Na Seif Mangwangi, Michuzi TV Arusha

MAKAMU WA Rais Dkt Emmanuel Nchimbi amewataka waandishi waendesha ofisi kuongeza jitihada katika kutekeleza majukumu yao bila woga na kwamba Serikali inatambua mchango wao mkubwa kwa kazi wanayoifanya na ndio sababu Rais Dkt Samia amekubali kuwa mlezi wa chama hicho.

Aidha amewataka kutoa ushauri mzuri Kwa viongozi wao Kwa kutumia uzoefu waliokuwa nao pale yanapotokea mazingira ya kutoa ushauri katika taasisi hizo kwa kuwa itawajengea heshima na kufanya kuaminika.

Dkt Nchimbi akizungumza Leo Mei21, 2026 kwenye mkutano mkuu wa chama hicho unaendelea katika kituo cha Mikutano cha Tanzania Convention Center Ngurdoto Arusha, amesema waendesha ofisi ni watu muhimu na hawapaswi kubezwa Kwa namna yoyote Ile.

" Taasisi yenu inaaminika na ndio sababu Rais amekubali kuwa mlezi wenu, niwaombe tu kuendelea kuwa waaminifu na mfanye kazi Kwa uadilifu wakati wote wa utekelezajibwa majukumu yenu," amesema.

Akisoma risala ya chama hicho Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi waendesha ofisi Tanzania (TAPSEA),Bi.Zuhura Songambele Maganga amekemea tabia ya udhalilishaji inayoendelea kufanywa kupitia mitandao ya kijamii kuhusu kada ya Waandishi waendesha ofisi.

" Sisi kama waandishi waendesha ofisi maarufu kama Makatibu Muhtasi tunasikitishwa na tabia ya baadhi ya udhalilishaji inayoendelea huko mitandaoni, hii ni kada inayojiheshimu na watendaji wamekuwa na maadili na wanafuata miongozo ya Serikali," amesema.

Amesema kada hiyo ya waandishi waendesha ofisi isidhalilishwe kama inavyofanyika kwenye mitandao ya kijamii na majukwaani na kwamba ni taasisi inayoheshimika na miongoni mwao wako wake wa viongozi serikalini hivyo hawawezi kufanya mambo machafu ofisini kwao.

Amesema tangu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kukubali kuwa maezi wa chama hicho, wamekuwa na ujasiri wa kutekeleza majukumu yao na kujiamini.

Aidha Bi.Zuhura amemuomba Rais Samia kuwaongezea mshahara endapo uchumi utaruhusu kutokana na majukumu mengi ambayo wamekuwa wakiyatekeleza kama waandishi waendesha ofisi.

Waziri wa nchi ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa umma, Ridhiwani kikwete, amesema katika mwaka 2026/2027, Serikali imepanga kuongeza ajira mpya 45,000 ikiwemo kada ya Waandishi waendesha ofisi Ili kuboresha na kurahisisha utumishi wa umma nchini.








-Pia yaanza maandalizi kuelekea kuadhimisha miaka 10 tangu ilipoanzishwa,Rais Samia kuwa

Mgeni rasmi

-Yazingumzia pia uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali katika hospitali hiyo,idadi ya wagonjwa waliohudumiwa



Na Said Mwishehe,Michuzi TV

UONGOZI wa Hospitali ya Benjamin Mkapa umeanza rasmi maandalizi ya maadhimisho ya miaka 10 tangu kuanzishwa kwake, sambamba na uzinduzi wa harambee ya kuchangisha fedha kwa ajili ya kuwa na Mfuko maalum utakaowezesha huduma za matibabu ya upandikizaji uloto kwa watoto wenye ugonjwa wa selimundu pamoja na huduma za upandikizaji figo.

Akizungumza leo katika kikao na Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa, Profesa Abel Makubi, amesema hospitali hiyo imeendelea kuwa tegemeo kubwa kwa wananchi kwa kuhudumia takribani watu milioni 10 kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania pamoja na wagonjwa kutoka nje ya nchi.

Amesema kwamba Julai 15, 2026, katika kilele cha maadhimisho ya miaka 10 ya hospitali hiyo, wanatarajia kufanya harambee yenye lengo la kupanua huduma za kibingwa, ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Kutokana na hali hiyo, Prof. Makubi amesema pia hospitali hiyo imekuwa moja ya vituo muhimu vya tiba utalii nchini huku akifafanua kupitia harambee hiyo, hospitali inalenga kukusanya jumla ya Shilingi bilioni 7 ndani ya kipindi cha miaka miwili, fedha zitakazosaidia kugharamia matibabu kwa wagonjwa 100.

