mujibu wa makubaliano ya awali, ili wananchi waliopaswa kunufaika na eneo hilo wapate haki yao. Aliagiza Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Kamishna wa Ardhi pamoja na maafisa ardhi husika kusimamia kikamilifu utekelezaji wa agizo hilo, hususan katika eneo lililonunuliwa na kampuni ya Bajuta Enterprises.

Waziri Mkuu alisisitiza kuwa utekelezaji wa maelekezo hayo ni sehemu ya dhamira ya Serikali ya kuendeleza maendeleo jumuishi, kusimamia haki za wananchi na kudumisha heshima ya viongozi waliolitumikia Taifa kwa uadilifu na uzalendo akiwemo Mzee wetu Mtei.







• Mazoezi yajenga afya, mahusiano na tija kazini

• Ushirikiano wa taasisi waimarishwa kupitia michezo

• Eng. Samamba asisitiza uwajibikaji na uadilifu kusukuma matokeo


DODOMA

Watumishi wa Wizara ya Madini na Taasisi zake wamehimizwa kufanya mazoezi ya mwili mara kwa mara kama njia ya kuimarisha afya, kujenga mshikamano na kuongeza tija katika utekelezaji wa majukumu ya kazi.

Wito huo umetolewa leo Januari 24, 2026 jijini Dodoma na Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, alipofungua Bonanza la tatu la michezo lililowakutanisha watumishi wa Wizara ya Madini na Taasisi zake, ikiwemo Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST), Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Tume ya Madini pamoja na Taasisi ya Uwazi na Uwajibikaji katika Rasilimali Madini, Mafuta na Gesi Asilia (TEITI).

Akizungumza katika uzinduzi wa bonanza hilo, Mhe. Mavunde amesema kuwa, mazoezi ya viungo ni nguzo muhimu ya afya njema kwa mtumishi, ufanisi na tija kazini hivyo kuna umuhimu wa watumishi kujitokeza kwa wingi katika shughuli za michezo ili kuimarisha afya zao na kuendeleza mshikamano kazini.

Aidha, Waziri Mavunde amezitaka taasisi zote zilizo chini ya Wizara ya Madini kuendelea kufanya kazi kwa bidi ili kuleta tija na matokeo chanya katika Sekta ya Madini mbele ya Watanzania na jumuiya ya kimataifa.

“Tunayo dhamana kubwa ya kuwatumikia Watanzania. Michezo inatupa fursa ya kuimarisha afya, kudumisha amani, mshikamano na upendo, na kujenga umoja wetu kama familia moja ya sekta ya madini,” amesema Mavunde.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Eng. Yahya Samamba, amewataka watendaji wa sekta hiyo kusimamia rasilimali za madini kwa weledi, uwajibikaji na uadilifu ili kuhakikisha sekta inaendelea kuwanufaisha Watanzania na kuongeza mchango wake katika uchumi wa Taifa.

Mhandisi Samamba amefafanua kuwa, Sekta ya Madini imeendelea kufanya vizuri, ambapo mpaka sasa mchango wa Sekta ya Madini katika Pato la Taifa umefikia asilimia 10.1 na makusanyo Serikali kufikia shilingi trilioni 1.071.

Ameeleza kuwa mafanikio hayo yametokana na maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na usimamizi madhubuti wa Wizara kwa kushirikiana na Taasisi zake.

Ameongeza kuwa juhudi za kuimarisha usalama katika shughuli za uchimbaji zimezaa matunda, huku akisisitiza kuendelea kuzingatia kikamilifu taratibu za afya, usalama na mazingira.

Eng.Samamba amewaelekeza Maafisa Madini Mkazi , kusimamia sehemu zenye mashimo hatarishi zisimamishwe mara moja na migogoro ya wachimbaji itatuliwe kwa haraka, hasa wakati huu ambapo bei ya dhahabu inaendelea kupanda.

