Na Mwandishi Wetu.

MWALIMU wa Shule Binafsi Irene Muthemba amesema Shule ya Ukonga Skillful imebeba siri kubwa na shuhuda za mafanikio ya vijana wengi hasa waliokuwa wamekata tamaa ya kuendelea na masomo ya sekondari.

Muthemba alitoa kauli hiyo juzi wakati wa mahafali ya 19 ya wanafunzi kidato cha sita wanaohitimu katika shule hiyo,alisema kwa muda mfupi aliokaa katika eneo amebaini mambo makubwa kuhusu shule hiyo kuhusu walimu na wanafunzi.

"Ningeambiwa niandike chochote kuhusu hii shule,ningesema kuwa ina siri kubwa na shuhuda nyingi sihitaji kuambiwa lakini ukiona watu wa hapa inaonyesha kuna shuhuda nyingi na siri kubwa mpaka wahusika wanafika hapa na wengine waliofanikiwa kwakupita hapa,"alisema Muthemba ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mahafali hayo.

Alisema pamoja na wanafunzi kusoma kwa bidii lakini walimu wa shule hiyo wanachukua nafasi kubwa katika kuwasimamia wanafunzi.

"Mimi ni mwaalimu wa miaka mingi uzoefu wangu ni miaka 12 na nusu,hii kazi siiifanyi tu kwa sababu ni mwaalimu,naomba niwakumbushe walimu wenzangu kuwa katika huduma za Mungu ualimu ni huduma ndo maana Mungu anatubariki.

"Walimu wa hii shule nawashukuru sana kitu cha kwanza nilichokiona ni nidhamu za wanafunzi,tangu nimekaa hapa naona watoto wametulia sio kawaida kundi lote hili kusiwe na hata na drama mnafanya kazi kubwa sana,"alisema Muthemba.

Aliwataka wanafunzi kusoma kwa bidii bila kukata tamaa na kwamba wapambane mpaka kieleweke.

Naye muasisi wa Ukonga Skillful Diodorus Tabaro alisema jumla ya wanafunzi 78 ambao wanatarajiwa kuhitimu kidato cha sita wametunukiwa vyeti katika mahafali hayo ambapo kati ya wanafunzi 72 ni kutoka makao makuui na wanafunzi sita wanatoka tawi la shule hiyo lililopo Mbezi Luis.

"Wanafunzi wanaohitimu Leo (juzi) ni wale waliosoma kidato cha tano na sita kwa mwaka mmoja,ni muendelezo wa shule hii katika kutoa wahitimu ambao ni kundi la watu waliokuwa wamekata tamaa yakuendelea na masomo.

"Vijana kama walihitimu kidato cha sita mwaka jana walikuwa 52,ninachokumbuka asilimia 98 ya Vijana nao walijiunga vyuo vikuu na wamepata mkopo.hivyo matokeo tuliyoyapata mwaka jana na mwaka huu tunaomba tuyapate kama hayo,"alisema Tabaro.

Alisema mahafali ya 19 ni ishara yakuelekea miaka 20 ya kuanzishwa kwa shule hiyo ifikapo mwakani.

"Haya ni mhafali ya 19,tulianza safari yetu kwa wanafunzi wenye ndoto ya elimu,miaka 19 yote ilikuwa safari yenye milima na mabonde faraja,ni moja ya safari yakusaidia na kuwainua wanafunzi waliokata tamaa katika elimu,sisi tupo kwa ajili ya kutumika ili wale wanaooonekana hawawezi wapigiwe saluti,"alisema Tabaro.

Alisema katika kipindi chote chakuanzishwa kwa shule hiyo wamekuwa na ufundishaji ambao ni tofauti kna watu wengine na kuwawezesha zaidi ya wanafunzi 700 kujiunga na vyuo katika ngazi shahada.


Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mhe. Shaka Hamdu Shaka, ametoa wito kwa wazazi, walimu, na watendaji wa kata kushirikiana kwa karibu katika kuhakikisha wanafunzi wanapata chakula cha mchana shuleni.

Amesisitiza kuwa lishe bora ni msingi wa maendeleo ya elimu na afya kwa watoto, hivyo ni jukumu la kila mmoja katika jamii kuhakikisha suala hilo linapewa kipaumbele na kwamba hatua hiyo inalenga kuhakikisha kuwa kila shule ina uwezo wa kuzalisha chakula chake, hivyo kuboresha lishe ya wanafunzi na kuongeza ufanisi katika elimu.

Aidha Mhe Shaka amebainisha kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa imejipanga kutumia rasilimali zilizopo, hususani ardhi yenye rutuba, kwa ajili ya kilimo cha chakula cha shule ambapo ametoa rai kwa watendaji wa kata ambao hawana maeneo ya kilimo kutoa taarifa ili wapatiwe ardhi kwa ajili ya shughuli hiyo muhimu.