“Kati yao, watoto 50 wanatarajiwa kufaidika na matibabu ya selimundu kupitia upandikizaji uloto, huku wagonjwa wengine 50 wakipatiwa huduma ya upandikizaji figo,” amesema Prof. Makubi na kuongeza tayari Sh.bilioni zimeshapatikana hivyo wanaendelea kuziomba taasisi za umma na binafsi pamoja na wananchi kuchangia kwa hiyari katika mfuko huo.

Hata hivyo, Prof. Makubi aliishukuru Ofisi ya Msajili wa Hazina pamoja na taasisi zake ambazo, kwa kushirikiana na wadau wengine, zimefanikiwa kuchangia kiasi cha Shilingi bilioni 4 hadi sasa.

“Kama mnavyofahamu, gharama za matibabu ni kubwa sana kwa wagonjwa. Tuna kila sababu ya kuendelea kumshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye alichangia Shilingi bilioni moja nje ya bajeti kwa ajili ya matibabu ya wagonjwa mbalimbali.

“Mchango huo ulisaidia wagonjwa waliokuwa hawana uwezo wa kugharamia matibabu yao, ambapo yeye alilipia gharama zote. Jambo hilo lilirejesha furaha kwa watoto, familia zao pamoja na wagonjwa wa figo waliopatiwa matibabu.”

Kuhusu mafanikio ya hospitali hiyo amesema kwa sasa ina watumishi 1,073, wakiwamo madaktari bingwa 100 sambamba na kuwa na vitanda 450 kwa ajili ya huduma za wagonjwa.

Pia amesema kwa sasa inatoa huduma za kibingwa 20, zikiwamo huduma za kibingwa za juu 18. Baadhi ya huduma hizo ni upandikizaji uloto, upasuaji wa moyo kwa kufungua kifua, uchunguzi wa moyo, kuzibua mishipa ya damu, upasuaji wa uti wa mgongo, upasuaji kwa kutumia matundu madogo pamoja na ubadilishaji wa nyonga na magoti.

“Hospitali imepata mafanikio makubwa kutokana na uwekezaji wa Serikali kuanzia awamu ya nne hadi ya sita, ambapo kiasi cha Shilingi bilioni 283 kimewekezwa katika majengo na vifaa tiba.

“Hivyo, unaweza kuona namna hospitali ilivyojidhatiti katika kuimarisha na kuboresha huduma za afya,” amesema huku akisisitiza hospitali hiyo imeendelea kutoa huduma za tiba utalii kwa raia kutoka nje ya nchi, ambapo baadhi yao huja moja kwa moja kufuata huduma hospitalini hapo.

“Kwa mfano, mwaka jana tuliwahudumia wagonjwa 2,897 kutoka Burundi. Pia wapo wagonjwa wanaokuja moja kwa moja kutoka nchini humo pamoja na wengine kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.”

Ametaja mafanikio mengine ni kufanyika kwa maboresho makubwa ya mifumo ya TEHAMA ambayo imerahisisha utoaji wa huduma bora kuanzia usajili wa wagonjwa. Pia wameanza makundi matano ya huduma huru yanayowezesha mawasiliano ya moja kwa moja na wagonjwa.









MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi wa Taasisi ya Tanzania Women Empowement Network (TAWEN) Balozi Amina Salum Ali, amesema viongozi na watumishi wanao wajibu kuhakikisha taasisi zao zinakuwa mfano wa kuigwa kutekeleza maelekezo ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan na sera ya kitaifa ya nishati safi.

Ameyasema hayo leo katika semina maalumu ya matumizi ya nishati safi, iliyoandaliwa na TAWEN na kushirikisha wakuu wa shule za sekondari za Wilaya ya Ubungo na wadau wa nishati na taasisi za kifedha.

Balozi Amina, amesema watumishi wanapaswa kuwa mabalozi wa mabadiliko hayo ya kuachana na nishati chafu na kuhamasisha familia na jamii zinazo wazunguka kutumia nishati safi.

Amesema dhamira ya Rais Dk. Samia, ambaye ni kinara wa matumizi ya nishati safi ya kupikia ni kuona jamii nzima ya watanzania inatumia nishati hiyo ambapo taasisi za elimu haziwezi kuachwa nyuma.

