Na Mwandishi Wetu

Mkutano wa hivi karibuni wa AviaDev Africa 2025, umekuwa wenye mafanikio makubwa katika sekta ya usafiri wa anga.

Mkutano huo uliosimamiwa na Kampuni ya Showtime ya Zanzibar, ulileta pamoja zaidi ya washiriki 500, ikiwa ni pamoja na wawakilishi kutoka kampuni 36 za ndege na mamlaka za utalii kutoka nchi 46, wote wakitafuta kujenga ushirikiano na kuboresha mawasiliano ya tasnia ya usafiri wa ndege katika bara la Afrika.

Maono ya Ukuaji

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Showtime, Ibrahim Mitawi alionesha furaha yake kuhusu mafanikio ya mkutano huu: "AviaDev Africa 2025 haijatoa tu jukwaa kwa ajili ya kampuni za ndege na viwanja vya ndege kuungana, bali pia imeimarisha jukumu muhimu la utalii katika mchakato wa maendeleo ya njia. Mafanikio yetu yanategemea roho ya ushirikiano iliyojengeka katika siku hizi mbili.

" Mkutano huu ulijumuisha mfumo wa mikutano uliopangwa kitaaluma ambapo uliwezesha makutano zaidi ya 1,200, ikiruhusu washiriki kukutana moja kwa moja na washirika katika jamii ya usafiri wa anga barani Afrika.”

Kauli za Viongozi

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi , alisisitiza umuhimu wa tukio hili: "Zanzibar ina malengo makubwa ya maendeleo na uwekezaji.

“Kupitia AviaDev 2025, tunaweza kuboresha uhusiano wa ndege, kufungua fursa mpya za ukuaji, na kuimarisha ushirikiano duniani kote. Serikali ya Zanzibar, kupitia Tume ya Utalii ya Zanzibar na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege vya Zanzibar, inatarajia kuandaa jukwaa hili kwa wajumbe kutoka maeneo mbalimbali kuja pamoja na kushiriki uzoefu."

Kauli hiyo pia ilizungumzwa na ilirudiwa na maafisa wengine muhimu, wakisisitiza umuhimu wa kuunganisha utalii na mikakati ya usafiri wa anga.

Juhudi za ushirikiano zilizoneshwa katika AviaDev ni muhimu kwa kuhakikisha huduma za ndege endelevu na ukuaji wa kiuchumi katika eneo hilo.

Umuhimu wa Ushirikiano wa Utalii Ujumbe muhimu kutoka mkutano huu ilikuwa jukumu kubwa la utalii katika mchakato wa maendeleo ya njia za usafiri angani.

Nchi ambazo hazijajumuisha mikakati yao ya usafiri wa anga na utalii zinakabiliwa na hatari ya kupoteza safari muhimu za ndege.

Ato Girma Wake, mtaalamu wa sekta, alisema: "Ulikuwa mkutano mzuri na wenye tija. Katika siku mbili, tulipata kile ambacho kwa kawaida hatupati katika wiki moja.

" Hii inasisitiza ufanisi wa fursa za kuungana zilizoletwa na AviaDev, ikirejesha haja ya kuendelea kuunganisha mamlaka za utalii na wadau wa usafiri wa anga.

AviaDev Afrika 2025 imeweka viwango vipya vya ushirikiano katika sekta ya usafiri wa anga. Kwa kuzingatia kujenga uhusiano na kukuza biashara, mkutano huu haujafaidisha washiriki tu bali pia umeifanya Zanzibar kama mchezaji muhimu katika mandhari ya usafiri wa anga duniani.

Tutakapoipima mikutano ya baadaye, ujuzi na uhusiano yaliyoundwa wakati wa AviaDev bila shaka yatatoa vipimo vya kuboresha huduma za ndege na maendeleo ya utalii barani Afrika.




 Na Karama Kenyunko Michuzi Tv 

SERIKALI  imetangaza mpango wa kuimarisha mchango wake katika juhudi za kulinda amani duniani kwa kukiboresha Kituo cha Mafunzo ya Ulinzi wa Amani cha Tanzania (TPTC) ili kiweze kutoa mafunzo kwa ngazi ya kitaifa, kikanda na kimataifa.

Mkuu wa Jeshi la Anga Meja Jenerali Shabani Mani amesema hayo Juni 13, 2025 jijini Dar es.salaam alipokuwa akifunga  mafunzo ya kwanza ya Kiraia kuhusu Ulinzi wa Amani yaliyofanyika katika kituo hicho.