Kikao hicho kimewashirikisha watendaji wa kata zote arobaini pamoja na wataalamu mbalimbali wa sekta ya lishe na elimu, Mhe Shaka amewataka watendaji hao kuacha kufanya kazi kwa mazoea na badala yake kuweka mkazo katika suala la lishe kwa wanafunzi huku akisisitiza kuwa agizo la kuhakikisha lishe bora kwa wanafunzi ni maelekezo ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, hivyo ni lazima litekelezwe kwa vitendo.

Hata hivyo, Mhe Shaka ameahidi kuwa Wilaya ya Kilosa itaendelea kumuunga mkono Mhe Rais kwa kuhakikisha kuwa suala la lishe kwa wanafunzi linapewa kipaumbele cha juu nakusema kuwa kwa kushirikiana na wazazi, walimu, na watendaji wa kata, watahakikisha kuwa kila mwanafunzi anapata chakula cha mchana shuleni, hivyo kuboresha afya na ufaulu wao.





UMOJA wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) umetoa wito kwa vijana wa Kitanzania kote nchini kujitokeza kwa wingi kushiriki katika mzunguko wa pili wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, unaotarajiwa kuanza Mei 1 hadi Julai 4, 2025.

Katibu wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi Taifa wa UVCCM, Jessica Mshama, ametoa wito huo leo Aprili 29, 2025 jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.

Pamoja na wito huo, Jessica ametoa onyo kali kwa watu wanaotaka kuwahadaa au kuwatumia vijana kwa misingi ya kuvuruga amani wakati wa mchakato huu, ikisisitiza kuwa Tanzania ni nchi ya amani, sheria na utaratibu.

Amesema ushiriki wa vijana katika uchaguzi ni muhimu kwa sababu kundi hilo pia lina asilimia 34.5 ya Watanzania wote kulingana na Sensa ya 2022. “Kila kijana mwenye umri wa miaka 18 au atakayefikisha miaka hiyo ifikapo siku ya uchaguzi mkuu, anatakiwa kuhakikisha amejiandikisha au ameboresha taarifa zake."amesemaa Jessica

Amesema ratiba ya uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura awamu ya pili imegawanywa katika mizunguko mitatu, ambapo mzunguko wa Kwanza kuanzia Mei Mosi hadi Mei 7 katika Mikoa 15 ya Geita, Kagera, Mara, Shinyanga, Mwanza, Simiyu, Rukwa, Tabora, Katavi, Kigoma, Iringa, Ruvuma, Mbeya, Njombe na Songwe.

Mzunguko wa pili utaanza Mei 16 hadi 22, 2025 katika mikoa ya Arusha, Manyara, Kilimanjaro, Tanga, Morogoro, Pwani, Singida, Dodoma, Dar es Salaam, Lindi, Mtwara, Mjini Magharibi, Kaskazini Unguja,

Kusini Unguja, Kaskazini Pemba na Kusini Pemba.
Pia mzunguko wa Tatu, Vituo vya magereza (130 Tanzania Bara) na vyuo vya mafunzo (10 Zanzibar).

utaanza Juni 28 hadi Julai 04, 2025.
Jessica amesema kuwa kwa mujibu wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, jumla ya vituo 7,869 vitatumika katika uboreshaji huo—vikiwemo vituo 7,659 Tanzania Bara na 210 Zanzibar.

Katika hatua nyingine, Jessica ameeleza kuwa serikali chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imefanikiwa kutengeneza zaidi ya ajira milioni nane kupitia sekta za umma na binafsi, sawa na asilimia 115 ya matarajio, kutokana na utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati.

Miradi hiyo ni pamoja na ujenzi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP), Reli ya Kisasa ya SGR, Bwawa la Kufua Umeme la Julius Nyerere, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato, pamoja na ajira katika sekta za elimu na afya.

"Zaidi ya Sh bilioni 250 zimetolewa kwa makundi ya vijana kupitia mikopo ya asilimia 10 ya mapato ya halmashauri kwa ajili ya kuwawezesha kiuchumi," alisema.

Jessica amewahimiza vijana kujiandikisha, kuboresha taarifa zao, kuchangamkia fursa za kugombea uongozi na kushiriki kikamilifu katika uchaguzi ujao.

“Tanzania ya sasa inahitaji viongozi vijana wenye maono, uadilifu na uzalendo wa dhati,” alisisitiza.

Jessica pia alieleza mafanikio mengine ya serikali ikiwemo ongezeko la upatikanaji wa huduma ya maji vijijini kwa asilimia 77 na mijini kwa asilimia 88. Alitaja pia ujenzi wa shule mpya 3,631 za msingi na sekondari, madarasa 21,912, vituo vya afya 367 na zahanati 980.

