.jpeg)

Tanzania ni miongoni mwa nchi barani Afrika zenye matumizi makubwa zaidi ya pombe haramu, hali inayoleta hatari kubwa kwa afya ya umma, wataalamu wameonya.
Haya yalibainishwa leo katika mkutano uliowakutanisha wadau kutoka Serikalini na Sekta Binafsi kujadili namna ya kukabiliana na tatizo hili linalotishia maisha na kudhoofisha ukusanyaji wa mapato kutoka sekta halali ya pombe.
Mkutano huo, wenye kaulimbiu ya "Kuungana Kupambana na Pombe Haramu Nchini Tanzania," ulisisitiza kuwa Tanzania inahitaji ushirikiano wa wadau mbalimbali, wasimamizi wa sheria, wazalishaji, na vyombo vya sheria ili kukabili changamoto ya pombe haramu, ambayo inakadiriwa kuwa asilimia 55 ya jumla ya pombe inayozalishwa, kusambazwa na kutumiwa nchini.
"Pombe haramu bado ni suala tete nchini Tanzania. Inaleta hatari kubwa kwa afya ya umma kutokana na uzalishaji wake usiosimamiwa, ukosefu wa udhibiti wa ubora, na mara nyingi huwa na mchanganyiko hatari. Zaidi ya hayo, biashara haramu ya pombe inadhoofisha biashara halali, inanyima Serikali mapato makubwa ya kodi, na inachochea mzunguko wa uchumi usio rasmi ambao ni vigumu kuufuatilia au kuusimamia," alibainisha Hussein Sufian, Mwenyekiti wa Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI).
Jukwaa hilo liliashiria uzinduzi rasmi wa utafiti wa kitaifa kuhusu pombe haramu unaolenga kubainisha ukubwa halisi na sababu za kuenea kwa pombe haramu nchini Tanzania. Aina za pombe zinazowekwa katika kundi la pombe haramu ni pamoja na bandia, pombe za kienyeji zilizotengenezwa nyumbani, pombe za magendo, pamoja na pombe zinazouzwa bila kulipa kodi za Serikali.
Utafiti huo wa pamoja kati ya Serikali na sekta binafsi unatokana na mazungumzo ya awali kati ya pande hizo mbili, ambayo yalitambua umuhimu wa kuwa na ushahidi unaoungwa mkono na takwimu katika kuunda sera, kanuni na sheria za kupambana na pombe haramu nchini.
Akizungumza kwa niaba ya wazalishaji wakuu wa pombe waliohudhuria mkutano huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Serengeti Breweries Limited (SBL), Obinna Anyalebechi, alisema sekta hiyo ilikuwa na shauku ya kutumia matokeo ya utafiti huo kubuni bidhaa maalum zitakazowavutia watumiaji kutoka kundi la pombe haramu kujiunga na pombe halali.
Kwa upande wa Serikali, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, alisema lengo la juhudi hizi za pamoja ni kuhakikisha kuwa sera za kitaifa na hatua za udhibiti za baadaye zinatokana na ushahidi wa kuaminika unaotokana na takwimu, na kwamba watafanya kazi kwa pamoja kutafuta suluhisho endelevu na lenye manufaa kwa Watanzania na kwa sekta rasmi.
"Mkutano huu ni hatua muhimu katika kuratibu juhudi zetu za kupambana na biashara ya pombe haramu, tatizo linalohatarisha afya ya umma, kudhoofisha biashara halali, na kupunguza mapato ya Serikali," alisema Chalamila.
Meneja wa Mradi wa Euromonitor, Benjamin Rideout, akizungumza kwenye mkutano wa wadau uliofanyika 30 Julai 2025 jijini Dar es Salaam, kujadili changamoto ya pombe haramu, inayoaminika kuchangia asilimia 55 ya matumizi ya pombe nchini. Mkutano huo uliandaliwa na CTI na kuhudhuriwa na wadau kutoka sekta binafsi na serikali. Pichani kutoka kushoto ni Prof. Lilian Kahale (UDSM), DC wa Kinondoni Mhe. Saad Mtambule, na Mkurugenzi Mtendaji wa Serengeti Breweries, Dr. Obinna Anyalebechi.