Naye, Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Ramadhani Lwamo, ametoa wito kwa watumishi wa Wizara ya Madini na Taasisi zake kuendelea kudumisha amani, mshikamano na upendo katika utekelezaji wa majukumu yao kwa manufaa ya Taifa.








Mkurugenzi wa Utafiti Viwanda TRIDO na Muwakilishi wa Mgeni rasmic, Humfrey Ndosi, katikati akizungumza wakati wa uzinduzi wa miaka 15 ya Gs1 Tanzania, uzinduzi huo umefanyika jijini Dar es Salaam leo Jamuari 24, 2026.

Na Mwandishi Wetu
TAASISI ya Utambulisho wa Bidhaa Tanzania (GS1 Tanzania) imeadhimisha miaka 15 tangu kuanzishwa kwake, hatua iliyoelezwa kuwa na mchango mkubwa katika kukuza biashara, viwanda na ushindani wa bidhaa za Tanzania katika masoko ya ndani na nje ya nchi.

Maadhimisho hayo yamefanyika leo Januari 26, 2026 jijini Dar es Salaam yakihusisha wadau wa sekta binafsi, taasisi za umma na wataalamu wa teknolojia ya biashara.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa GS1 Tanzania, Fatma Kange, amesema GS1 imepitia safari ndefu ya mabadiliko tangu ilipoanzishwa, ikianza na shughuli za siku moja na sasa kuelekea mifumo ya kisasa inayohusisha teknolojia za kidijitali.

Amesema GS1 Tanzania inaendelea kubadilika kulingana na mahitaji ya soko na mabadiliko ya teknolojia, huku maandalizi ya maadhimisho makubwa yakipangwa kufanyika rasmi Septemba mwaka huu.

“Kama taasisi, tunajiuliza tunatoka wapi, tuko wapi na tunaelekea wapi. Teknolojia zinabadilika kwa kasi, na GS1 Tanzania ina wajibu wa kuhakikisha wanachama wake hawabaki nyuma,” amesema Fatma,

Pia amebainisha kuwa mabadiliko hayo yanalenga kuwasaidia wazalishaji na wafanyabiashara kutambulisha bidhaa zao kwa ufanisi zaidi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Utafiti Viwanda TRIDO na Muwakilishi wa Mgeni rasmic, Humfrey Ndosi, amesema GS1 imekuwa chombo muhimu katika kusaidia viwanda vya ndani kuboresha ushindani wa bidhaa zao, hasa kwa kuwezesha utambulisho unaokubalika kimataifa.

Ameeleza kuwa kabla ya uwepo wa GS1, wazalishaji wengi walikumbana na changamoto za kuingiza bidhaa zao sokoni, hali iliyowalazimu wengine kutegemea masoko ya nje.

Licha ya hayo aliwasilisha salamu za wizara na kuipongeza GS1 Tanzania kwa mchango wake katika kukuza sekta binafsi.

Amesema serikali itaendelea kushirikiana na taasisi kama GS1 katika kujenga mazingira wezeshi ya biashara na kuimarisha miundombinu ya kiuchumi.

Ameeleza kuwa mafanikio ya GS1 Tanzania yametokana na ushirikiano mpana kati ya serikali na sekta binafsi, ikihusisha taasisi mbalimbali zikiwemo TRIDO, TBS, BRELA, SIDO, TPSF, ZNCC, TCCIA, CTI, TAHA pamoja na vyama vya wazalishaji wa mazao na viungo.

Katika maadhimisho hayo, GS1 Tanzania imetangaza kuendelea na mabadiliko ya kidijitali, ikiwemo uzinduzi wa mfumo wa 2D migration, unaolenga kuboresha zaidi utambulisho wa bidhaa za Tanzania na kuongeza ufanisi katika minyororo ya thamani ya biashara.

Ufunguzi wa Maadhimisho hayo yametoa wito kwa Watanzania kujiamini, kujituma na kutumia fursa zilizopo katika mazingira bora ya biashara yaliyowekwa na serikali.