Kwa mujibu wa Jessica, vifo vya wajawazito vimepungua kutoka 556 hadi 104 kwa kila vizazi hai 100,000 huku matumizi ya nishati safi ya kupikia yakiimarika kwa asilimia 85. Pia, huduma ya bima ya afya imeboreshwa na kuwafanya wananchi kupata matibabu kuanzia zahanati hadi hospitali za rufaa.
Mwenyekiti wa Bodi ya TASAC  Nah.Mussa Mandia akizungumza na wananchi wa Mwalo wa Luhita wakati Bodi hiyo ilipofanya ziara katika Mwalohuo hawapo pichani.

Na Mwandishi Wetu

WANACNHI wa Kijiji cha Luhita, wanaotumia Ziwa la Burigi kwa shughuli za usafiri na uvuvi, wameiomba Mamlaka ya Usimamizi wa Usafiri wa Majini (TASAC) kuchukua hatua za haraka kuondoa magugu maji yanayozidi kuenea katika ziwa hilo na kuathiri shughuli zao za kila siku.

Wito huo umetolewa wakati wa ziara ya Bodi ya TASAC walipotembelea Mwalo wa Luhita kwa lengo la kukagua hali ya usalama wa usafiri wa majini katika Ziwa Burigi. Wananchi wameeleza kuwa magugu hayo yamesababisha njia wanazotumia kusafiri na kuvua samaki kuwa nyembamba, kiasi kwamba vyombo vya usafiri majini viwili haviwezi kupishana.

Mwenyekiti wa Usimamizi wa Mazingira ya Fukwe (BMU), Nelson Atanas, amesema kuwa hali hiyo imekuwa kikwazo kikubwa kwao, hasa katika kipindi cha mvua ambapo magugu huzidi kuenea. Ameeleza kuwa ujio wa Bodi ya TASAC unatoa matumaini ya kupata msaada wa kuondoa magugu hayo na kuboresha mwalo huo kwa shughuli za kijamii na kiuchumi.

Naye Leopord Baltazal, mmoja wa wananchi wa kijiji hicho, amesema ongezeko la magugu hayo linaweza kuathiri kabisa shughuli za uvuvi na kusababisha maisha kuwa magumu zaidi kwa wananchi wanaotegemea ziwa hilo kwa kipato chao.

Akijibu hoja hizo, Mwenyekiti wa Bodi ya TASAC, Nahodha Mussa Mandia, amesema mamlaka hiyo imepokea changamoto hizo na itaendelea kushirikiana na wananchi kuhakikisha shughuli zao zinaendelea kwa ufanisi. Amesisitiza kuwa mojawapo ya hatua zitakazochukuliwa ni ujenzi wa gati na miundombinu ya msingi katika mwalo huo.

Nahodha Mandia pia alimwagiza Mtendaji wa kijiji hicho kuwasilisha maandishi rasmi ya mahitaji yao kwa Afisa Mfawidhi wa TASAC Mkoa wa Kagera, ili hatua za utekelezaji zianze kuchukuliwa. Alisisitiza umuhimu wa kuwa na vifaa vya uokozi wakati wote, kwa mujibu wa sheria za usalama wa majini.

Aidha, ameeleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, inaendelea kutatua changamoto mbalimbali za wananchi, ikiwemo kuboresha bandari, mialo ya uvuvi na huduma za usafiri wa majini.

Mkazi wa Luhita Leopord Baltazar akitoa maelezo  kwa Bodi ya TASAC Kuhusiana changamoto ya miundombinu katika mwalo wa Luhita katika ziwa Burigi.
Mwenyekiti wa Usimamizi wa Mazingira ya Fukwe Mwalo wa Luhita Nelson Atanas akizungumza kuhusiana changamoto ya magugu katika mwalo Luhita katika Ziwa Burigi.
Wafanyakazi wa TASAC na Meneja wa Forodha Mkoa wa Kagera mwenye miwani.
Matukio  katika picha ya Bodi ya TASAC  na viongozi wa Kijiji cha Luhita.

 

Afisa Habari Mkuu,kutoka Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Bi. Joyce Mgaya,akizungumza na watoto Yatima na wenye Ulemavu 100 kutoka Kituo cha Kulelea Yatima cha Tulee Yatima Tanzania (TUYATA) kutoka Dar es Salaam mara baada ya kuwasili jijini Dodoma kwa ajili ya ziara ya mafunzo pamoja na kutembelea Mji wa Serikali Mtumba ziara ya mafunzo iliyodhaminiwa na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA).
.....
WATOTO Yatima na wenye Ulemavu 100 kutoka Kituo cha Kulelea Yatima cha Tulee Yatima Tanzania (TUYATA) kutoka Dar es Salaam wametembelea Mji wa Serikali Mtumba Dodoam huku wakiushukuru Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni ( BRELA) kwa kudhamini ziara ya mafunzo kwa kutumia reli ya kisasa (SGR).