Meja Jenerali Mani alimwakilisha Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Jacob Mkunda, ambaye hakuweza kuhudhuria kutokana na majukumu mengine ya kikazi.

Amesema kuwa maboresho hayo yataifanya TPTC kuwa kitovu muhimu cha mafunzo ya vipengele vyote vitatu vya operesheni za ulinzi wa amani za Umoja wa Mataifa: jeshi, polisi na raia.

Amesisitiza kuwa kituo hicho kitakapoboreshwa kitaweza kuandaa vikosi kamili vya ulinzi wa amani vilivyofunzwa kwa kiwango cha juu na tayari kwa misheni mbalimbali duniani.

Aidha, ameeleza kuwa kituo hicho kinatarajia kuanzisha kozi mpya zinazolenga kuwajengea uwezo Watanzania, wakiwemo raia, ili waweze kushiriki ipasavyo katika juhudi za kulinda amani duniani.

“Mafunzo haya ya mwanzo ni hatua muhimu katika safari ya Tanzania kwenye ulinzi wa amani. Yanalenga kuhakikisha kuwa kila anayeshiriki katika misheni anakidhi viwango vya kimataifa,” amesema.

Ameongeza kuwa huo ni mwanzo tu wa mpango mpana zaidi, na kwamba mafunzo mengine yatafuata hivi karibuni.

Kwa upande wake, Kamanda wa TPTC, Brigedia Jenerali George Itang’are, amesema kuwa mafunzo hayo yamefanyika kwa ushirikiano na Serikali ya Japan kupitia Shirika la Mpango wa Maendeleo la  Umoja wa Mataifa (UNDP).

“Tunafurahi kuona raia wakionyesha hamasa ya kujifunza jinsi vipengele mbalimbali vya ulinzi wa amani vinavyofanya kazi. Aidha, mafunzo haya pia yalihusisha askari polisi waliovaa sare,” ameeleza.

Nomura Hiroyuki, mwakilishi wa Balozi wa Japan nchini Tanzania, alieleza kuwa Japan inajivunia kusaidia mpango huo kama sehemu ya kujitolea kwake katika kuendeleza amani duniani na kuinua jamii.

“Tunaamini kuwa kwa ushirikiano na dhamira ya pamoja, hata mataifa ya mbali kama Japan yanaweza kuwa na mchango chanya katika maeneo ya ndani kama haya,” amesema.

“Kwa kushirikiana kwa karibu na Umoja wa Mataifa pamoja na wadau mbalimbali, tumeweka juhudi mahususi kuunga mkono na kuendeleza jitihada zenye mafanikio,” ameongeza.

Naye, Naibu Mwakilishi Mkazi wa UNDP John Rutele amesema kuwa programu hizo za mafunzo zitasaidia kuongeza mchango wa Tanzania katika operesheni za kimataifa za ulinzi wa amani na kuiimarisha nafasi yake kimataifa.

Amesema  kuwa Tanzania inaendelea kufanya maendeleo makubwa, na kwamba UNDP inaiona nchi hiyo kama kinara anayeibuka katika ulinzi wa amani ndani ya ukanda wa Afrika Mashariki na Kusini.

Rutele amesisitiza pia umuhimu wa kuendeleza ushirikiano na washirika ya maendeleo ili kuendeleza na kupanua programu za mafunzo, ikiwa ni pamoja na kuwakaribisha washiriki kutoka nchi jirani.

“UNDP imejidhatiti kuisaidia Serikali ya Tanzania katika kuimarisha amani endelevu na maendeleo, kuhakikisha kuwa Watanzania wanakuwa na uwezo wa kuchangia kikamilifu katika utulivu wa kikanda na kimataifa,” amesema kwa msisitizo.

Nice Munis, Afisa wa Masuala ya Nje kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amesema “Majukumu yetu yanahusisha utekelezaji wa sera ya mambo ya nje, ikiwa ni pamoja na kuimarisha amani na usalama – jambo ambalo linagusa maslahi ya kila taifa duniani.”

“Mafunzo haya yamenipa uelewa mpana na kunitia nguvu. Nimegundua kwamba hata sisi raia, licha ya kutokuwa sehemu ya vyombo vya ulinzi na usalama, tunaweza kushiriki kikamilifu katika shughuli za ulinzi wa amani, hasa tunapotumwa kwenye misheni za kimataifa.”