Katika hati ya mashtaka iliyosomwa mahakamani hapo na Wakili wa Serikali, Frank Rimoy, washtakiwa wametajwa kuwa ni PF Inspekta Fredrick Malekela (45), E 4627 Sajenti Kalemwa Kaunga (54), E 7855 Sajenti Edger Mlogo (54), F 1129 Sajenti Robert Titus (47), na F 5092 Sajenti John Kaponswe (46).
Washtakiwa wengine ni Damson Minyilenga (46), Simon Aloyce (60) ambaye ni mfanyabiashara, na Verand Liberio (29).
Katika kesi hiyo, washtakiwa wanakabiliwa na shtaka moja la kuwasilisha nyaraka ya uongo na mashtaka 15 ya kughushi.
Mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Geofrey Mhini, ilidaiwa kuwa mwaka 2024 ndani ya Mkoa wa Dar es Salaam, washtakiwa kwa pamoja walitengeneza nyaraka ya uongo kwa nia ya udanganyifu, ikionyesha kibali cha kumiliki silaha chenye jina la Ahmed Abdallah Ally, huku wakijua kuwa taarifa hizo si za kweli.
Imeelezwa kuwa washtakiwa hao pia waliwasilisha nyaraka ya uongo iliyodai kuwa ni kibali cha kumiliki silaha chenye jina la Ahmed Sandrudin, wakiwa na nia ovu ya kulaghai mamlaka husika.
Katika mashtaka ya kughushi, kwa mujibu wa upande wa mashtaka, inadaiwa kuwa katika kipindi hicho cha mwaka 2024, washtakiwa wote, wakiwa na nia ovu ya kulaghai, walitengeneza vibali vya umiliki wa silaha kwa kutumia majina na namba mbalimbali za watu tofauti tofauti, huku wakijua kuwa nyaraka hizo ni za kughushi.
Hata hivyo, washtakiwa wote wamekana kutenda makosa hayo na wamerudishwa rumande kwa kushindwa kutimiza masharti ya dhamana, ambapo mahakama ilimtaka kila mshtakiwa kuwa na mdhamini mmoja atakayesaini bondi ya Sh. Milioni nne, awe na kitambulisho cha NIDA na barua ya utambulisho kutoka serikali za mitaa.
Kesi hiyo imepangwa kutajwa tena Agosti 12, mwaka huu.
Katika ziara hiyo, wanafunzi wa darasa la sita waliwaonyesha wageni umahiri wao wa kuelewa na kueleza masomo ya sayansi kwa Kiingereza. Mwanafunzi Abiero Odwar aliwaelekeza wenzake kwa ufasaha kuhusu mfumo wa hewa na chakula mwilini, huku Subra Saad Kumbata akieleza kwa umahiri njia za uzalishaji wa umeme kwa kutumia vifaa mbalimbali.
Uwezo huo wa wanafunzi unatokana na uwekezaji wa Serikali kupitia Mradi wa Kuimarisha na Kuboresha Elimu ya Awali na Msingi (BOOST), ambao mwaka 2024 ulitoa zaidi ya shilingi milioni 306 kwa ajili ya uanzishwaji wa shule hiyo.
Kupitia fedha hizo, shule imepata madarasa tisa, matundu 16 ya vyoo, na miundombinu mingine muhimu, hali iliyoongeza hamasa ya walimu kufundisha na wanafunzi kujifunza. Shule hiyo sasa ina wanafunzi 647 — wavulana 313 na wasichana 334 — na imekuwa kivutio cha wanafunzi kutoka shule nyingine kutokana na ufaulu wa juu katika mitihani ya kitaifa.