Akizungumza leo Aprili 29,2025 kwa niaba ya BRELA, Afisa Habari Mkuu, BRELA Bi. Joyce Mgaya amesema ziara hiyo in kuonesha dhamira ya BRELA katika kusaidia makundi yenye uhitaji maalum.

“Mtendaji Mkuu wetu aliona ni jambo jema kuwapa watoto hawa fursa ya kutembelea makao makuu ya nchi na kujionea miradi ya maendeleo inayotekelezwa,” amesema Bi Mgaya.

Hata hivyo ameongeza kuwa kwa wengi wao,ni mara ya kwanza kupanda treni ya SGR na kufika Dodoma, na kwamba ziara hiyo ni sehemu ya mikakati ya BRELA kusaidia jamii kupitia programu mbalimbali za kuwafikia wananchi.

Aidha Bi.Mgaya ametoa wito kwa Taasisi zingine ziendelee kuwakimbilia watu wenye mahitaji Kwa kuhakikisha wanawasaidia mahitaji mbalimbali.
Kwa upande wake Mkurugenzi na Mwanzilishi wa kituo cha TUYATA, Bi Fauzia Jabir amesema kuwa wanaishukuru BRELA kwa safari hiyo kwani watoto wengi wamefurahi na katika maisha yao hawajawahi kupanda treni.

“Watoto wamefurahi mno, jambo hili halijawahi kutokea. BRELA imefanya jambo kubwa kwa kusimama na watoto hawa wahitaji. Wamehamasika kusoma zaidi baada ya kuona uzuri na fursa zilizopo nchini,” amesema Bi Jabir.

Hata hivyo, ameeleza kuwa licha ya mafanikio ya kielimu waliyonayo, kituo hicho kinakabiliwa na changamoto kubwa ya makazi kwa watoto yatima, na hivyo kuomba msaada wa ujenzi wa nyumba za makazi kwa watoto na wajane.

Mmoja wa walionufaika na kituo hicho, Bi Ayman Jaffar Abubakar ambaye pia ni msemaji wa TUYATA, amesema kulea watoto kutoka mazingira mbalimbali si kazi rahisi lakini kwa neema ya Mungu, wanajitahidi kutoa malezi bora na kuwaelekeza katika njia sahihi.

“Watoto wengi wanaishi kwa walezi, hivyo ni changamoto kuwafuatilia kikamilifu. Tunaishukuru BRELA kwa kutuunga mkono na tunaomba waendelee kuwa nasi hadi tufikie malengo yetu,” amesema
WATOTO Yatima na wenye Ulemavu 100 kutoka Kituo cha Kulelea Yatima cha Tulee Yatima Tanzania (TUYATA) kutoka Dar es Salaam wakiwa ndani ya reli ya kisasa (SGR) kuja jijini Dodoma kutembelea Mji wa Serikali Mtumba ziara ya mafunzo iliyodhaminiwa na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA).
WATOTO Yatima na wenye Ulemavu 100 kutoka Kituo cha Kulelea Yatima cha Tulee Yatima Tanzania (TUYATA) kutoka Dar es Salaam wakishuka ndani ya reli ya kisasa (SGR) mara baada ya kuwasili jijini Dodoma kutembelea Mji wa Serikali Mtumba ziara ya mafunzo iliyodhaminiwa na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA).
Afisa Habari Mkuu,kutoka Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Bi. Joyce Mgaya,akizungumza na watoto Yatima na wenye Ulemavu 100 kutoka Kituo cha Kulelea Yatima cha Tulee Yatima Tanzania (TUYATA) kutoka Dar es Salaam mara baada ya kuwasili jijini Dodoma kwa ajili ya ziara ya mafunzo pamoja na kutembelea Mji wa Serikali Mtumba ziara ya mafunzo iliyodhaminiwa na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA).
Watoto Yatima na wenye Ulemavu 100 kutoka Kituo cha Kulelea Yatima cha Tulee Yatima Tanzania (TUYATA) kutoka Dar es Salaam wakifurahia Mji wa Serikali Mtumba baada ya kutembelea ziara ya mafunzo iliyodhaminiwa na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA).
Afisa Habari Mkuu,kutoka Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Bi. Joyce Mgaya,akizungumza na waandishi ya habari jijini Dodoma mara baada ya kudhamini ziara ya mafunzo ya Watoto Yatima na wenye Ulemavu 100 kutoka Kituo cha Kulelea Yatima cha Tulee Yatima Tanzania (TUYATA) kutoka Dar es Salaam mara baada ya kutembelea Mji wa Serikali Mtumba ziara iliyodhaminiwa na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA).
Mkurugenzi na Mwanzilishi wa kituo cha TUYATA, Bi Fauzia Jabir,akiishukuru BRELA kwa safari hiyo kwani watoto wengi wamefurahi na katika maisha yao hawajawahi kupanda treni.
Mmoja wa walionufaika na kituo cha TUYATA na msemaji wa TUYATA Bi Ayman Jaffar Abubakar,akielezea historia yake kwa waandishi wa habari.