"Hivyo basi nyie wakuu wa shule ni watu muhimu katika kusaidia jitihada hizo za Rais Dk. Samia, kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kutumianishati safi. Tunataka kila mtu katika jamii atumie fursa hii. Tumsaidie rais kuibeba ejenda hii muhimu,"ameeleza Balozi Amina.

Ameeleza, Rais Dk. Samia, ametoa maelekezo kwa taasisi zikiwamo shule za bweni kutumia nishati safi hivyo kupongeza TAWEN kutoa elimu hiyo kwa wakuu wa shule ambao ni wadau muhimu wa utekelezaji wa ajenda hiyo.

"Vilevile ninaipongeza TAWEN kwa kazi kubwa ya kuunganisha wadaiu, kuendesha makongamano ya kitaifa na kimataifa na kuhamasisha uwekezaji katika nishati safi. Hii ni ishara ya uongozi thabiti na dhamira ya kweli kuleta mabadiliko chanya kwa taifa letu,"ameeleza.

Awali Mkurugenzi Mtendaji wa Tawen, Florence Masunga, amesema lengo la semina hiyo ni kuhamasisha wakuu wa shule kutumia nishati safi shuleni, kuwapa fursa zinazo patikana kupitia uwekezaji katika nishati safi na fursa za kifedha hususan uwekezaji.

"Pia semina hii ili lenga kuwapa elimu wakuu wa shule ambayo itawafanya kuwa mabalozi wazuri wa matumizi ya nishati safi na kusaidia serikali chini ya Rais Dk. Samia, kufikia malengo ya watu wote katika jamii yetu kutumia nishati hii,"amesema Masunga.

Ameeleza, sekta ya nishati safi ina firsa nyingi ambapo wakuu wa shule wanaweza kuwekeza na kujiingizia kipato kitakacho wasaidia hata baada ya kustaafu.

Ameeleza TAWEN itaendelea kutoa elimu hiyo kwa jamii nzima ya kitanzania na hata nje ya nchi kwa kuibeba ajenda hiyo muhimu iliyoasisiwa na Rais Dk. Samia, ambayo inasaidia pia kulinda mazingira, kudumisha afya na ustawi wa jamii salama.

Ofisa Elimu ya Sekondari wa Wilaya ya Ubungo, Benedict Sandy, amewahimiza wakuu wa shule kuanza kutekeleza maelekezo ya serikali ya kutumia nishati safi na kwamba semina hiyo iwe chachu kwao.

"Tunawashukuru TAWEN kwa semina hii. Sasa iwe chachu kwetu kuanza utekelezaji wa maagizo ya serikali na kuibeba ajenda ya Rais Dk. Samia. Tuwe mabalozi, tuipeleke elimu hii kwa wanafunzi nao waipeleke katika jamii,"alisema Sandy.

Miongoni mwa taasisi zilizoshiriki semina hiyo ni Shirika la Madini Tanzania (STAMICO), Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Benki ya NMB, UTT Amis, Taifa Gas na PSSSF.








-Serikali yaja na mkakati wa kuongeza uzalishaji, kutoa mizinga 11,000

Sekta ya ufugaji nyuki nchini imepata msukumo mpya baada ya Serikali kutangaza mpango wa kutoa mizinga 11,000 pamoja na mafunzo kwa zaidi ya wafugaji 3,000 katika mwaka wa fedha 2026/2027, hatua inayolenga kuongeza uzalishaji wa asali na kuinua uchumi wa wananchi wanaotegemea shughuli hiyo.

Hatua hiyo ilibainishwa katika mdahalo mkubwa wa wadau wa sekta ya nyuki uliofanyika mkoani Tabora, ukihusisha wafugaji wa nyuki, wataalamu wa misitu na nyuki, taasisi mbalimbali pamoja na wadau wa maendeleo kujadili mikakati ya kuimarisha ufugaji wa kisasa na kuongeza thamani ya mazao ya nyuki nchini.

Akizungumza katika mdahalo huo, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora, Bi. Upendo Joseph Haule, aliyemwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, alisema ufugaji wa nyuki umeendelea kuwa chanzo muhimu cha ajira na kipato kwa wananchi wengi, hasa wanaoishi jirani na maeneo ya misitu.

Alisema Serikali inaendelea kuhimiza matumizi ya teknolojia bora, mizinga ya kisasa na uwekezaji katika uchakataji wa mazao ya nyuki ili kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania katika soko la kimataifa.