Matukio mbalimbali wakati wa uzinduzi wa miaka 15 ya Gs1 Tanzania. ambapo Kilele chaku kufanyika Septemba mwaka huu.

 Na Benny Mwaipaja, Tanga


Naibu Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Laurent Luswetula, ametoa rai kwa Watanzania kutembelea vivutio vya asili vilivyopo nchini ili kukuza utalii wa ndani pamoja na kuongeza pato la Taifa.

Mhe. Luswetula ametoa rai hiyo jijini Tanga alipotembelea Hifadhi ya Mapango ya Amboni, ikiwa ni sehemu ya utalii wa ndani, akiwa katika ziara ya kikazi mkoani humo.

Alisema kuwa mapango ya Amboni ni tunu ya kipekee ambayo nchi imejaaliwa na Mwenyezi Mungu, yenye kila aina ya maajabu ambayo Watanzania na wageni kutoka nje ya nchi wanatakiwa kuyashuhudia.

Wakizungumza kuhusu Hifadhi ya Mapango ya Amboni, yaliyoko chini ya usimamizi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, Mhifadhi wa Hifadhi hiyo, Bw. Ramadhan Rashid na Muongoza Watalii, Bw. Muhsin Rajabu, walisema kuwa eneo hilo lina simulizi nyingi za kijiografia na historia ya wapigania uhuru wa nchi.

Aidha walisema kuwa mazingira yake ya ndani ya hifadhi yameboreshwa na kurahisisha ziara za wageni wanaotembelea eneo hilo ambalo licha ya kuwa na mapango, pia lina Wanyama wa msituni na majini wakiwemo mamba walioko kwenye mto Mkurumuzi unaopita karibu na hifadhi hiyo.

Mapango ya Amboni Tanga yana umri wa zaidi ya miaka 150, yakiwa na ukubwa wa ekari 39.5 na urefu wa mita 755 kutoka usawa wa Bahari, yanapatikana kilometa 8 kaskazini mwa mji wa Tanga ambapo tafiti zinaonesha kuwa eneo hilo lilikuwa chini ya maji kwa takriban miaka milioni 20 iliyopita.

Katika tukio lingine, Naibu Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Laurent Luswetula, alitembelea Hifadhi ya Mikoko iliyoko Jijini Tanga, na kuupongeza Uongozi wa Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) kwa ubunifu wao na kuigeuza hifadhi hiyo kuwa sehemu ya kitega uchumi cha Taifa pamoja na kuwa eneo la utalii kwa wananchi na wageni wengine kutoka nje ya nchi wanatembelea mkoa wa Tanga.
Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb), (mwenye kofia na shati la draft) kushoto, akisikiliza maelezo kutoka kwa Mhifadhi wa Hifadhi ya Mapango ya Amboni, yaliyoko mkoani Tanga, Bw. Ramadhani Rashid, alipotembelea mapango hayo ikiwa sehemu ya utalii wa ndani alipokuwa kikazi mkoani humo.

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb), (mwenye kofia na shati la draft) kushoto, akisikiliza maelezo kutoka kwa Muongoza Watalii wa Hifadhi ya Mapango ya Amboni, yaliyoko mkoani Tanga, Bw. Muhsin Rajabu, alipotembelea mapango hayo ikiwa sehemu ya utalii wa ndani alipokuwa kikazi mkoani humo.
Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb), (mwenye kofia na shati la draft) wa pili kulia, akiwa ndani ya Hifadhi ya Mapango ya Amboni, yaliyoko mkoani Tanga, ambapo alipatiwa maelezo ya kufurahisha kuhusu historia iliyopo ndani ya mapango hayo, alipokuwa kikazi mkoani humo.

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb), akitoka katika moja ya mapango yaliyo katika Hifadhi ya Mapango ya Amboni, yaliyoko mkoani Tanga, alipotembelea mapango hayo ikiwa sehemu ya utalii wa ndani alipokuwa kikazi mkoani humo.