 


Wasanii wa filamu na maigizo nchini wametakiwa kutumia Lugha ya kiswahili kama fursa ya kibiashara kimataifa ili kuongeza tija itokanayo na filamu hizo katika kujiongezea kipato chao


Rai hiyo imetolewa na Dkt Godwin Maimu ambaye ni Mkurugenzi mtendaji wa tamasha la kimataifa la filamu za kiswahili (ISFF) wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini dar es salaam ambapo amesema lengo la kuanzisha tamasha hilo ni kubidhaisha lugha ya kiswahili kimataifa kupitia filamu za kiswahili zitakazoonyeshwa katika mataifa mbalimbali.


Kwa upande wake mchunguzi lugha mkuu kutoka baraza la kiswahili Tanzania (BAKITA) amewasisi wasanii nchini Kutumia lugha ya kiswahili kwa ufasaha ili kulinda hadhi ya lugha hiyo huku wakiendelea kuutangaza utamaduni wa kitanzania kimataifa 


Naye Dusabimana Apollos msanii kutoka nchini Rwanda amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kwa wasanii wa afrika mashariki katika kukuza matumizi ya lugha ya kiswahili hususan katika masoko ya kimataifa








 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Ridhwan Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa ORICA  baada ya kutembelea banda lao katika maadhimisho  ya Wiki ya  Usalama na Afya  Mahala Pa Kazi yanayendelea kufanyika mkoani Singida.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Ridhwan Kikwetev akitembela banda la Orica Tanzania na kujifunza kuhusu shughuli zao za ulipuaji migodi wakati akifanya ukaguzi katika maadhimisho ya Wiki ya kimataifa ya Usalama mahali pa kazi inayofanyika kitaifa mkoani Singida


WAKATI  Dunia ikiadhimisha Siku ya Usalama Kazini Aprili 28, 2025 chini ya kaulimbiu ‘Nafasi ya Akili Mnemba na Teknolojia za Kidijitali katika Kuimarisha Usalama na Afya Mahala Pa Kazi, Orica Tanzania inayojishughulisha na utengenezaji Pamoja na uuzaji wa baruti kwa ajili ya ulipuaji migodini imetoa wito wa kuhakikisha usalama unazingatiwa wakati wa kazi ili kuepusha madhara yatokanayo na ajali za baruti.

Akizungumza katika Maonesho ya Wiki ya Usalama na Afya Mahali Pa Kazi Duniani yanayoendelea Kitaifa mkoani Singida, Mhandisi wa Baruti kutoka Orica Bw. Boaz Samwel amesema kuwa baruti ni kihatarishi kikubwa migodini na huweza kuleta madhara makubwa endapo hakitatumiwa kwa kuzingatia kanuni za matumizi sahihi.

“Kupitia maonesho haya, tumekuja na teknolojia ya kisasa inayotumia Akili Mnemba kwa ajili ya ulipuaji bila madhara yoyote na kupitia teknolojia hii, kazi ya ulipuaji inaweza kufanyika kwa ufanisi na usalama zaidi pasipo kuwepo mtu yeyote ndani ya eneo la karibu na mlipuko.” amesema Bw.Samwel.

“Tofauti na miaka ya nyuma, Teknolojia imebadili kwa kiasi kikubwa sana mfumo mzima wa ulipuaji na kuifanya kazi hii kuwa rahisi na salama zaidi, kipaumbele kikubwa kikiwa ni kulinda uhai wa watu, mazingira na ufanisi katika uzalishaji.

Amesema ili kupunguza na kuondoa madhara yanayoweza kutokea maeneo ya migodini, licha ya Orica kuwa watengenezaji na wauzaji wa baruti , wao pia wamekuwa wakitoa ushauri kwa matumizi sahihi ya teknolojia salama katika kazi hiyo kwa kuzingatia sheria na taratibu zote za Wakala wa Usalama na Afya Mahala Pa Kazi (OSHA).

Bw.Boaz amezitaja baadhi ya teknolojia zinazotumia akili Mnemba kuwa ni pamoja Blast IQ, ORBS, 4D, RHINO, OREpro 3D, ENVIROTrack, FRAGTrack na GroundProbe inayoweza kuhisi na kutambua mabadiliko yoyote katika mwamba na kutoa taarifa wakati huo huo na kuzuia ajali inayoweza kusababishwa na kuanguka kwa mwamba.

Amesema uwekezaji huu ni maendeleo makubwa katika sekta ya madini ikiendelea kubadilika kwa njia ya kidijitali na uvumbuzi.