“Tumezaliwa na kulelewa hapa Tanzania, hatujawahi kupitia vita kwa moja kwa moja, lakini tunasikia kutoka kwa waliopitia hali hizo.”

Ameongeza kuwa Tanzania imekuwa mstari wa mbele kwa muda mrefu katika kusaidia nchi zilizoathiriwa na migogoro, kwa lengo la kurejesha na kudumisha amani.

Mkuu wa Chuo Cha Mafunzo Ya Ulinzi wa Amani Tanzania, Brigedia Jenerali George Itang'are akizungumza wakati wa hafla  ufungaji wa mafunzo ya kwanza ya Kiraia ya Ulinzi wa Amani nchini

  Mafunzo hayo yalianza Juni 9 2025  na kumalizika Juni 13, 2025.


Mkuu wa Chuo Cha Mafunzo Ya Ulinzi wa Amani Tanzania, Brigedia Jenerali George Itang'are akimkabidhi tuzo mwakilishi wa Balozi wa Japan nchi Nomura Hiroyuki kama ishara ya ushirikiano wa mafunzo ya ulinzi wa Amani wakati wa ufungaji wa mafunzo ya kwanza ya Kiraia ya Ulinzi wa Amani nchini, anayeshuhudia katikati ni Mkuu wa Kamandi ya Anga Meja Jenerali Shabani Mani. Mafunzo hayo yaliyoanza Juni 9 2025  na kumalizika Juni 13, 2025.




Na John Mapepele

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa amewataka Wakuu wa Mikoa na Wilaya nchini kuwaongeza wananchi katika maeneo yao kufanya "jogging" na mazoezi ili kuimarisha afya.

Mhe. Mchengerwa ametoa maelekezo hayo leo Juni 14, 2025 mara baada ya kuongoza na kuhitimisha mbio za pole pole (jogging) za kilomita 10 zilizoratibiwa na Wizara yake katika eneo la Mji wa Serikali wa Mtumba jijini Dodoma.

"Hamasa hii ya kufanya mazoezi iliasisiwa na viongozi wetu wakuu kuanzia enzi za Baba wa taifa letu Mwalimu Nyerere hadi Rais wetu wa sasa Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan lengo likiwa kuimarisha afya na kujikinga na magonjwa nyemelezi hivyo na sisi tuna wajibu wa kuendelea kuwahamasisha watumishi wa Serikali na wananchi kwa ujumla kwa faida ya vizazi vya sasa na baadaye " amefafanua Waziri Mchengerwa.
Aidha, amewataka watumishi wa TAMISEMI kujenga utamaduni wa kufanya mazoezi wao pamoja na familia zao ili jamii yote iweze kuimarisha afya.

Amesema utamaduni wa kufanya mazoezi ukijengeka siyo tu kwamba utasaidia kuimarisha afya bali utasaidia kupunguza gharama za kutibu magonjwa ambayo yanaweza kujitokeza kutokana na tabia bwete.

Pia Waziri Mchengerwa ametoa wito kwa watanzania kuwa na tabia za kupima afya zao badala ya kungojea hadi wanapoumwa.

Mbio hizo za pole zilizohudhuriwa na mamia ya watumishi wa TAMISEMI ziliishia katika jengo la Ofisi ya TAMISEMI ambako kulikuwa na zoezi la upimaji wa afya kwa hiari.

Kwa upande mwingine, Mhe. Mchengerwa amesema Wizara yake kwa kushirikiana na Wizara ya Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo na Wizara ya Elimu zinaratibu Mashindano ya Michezo kwa Shule za Msingi ( UMITASHUMTA) na Sekondari (UMISSETA) ambapo amefafanua kuwa mashindano hayo yanasaidia kuibua vipaji vya wachezaji.

Amesema Serikali imeendelea kuboresha mashindano hayo ili kuwajengea utamaduni wa wanafunzi kufanya mazoezi na kupenda michezo katika umri mdogo.



 



Mwamvua Mwinyi, Kibaha

Viongozi 20 wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kibaha Mjini, mkoani Pwani—wakiwemo Wenyeviti, Makatibu na Makatibu wa Jumuiya mbalimbali—wameachia nafasi zao wakitarajia kugombea Udiwani wa Kata pamoja na Viti Maalum katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.

Akizungumza kuhusu maandalizi ya uchaguzi huo, Katibu wa CCM Wilaya ya Kibaha Mjini, Issack Kalleiya, alisema viongozi hao wamefuata taratibu stahiki za chama kabla ya kuachia nafasi zao.