“ Mkoa umeendelea kuhamasisha uwekezaji katika uchakataji wa mazao ya nyuki, matumizi ya teknolojia bora pamoja na kuongeza thamani ya bidhaa za nyuki. Pia umeanzishwa wazo la kuunda Kongani la Ushindani wa Asali ya Tabora (Tabora Honey Competitive Cluster),” alisema Bi. Haule.

Alisema lengo la kongamano hilo ni kuwakutanisha wadau wote wa mnyororo wa thamani wa mazao ya nyuki ili kuongeza ubora na ushindani wa asali ya Tabora katika masoko ya ndani na nje ya nchi.

Bi. Haule alionya kuhusu ongezeko la matukio ya moto wa misitu yanayohatarisha shughuli za ufugaji nyuki katika baadhi ya maeneo na kusisitiza umuhimu wa jamii kushiriki kikamilifu katika uhifadhi wa mazingira na vyanzo vya chakula vya nyuki.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki Wizara ya Maliasili na Utalii Bw, Daniel Pancrasi, alisema katika mwaka wa fedha 2025/2026 Serikali imetoa jumla ya mizinga 9,215 na kuwafikia wafugaji 4,934 kupitia mafunzo mbalimbali ya ufugaji wa kisasa wa nyuki.

Alisema katika mwaka ujao wa fedha, Serikali inalenga kuongeza utoaji wa mizinga hadi 11,000 sambamba na kuendelea kuwajengea uwezo wananchi ili sekta hiyo iwe chanzo kikubwa cha mapato ya kaya na taifa.

“Tunawaomba wananchi kuchangamkia fursa hii kwa kuingia kwenye ufugaji wa kisasa wa nyuki ambao una tija kubwa kiuchumi na kimazingira,” alisema Bw. Pancras.

Katika mdahalo huo, wadau walisisitiza umuhimu wa kuongeza thamani ya mazao ya nyuki kupitia usindikaji wa kisasa, ufungashaji bora na kuzingatia viwango vya ubora vinavyokubalika kimataifa ili bidhaa za Tanzania ziweze kushindana kwenye masoko ya nje.

Pia walipendekeza kuongezwa kwa mafunzo kwa vikundi vya wafugaji wa nyuki, hususan vijana na wanawake, ili waweze kushiriki kikamilifu katika uzalishaji, usindikaji na biashara ya mazao ya nyuki.

Wadau hao walieleza kuwa sekta ya nyuki ina uwezo mkubwa wa kuzalisha ajira, kuongeza mapato ya wananchi na kuchangia uhifadhi wa misitu, endapo uwekezaji wa kimkakati utaongezwa na ushirikiano kati ya Serikali, sekta binafsi na jamii utaimarishwa.







▪️Asisitiza ushirikiano wa kikanda katika kulinda rasilimali za ziwa
▪️Aagiza kuimarishwa kwa mifumo ya uokoaji na usalama majini
▪️Ataka matumizi ya teknolojia katika usimamizi wa rasilimali za maji


WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki zinapaswa kuendelea kushirikiana kulinda na kulihifadhi Ziwa Victoria kwa kuwa ni rasilimali muhimu inayogusa maisha, uchumi na mustakabali wa mamilioni ya wananchi wa ukanda huo.

“Ziwa Victoria si mali ya nchi moja pekee. Ni rasilimali inayotuunganisha kama Jumuiya na tunapaswa kushirikiana katika kulinda mazingira, usalama na uchumi unaotegemea ziwa hili,” amesema Dkt. Nchemba.

Amesema hayo leo Alhamisi, Mei 21, 2026 wakati akizindua rasmi Siku ya Ziwa Victoria na kufunga kilele cha maadhimisho ya kwanza yaliyofanyika katika Viwanja vya Nanenane Nyamhongolo jijini Mwanza.

Kauli mbiu ya maadhimisho hayo ilikuwa “Maji Yetu, Mustakabali Wetu: Tuungane kwa Uendelevu wa Bonde la Ziwa Victoria.”

Katika hotuba yake, Waziri Mkuu amesema maadhimisho hayo yanapaswa kuwa sehemu ya kuhamasisha usimamizi endelevu wa rasilimali za maji, kuimarisha mshikamano wa kikanda na kuongeza uwajibikaji wa pamoja katika kulinda mazingira ya Ziwa Victoria.

Aidha, amesema Serikali itaendelea kushirikiana na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika kuimarisha mifumo ya usalama majini, kudhibiti uharibifu wa mazingira na kuendeleza matumizi ya teknolojia katika usimamizi wa rasilimali za ziwa hilo.