Akitoa mtazamo mpana kuhusu dhamira ya Orica Tanzania, Daniel Paul, Mtaalamu wa Rasilimali Watu kwa Kanda ya Kusini mwa Afrika ya Orica — akizungumza kwa niaba ya Mhandisi Asha Mambo, Meneja wa Eneo la Orica Tanzania — alisema:

"Katika Orica Tanzania, tunaamini kuwa usalama, afya, na ustawi wa wafanyakazi ni nguzo kuu za mafanikio ya biashara yetu. Kama sehemu ya Orica Limited, kampuni inayoongoza duniani katika vilipuzi vya kibiashara, mifumo ya ulipuaji na huduma za madini inayofanya kazi katika zaidi ya nchi 100, tumejikita katika kuweka viwango vya juu zaidi vya usalama — katika shughuli zetu pamoja na katika sera na taratibu.

Alisisitiza zaidi kuwa usalama si jukumu la wachache, bali ni wajibu wa pamoja kwa wadau wote — imani ambayo inaendelea kuimarisha mafanikio na uimara wa Orica Tanzania.

Orica inafanya kazi katika zaidi ya nchi 100, ikiwa na zaidi ya miaka 150 ya uzoefu. Mashirika na makampuni mbalimbali yameshiriki katika maonesho hayo yaliyodumu kwa wiki nzima.

Akiongea wakati wa ufungaji, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Ridhiwani Kikwete amewataka washiriki kuimarisha juhudi za usalama wa wafanyakazi na kuwa kipaumbele katika shughuli zao.

Na Diana Byera – Missenyi

Kampeini ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia wilayani Missenyi Mkoani Kagera, imefanikiwa kwa asilimia 95.3 ndani ya siku 15 tangu ilipozinduliwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro, Aprili 14 mwaka huu katika viwanja vya Mayunga, Manispaa ya Bukoba.

Mratibu wa kampeini hiyo wilayani Missenyi Maxmillan Fransis, alisema kuwa ndani ya siku hizo 15, kuanzia Aprili 15 hadi Aprili 28, kata zote 15 zilizopangwa kufikiwa zimefikiwa, na vijiji 43 vilivyopangwa kufikiwa, 41 vilifikwa.

"Kampeini imekuwa na mafanikio makubwa na mwitikio mkubwa sana. Mwanzoni ilipangwa iwe ya siku 10, lakini serikali iliongeza siku 5 kulingana na uhitaji wa wananchi, Tumefikia vijiji 41, na vijiji viwili ambavyo kampeini haikufanikiwa, tulifika lakini viongozi walisema wana misiba mikubwa. Vingine vyote vimenufaika na kampeini hiyo," alisema.

Aliongeza kuwa kupitia kampeni hiyo, makundi mbalimbali yalipata elimu, yakiwemo ya bodaboda, wanafunzi, wakulima, wazee, watu wenye ulemavu, taasisi binafsi, waajiriwa serikalini, huku elimu kuhusu umiliki wa ardhi, matumizi sahihi ya ardhi, wosia, mirathi, ukatili na matunzo ya watoto ikitolewa katika mikutano ya hadhara ili kunufaisha umma na kuwafundisha kufuata sheria.

Alisema kuwa migogoro iliyojitokeza kwa wingi ni ya ardhi, mirathi na ukatili, ambapo mingi imetatuliwa kwa njia ya usuluhishi. Migogoro ambayo haijatatuliwa imekabidhiwa kwa vitengo husika ili kupata utatuzi wa kudumu.

Aidha, migogoro ya kisheria kwa wananchi ambao hawana mawakili, tayari mashauri yao yamekabidhiwa kwa mawakili ili kuwasaidia kuendelea na hatua za mahakama.

Akitaja mafanikio yaliyopatikana, alisema kuwa elimu ya masuala ya kisheria imetolewa na kufikia wananchi 14,020, ambapo wanaume ni 6,905 na wanawake ni 7,115.

Aidha, watendaji wa vijiji, kata, wenyeviti wa vijiji na vitongoji pamoja na madiwani wamejengewa uwezo juu ya masuala ya kisheria kutokana na kushughulikia kero za wananchi kila siku, ambazo zinahitaji utaalamu wa masuala ya kisheria.

Changamoto zilizojitokeza ni pamoja na uwepo wa malalamiko ya muda mrefu kuhusu matumizi ya ardhi baina ya wananchi na serikali za vijiji, jambo ambalo limechochea uvunjifu wa amani na baadhi ya wananchi kugoma kuchangia maendeleo ya vijiji kwa sababu ya migogoro ya ardhi.