“Mimi kama msimamizi wa kanuni katika wilaya, natambua kuwa viongozi hao wamefuata utaratibu wa chama, Chama kina taratibu, katiba, kanuni na miongozo ambayo wanapaswa kuiheshimu,” alisema Kalleiya.

Hata hivyo, alitoa angalizo kuwa pamoja na kujiuzulu, viongozi hao hawaruhusiwi kuanza kampeni kabla ya muda rasmi kuruhusu kufanya hivyo.

“Sasa wao wamepisha ,hatua inayofuata ni kwenda kupata wajumbe wengine watakaochukua nafasi zao ili baadae vikao viweze kujadili , maana unawezakuta watu wanne ama watano walikuwa wajumbe wa kamati ya siasa, hivyo kama wamepisha lazima wapatikane wengine watakaoziba mapengo "alieleza Kalleiya. 

Aidha, Kalleiya aliwasihi wenye nia ya kugombea kushikamana na kufuata taratibu za chama, bila kuleta vurugu au kuanzisha makundi ya kisiasa yatakayohatarisha utulivu wa wilaya.

“Wasitengeneze makundi ya vurugu, wasubiri mchakato rasmi wa kuchukua na kurejesha fomu utakapofunguliwa, Wilaya yetu bado iko salama, changamoto zilizopo ni ndogo na za kawaida hasa kuelekea kipindi cha uchaguzi,” alisisitiza.

Aliongeza kuwa ni jambo la kawaida kwa makundi kujitokeza katika hatua za mchakato wa uchaguzi, lakini alisisitiza kuwa hayapaswi kusababisha mgawanyiko au kuathiri mshikamano ndani ya chama.

“Nawasihi pia wasikubali kushawishiwa na zawadi au ahadi zisizo rasmi ambazo zinaweza kuchochea vurugu, Waendelee kuwa watulivu hadi pale utaratibu wa chama utakaporuhusu hatua zinazofuata,” alionya.

Kwa mujibu wa ratiba ya uchaguzi ya CCM mwaka 2025, kuchukua na kurejesha fomu za kugombea Udiwani,Wadi, Ubunge, Uwakilishi na Viti Maalum kutafanyika kuanzia Juni 28 hadi Julai 2 mwaka huu. 

Vikao vya uchujaji wa wagombea vitaanza Julai 4,2025 kabla ya kufanyika kwa kura za maoni.

Na Mwamvua Mwinyi-

Pwani – Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Wilson Mahera, amefunga awamu ya kwanza ya mafunzo ya Utawala Bora wa Elimu kwa Maafisa Elimu Kata 346 kutoka mikoa ya Pwani na Morogoro, yaliyofanyika kwa siku tatu kuanzia Juni 11 hadi 13, 2025.

Mafunzo hayo yaliratibiwa na Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM), yakilenga kuwawezesha Maafisa Elimu hao kusimamia vyema shughuli za maendeleo ya elimu katika ngazi ya kata, kwa kuzingatia misingi ya utawala bora, uwajibikaji na ufanisi.

Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo, Dkt. Mahera amepongeza juhudi za Serikali katika kuboresha elimu kupitia uimarishaji wa uongozi katika ngazi za msingi. 

Mahera ameeleza mafunzo haya kutoka ADEM yamelenga kuhakikisha kuwa Maafisa Elimu wa mikoa, halmashauri na kata wanazingatia misingi ya uongozi bora na utoaji wa huduma bora za elimu. 

Mtendaji Mkuu wa ADEM, Dkt. Maulid J. Maulid, amesema mafunzo hayo yataendelea kutolewa kwa Maafisa Elimu wa mikoa na halmashauri zote nchini na yamefadhiliwa na mradi wa BOOST kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia . 

Lengo likiwa kuhakikisha Maafisa Elimu Kata ambao ndio viongozi, wasimamizi na washauri wa masuala yote ya kielimu katika ngazi ya kata wanapata ujuzi stahiki wa namna ya kusimamia vyema shughuli zote za kielimu zinazotekelezwa katika ngazi ya Kata kwa kuzingatia vigezo vya Utawala Bora katika elimu.


 

Serikali kupitia Wakala wa barabara Tanzania(TANROADS) Mkoani Ruvuma,imeanza kufanya matengenezo makubwa ya barabara zinazoelekea kwenye maeneo ya uzalishaji ikiwemo maeneo yanayolimwa zao la kahawa ili kutoa fursa kwa wakulima kusafirisha mazao yao kwa urahisi pindi wanapohitaji kupeleka sokoni.