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb), akifurahia maajabu ya baadhi ya miamba katika mapango yaliyo katika Hifadhi ya Mapango ya Amboni, mkoani Tanga, alipotembelea mapango hayo ikiwa sehemu ya utalii wa ndani alipokuwa kikazi mkoani humo.

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb), (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Viongozi na Watumishi wa Wizara ya Fedha, Wilaya ya Tanga na Wasimamizi wa Hifadhi ya Mapango ya Amboni Tanga, baada ya kuhitimisha ziara ya kuyatembelea mapango hayo ikiwa ni seheu ya utalii wa ndani, akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Tanga. Kulia kwake ni Kaimu Kamishna wa Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha, Wizara ya Fedha, Bi. Dionisia Mjema.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Wizara ya Fedha-Tanga)


Farida Mangube Mvomero, Morogoro 

Vijana na wanawake wa vijiji vitano vikiwemo vya Lubungo, Mafuru na Mingo Wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro, wamepata fursa ya kujikomboa kiuchumi kupitia mradi wa uzalishaji wa mzao ya bustani kibiashara unaotekelezwa na Washirika wa Wahitimu Wajasiriamali wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUGECO).

Mradi huu unatekelezwa kwa ushirikiano wa SUGECO na Programu ya Beyond Farming Collective (BFC), inayofadhiliwa na Bill na Melinda Gates Foundation.

Simtanu Yohane ni Afisa Kilimo huduma za Ugavi Wilaya ya Mvomero, amesema mradi huu utaleta mageuzi makubwa kwa jamii hasa kwa vijana na wanawake kwa kuwapata nafasi ya kujiajiri kupitia kilimo cha bustani kibiashara.

 "Kilimo cha kisasa kitaongeza uzalishaji na kutoa masoko ya uhakika kwa mazao," alisema Afisa Kilimo huyo

Kwa upande  wake Mkurugenzi wa SUGECO Bw. Revocatis Kimario amesema mradi huo umegharimu zaidi ya  shilingi Bilioni 1 fedha zitakazotumika kuweka miundombinu ya umwagiliaji, Teknolojia mpya na vifaa vya kisasa katika shughuli za kilimo ikiwemo matumizi ya nishati ya jua na mfumo wa umwagiliaji.

Kimario amesema mradi huo utakuwa na miundombinu yote  hivyo ni wajibu wa vijana waliopata fursa kutumia mradi huo kuzalisha mazao ya bustani huku akiwahakikishia kuwepo kwa masoko ya uhakika wa mazao yatakayozalishwa.

"Kupitia Mradi huu ambao tumeweka miundombinu masingi ya kuwezesha uzalishaji tunampa kijana eneo la kuzalishia lenye miundombinu ya masingi, tumechimba visima 4 na mabwawa, kijana anapewa ekali moja hadi tatu na tunampa haki ya tumia eneo hilo kwa kipindi Cha miaka mitatu lengo letu ndani ya hicho kipindi Cha miaka mitatu azalishe auze na atengeneze Fedha anunue Ardhi yake na ajimilikishe yeye mwenyewe". Amesema Mkurugenzi wa SUGECO.

Nao wakazi wa Kijiji Cha Lubungo unaotekelezwa Mradi huo wamesema 
 kupitia Mradi huo vijana watanufaika na mageuzi ya kilimo kwani awali walikuwa wanalima kilimo Cha msimu kwa kutegemea mvua.

"Sisi tunalima Mbaazi, mtama na mahindi lakini kilimo chetu ni chakutegemea mpaka msimu lakini ujio wa SUGECO na mradi wa kilimo Cha bustani sisi vijana Sasa tutanufaika nacho". Amesema Maneno Issa mkazi wa Lubungo 


Mradi huo umedhaminiwa na Program ya Beyond Farming Collective (BFC) kwa ufadhili wa Bills and Melinda Gates Foundation umelenga kupanua mfumo wa kizimba Bussiness world Model (KBM) ambao unatekelezwa na Washirika wa Wahitimu wajasiliamali wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA (SUGECO).









Top News