Na Mwandishi Wetu – Singida

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Ridhiwani Kikwete, amesisitiza umuhimu wa wananchi kujiunga na kuchangia Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) ili kunufaika na mafao mbalimbali yakiwemo Mafao ya Matibabu kwa Wananchi waliojiajiri. Kwa upande wa wafanyakazi wa NSSF, Mhe.Waziri amewataka kuendelea kuhudumia wanachama kwa weledi.

Mhe. Ridhiwani amesisitiza hayo alipotembelea banda la NSSF kwenye Maonesho ya Wiki ya Usalama na Afya Mahala pa Kazi Duniani, yanayofanyika Kitaifa katika viwanja vya Mandewe, mkoani Singida.

Amesema NSSF ina jukumu kubwa la kutoa huduma za hifadhi ya jamii kwa wanachama wa sekta binafsi na kuwafikia wananchi waliojiajiri kupitia Mfumo wake wa Hifadhi Skimu, ili kuhakikisha hata wale waliojiajiri wenyewe wanapata mafao ya muda mfupi na mrefu.

“NSSF ina wajibu mkubwa wa kuimarisha maisha ya wanachama wake, hasa pale wanapokumbwa na majanga yanayoathiri kipato chao. Hivyo amesisitiza kuendelea kutoa elimu ya mafao na huduma zinazotolewa na Mfuko huo kwa wananchi.

Aidha, Mhe. Ridhiwani alionesha kuridhishwa na jinsi NSSF ilivyotekeleza dhana ya usalama na afya mahala pa kazi.

Kwa upande wake, Meneja wa NSSF Mkoa wa Singida, Bw. Oscar Kalimilwa, amesema NSSF imeshiriki maonesho hayo kwa lengo la kutoa elimu kuhusu hifadhi ya jamii, kusajili wanachama wapya kutoka sekta binafsi pamoja na wale waliojiajiri wenyewe.

Bw. Kalimilwa alisisitiza kuwa maonesho hayo yamewapa nafasi ya kuwakumbusha waajiri wa sekta binafsi juu ya wajibu wao wa kuwasajili na kuwasilisha michango ya wafanyakazi wao kwa wakati.

“Ninatoa rai kwa waajiri kuhakikisha michango ya wafanyakazi wao inawasilishwa NSSF kwa wakati kwani hilo ni takwa la kisheria. Kufanya hivyo kutawahakikishia wanachama kulipwa mafao yao kwa wakati na kuondoa usumbufu usio wa lazima," alisema.

Vilevile, aliwahamasisha wananchi waliojiajiri, wakiwemo bodaboda, mama lishe, wavuvi, wakulima, wachimbaji wadogo, wasusi, vinyozi, wasanii na wajasiriamali wengine, kujiunga na kuchangia katika NSSF kupitia Hifadhi Skimu.

Alibainisha kuwa mwanachama aliyejiajiri anapaswa kuchangia si chini ya shilingi 30,000/- kwa mwezi ili kupata mafao mbalimbali yakiwemo ya matibabu, na shilingi 52,200/- mwanachama atapata Mafao ya matibabu yeye na familia yake wakiwemo watoto wanne. Ameongeza kuwa michango hiyo inaweza kufanyika kidijitali kupitia simu za kiganjani ili kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa uharaka.









Mwemyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza na watendaji wa uboreshaji ngazi ya Kata na Waandishi Wasaidizi na Waendesha vifaa vya Biometriki kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Iringa mkoani Iringa leo Aprili 29,2025 wakati alipotembelea mafunzo hayo ikiwa ni maandalizi ya awamu ya pili mzunguko wa kwanza wa uboreshaji Daftari la Kudumu la Wapiga Kura unaoanza Mei Mosi hadi Mei 07, 2025 katika mikoa 15.
Sehemu ya Washiriki wa Mafunzo hayo wakimsikiliza Mwenyekiti wa Tume.

Sehemu ya Washiriki wa Mafunzo hayo wakimsikiliza Mwenyekiti wa Tume.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akikagua mafunzo ya watendaji wa Uboreshaji ngazi ya Kata kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Iringa leo Aprili 29,2025 ikiwa ni maandalizi kuelekea awamu ya pili ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na uwekaji wazi wa Daftari la awali la wapiga Kura. 


Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akikagua mafunzo ya watendaji wa Uboreshaji ngazi ya Kata kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Iringa leo Aprili 29,2025 ikiwa ni maandalizi kuelekea awamu ya pili ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na uwekaji wazi wa Daftari la awali la wapiga Kura. 
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Daftari na TEHAMA wa Tume.
*******
Na. Mwandishi wetu, Iringa
TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi imewataka watendaji wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kufanya kazi kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na taratibu za Uchaguzi wakati wa utekelezaji wa awamu ya pili ya zoezi hilo litakalofanyika sambamba na uwekaji wazi wa Daftari la Awali la Wapiga Kura ambapo mzunguko wa kwanza utahusisha mikoa 15 kuanzia mei mosi hadi saba mwaka huu.
 