“Sote tunawajibika kutunza mazingira ya Ziwa Victoria kwa manufaa ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo,” amesema.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesisitiza umuhimu wa kuimarishwa kwa mifumo ya uokoaji majini pamoja na matumizi ya mifumo ya kidijitali katika kufuatilia shughuli za uvuvi, ubora wa maji na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Pia ametoa wito kwa taasisi za utafiti kuendelea kufanya tafiti zitakazosaidia kupata suluhisho la changamoto mbalimbali zinazoathiri mazingira ya Ziwa Victoria ikiwemo ongezeko la magugu maji na uharibifu wa vyanzo vya maji.

Awali, Waziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema Tanzania itaendelea kuwa mstari wa mbele katika kulinda na kuhifadhi Ziwa Victoria kwa kuwa ni nguzo muhimu ya uchumi, usalama na maendeleo ya wananchi wa ukanda wa ziwa.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, James Ole Millya amesema Tanzania itaendelea kushirikiana na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika kuandaa na kutekeleza mipango ya pamoja ya kuhifadhi rasilimali za Bonde la Ziwa Victoria.

Naye Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Bonde la Ziwa Victoria, Masinde Bwire amesema maadhimisho hayo ni hatua muhimu ya kuimarisha dhamira ya pamoja ya nchi wanachama katika kulinda moja ya rasilimali kubwa za maji barani Afrika.

Wawakilishi kutoka Kenya na Uganda waliishukuru Tanzania kwa kuwa mwenyeji wa maadhimisho hayo na kusisitiza umuhimu wa ushirikiano wa kikanda katika kukabiliana na changamoto za uchafuzi wa mazingira, mabadiliko ya tabianchi na usalama wa majini ndani ya Ziwa Victoria.

Katika maadhimisho hayo, Waziri Mkuu pia alizindua rasmi Siku ya Ziwa Victoria ambayo sasa itaadhimishwa kila mwaka tarehe 21 Mei katika nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.










Na Mwandishi Wetu,Michuzi TV

SHIRIKA la Umeme Tanzania(TANESCO)Mkoa wa Kinondoni Kusini jijini Dar es Salaam limewakumbusha wateja wake hasa wateja wakubwa kuhakikisha wanalipa ankra za umeme (bill)kwa wakati.

Akizungumza leo Mei 20,2026 katika kikao kati ya TANESCO Mkoa wa Kinondoni Kusini na Wateja Wakubwa  kilichokuwa na lengo la kujadiliana masuala mbalimbali Meneja wa TANESCO mkoa huo Adam Abdul ametumia bafasi hiyo kusisitiza ulipaji wa ankara za umeme kwa wakati ili kuwezesha shirika kuendelea kutoa huduma katika maeneo mengine.

“Tumekutana na Wateja Wakubwa katika mkoa wetu wa Kinondoni Kusini ,tumepokea changamoto zao na nyingi tumezifanyia kazi.Lakini nitumie nafasi hii kuwaambia wateja wetu wote walipe bill(Ankra)za umeme kwa wakati kwasababu zinapolipwa nasi zinatusaidia kufanya kazi na kuhakikisha upatikanaji wa umeme katika maeneo yote.”

“Kupitia kikao hiki wateja wetu wakubwa tumekubaliana wataendelea kulipa bill zao vizuri ,”amesema Abdull  na kufafanua pia  kwa sasa upatikani wa umeme umendelea kuimarika na hivyo kuondoa malalamiko kwa wateja wao.

Pia amesema kwa sasa TANESCO wanafanya kazi nzuri na malalamiko kwa wateja yamepungua na hata wateja wetu wakubwa katika kikao hawakuwa na malalamiko makubwa zaidi ya kuomba ankra kwa upande ziwahishwe ili nao walipe kwa wakati.

Kuhusu kikao cha TANESCO Kinondoni Kusini na Wateja Wakubwa,Abdull amesema kimekuwa na mafanikio makubwa na kwamba vikao vya namna hiyo ni endelevu kwani vinasaidia pande zote mbili kupata taarifa zenye lengo la kuboresha huduma.

Kwa upande wao baadhi ya wateja wakubwa waliohudhurika kikao hicho wametoa pongezi kwa TANESCO Mkoa wa Kinondoni Kusini kuandaa kikao ambacho kimewapa nafasi na kueleza yale ambayo wanaona yanakwenda kuboresha huduma za upatikanaji umeme . 









Top News