Hayo yamesemwa leo Aprili 29,2025 na Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele wakati akizungumza na washiriki wa mafunzo ya siku moja ya watendaji hao ngazi ya Kata kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Iringa mkoani Iringa.
“Nawakumbusha tena kama nilivyowakumbusha katika zoezi lililopita, kwamba katika utekelezaji wa zoezi hili mzingatie sheria, kanuni na taratibu za uchaguzi, muwe wanyenyekevu kwa wateja mtakao kuwa mnawahudumia,”alisema Jaji Mwambegele.
 
Jaji Mwambegele amewaeleza watendaji hao kuwa wateja wengi watakaowahudumia ni wananchi wa kawaida hivyo hawana budi kuwahudumia vyema kwa lugha nzuri naikitokea kuna ulazima wa kuwarekebisha pale wanapokosea basi wafanye hivyo kwa staha.
 
“Zoezi hilo linafanyika kwa mujibu wa masharti ya kifungu cha 16(5) cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Na. 1 ya mwaka 2024 kinachoipa Tume jukumu la kuboresha Daftari la Kudumu la Wapiga Kura mara mbili mara baada ya uchaguzi mkuu na kabla ya uteuzi wa wagombea kwa uchaguzi mkuu unaofuata,” alisema.
 
Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya pili utafanyika sambamba na uwekaji wazi wa Daftari la Awali la Wapiga Kura kuanzia tarehe 01 Mei, 2025 na kukamilika tarehe 04 Julai, 2025.
 
Uboreshaji wa Daftari unataraji kufanyika kwa mizunguko mitatu ambapo mzunguko wa kwanza utajumuisha mikoa 15, mzunguko wa pili mikao 16 na mzunguko wa tatu utajumuisha vituo vya magereza na vyuo vya mafunzo.
 
Mikoa itakayohusika kwenye mzunguko wa kwanza wa uboreshaji ni pamoja na Iringa, Geita, Kagera, Mara, Shinyanga, Mwanza, Simiyu, Rukwa, Tabora, Katavi, Kigoma, Ruvuma, Mbeya, Njombe na Songwe ambapo zoezi hilo litafanyika kuanzia Mei 1 hadi 7 mwaka huu.
 
Aidha, mzunguko wa pili utahusisha mikoa ya Arusha, Manyara, Kilimanjaro, Tanga, Morogoro, Pwani, Singida, Dodoma, Dar es Salaam, Lindi, Mtwara, Mjini Magharibi, Kaskazini Unguja, Kusini Unguja, Kaskazini Pemba na Kusini Pemba ambapo zoezi hilo litafanyika kuanzia Mei 16 hadi 22, 2025.
 
Mzunguko wa tatu wa zoezi la uboreshaji wa Daftari utahusisha vituo 130 vilivyopo kwenye magereza ya Tanzania Bara na vituo 10 vilivyopo katika Vyuo vya Mafunzo Tanzania Zanzibar kwa wakati mmoja na utafanyika kwa muda wa siku saba kuanzia Juni 28 hadi Julai 04, 2025.
 
Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa awamu ya pili, utafanyika ngazi ya kata kwa Tanzania Bara na ngazi ya jimbo kwa Tanzania Zanzibar, ambapo jumla ya vituo 7,869 vitahusika, vituo 7,659 vipo Tanzania Bara na vituo 210 vipo Tanzania Zanzibar.
 
Katika awamu ya pili ya uboreshaji, wapiga kura wapya 1,396,609 wataandikishwa, wapiga kura 1,092,383 wataboresha taarifa zao na wapiga kura 148,624 watafutwa kwenye Daftari kwa kukosa sifa za kuendelea kuwepo kwenye Daftari,” amesema Jaji Mwambegele.
 
Mambo mengine ni kuhamisha taarifa za wapiga kura waliohama kutoka kata au jimbo walipoandikishwa awali na kuondoa  taarifa za wapiga kura waliopoteza sifa za kuwemo kwenye Daftari kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kifo.
 
Aidha, kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 11(1) na (2) cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Na. 1 ya Mwaka 2024, Tume pia ina jukumu la kuandaa Daftari la Awali la Wapiga Kura na kuliweka wazi kwa umma.
 
Lengo la uwekaji wazi wa Daftari hilo ni kutoa fursa kwa wananchi kukagua, kufanya marekebisho ya taarifa za wapiga kura na uwekaji wa pingamizi dhidi ya wapiga kura waliomo kwenye daftari ambao hawana sifa na litabandikwa katika vituo vyote vilivyotumika wakati wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya kwanza.
 
Tume iliboresha Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya kwanza kuanzia tarehe 20 Julai, 2024 na kukamilisha tarehe 25 Machi, 2025.


Top News