Barabara ambazo zimeanza kufanyiwa matengenezo zinaunganisha Wilaya ya Mbinga na Nyasa ambazo ni maarufu kwa kilimo cha zao la kahawa ambalo ni nguzo muhimu kiuchumi kwa wananchi,na Mkoa wa Ruvuma kwa ujumla, kufanyika kwa urahisi ili kuwahi masoko yaliyopo kwenye maeneo ya mjini.

Kaimu Meneja wa Tanroads Mkoa wa Ruvuma Mhandisi Fedinand Mdoe amesema,miongoni mwa barabara zinazofanyiwa matengenezo ni barabara ya Nyoni-Mpapa-Mkenda yenye urefu wa kilometa 108.52 inayounganisha Wilaya ya Mbinga na Nyasa.

Amesema,katika barabara hiyo kazi zinazofanyika ni matengenezo ya kawaida urefu wa kilometa 80.52 na Serikali kupitia Tanroads imetenga Sh.milioni  421,260,000.

Aidha amesema,wanafanya matengenezo sehemu korofi kilometa 27 kwa gharama ya Sh.milioni  763,368,000 pamoja na kujenga kingo  ya madaraja 3  kazi itakayogharimu Sh.milioni 60.046.

Mdoe ametaja kazi nyingine zinazofanyika katika barabara hiyo ni ujenzi wa makalavati 2 kwa gharama ya Sh.milioni 288.051 kazi inayotarajiwa kukakamilika mwezi Septemba mwaka huu.

Pia amesema,wameanza matengenezo ya maeneo mabovu kwenye barabara ya Nyoni-Mpapa-Maguu yenye urefu wa kilometa 30 na barabara ya Mbinga-Mkiri.

Amesema,katika barabara hiyo kazi zinazofanyika ni kuweka lami kwenye miinuko na maeneo korofi kutokana na  umuhimu wa barabara hiyo kiuchumi kwa wananchi wa Wilaya ya Mbinga na Wilaya ya Nyasa.

“Barabara nyingine zinazofanyiwa matengenezo ni Mbambabay-Lituhi ambayo iko kwenye ukarabati mkubwa,kuna kazi ya dharura inayoendelea katika eneo ya Lwika takribani kilometa 15 kutoka Mbambabay,tutaboresha  kwa kuinua tuta na kujenga box kalavati na kumwaga changarawe”alisema Mdoe.

Kwa mujibu wa Mdoe,barabara ya Nang’ombo kwenda Chiwindi nayo  inafanyiwa matengenezo kwa kuweka kifusi,lakini changamoto kubwa ni  magari yenye uzito mkubwa hasa yanayobeba makaa ya mawe kupitia kwenye daraja la chuma.

“tunawaomba wenzenu makampuni yanayojishughulisha na uchimbaji wa makaa ya mawe,kuzingatia sheria  kwa kutozidisha uzito kwenye magari yao,wasijali biashara yao  badala yake waangalie maslahi ya watu wengine ambao ni watumiaji wa barabara  ile”alisisitiza Mdoe.

“kimsingi kazi zetu nyingi tutazikamilisha mwaka huu wa fedha,zile barabara chache za kipaumbele tutaendelea nazo hadi mwezi Septemba mwaka 2025”alisema Mdoe.



Tamasha la Fintech la teknolojia ya kifedha katika Afrika mashariki lilionza tarehe 13 juni mwaka 2025 katika ukumbi wa Julius Nyerere international convention center (JNICC), limeelezwa ndio tamasha kubwa zaidi Afrika mashariki linalokutanisha wakali wa teknolojia wa fedha kutoka nchi zaidi ya 70 Duniani na kuungana na jumuiya ya fintech na kujadili fursa mbalimbali zinazosaidia kukuza teknolojia ya kifedha pamoja na kuinua uchumi kwa njia ya teknolojia.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi mkuu wa kampuni ya Eastern Star consulting group bw. Deogratius Kilawe katika ufunguzi wa tamasha hilo.




NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

Wahitimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) wametakiwa kuthibitisha kwa vitendo uwezo wao walioupata chuoni kwa kutumia maarifa hayo kuleta mabadiliko chanya katika jamii na taifa kwa ujumla.

Wito huo umetolewa leo Juni 13, 2025 katika Mahafali ya 55 ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam.

“Sasa ni wakati wa kuchukua hatua, kuandika, kuzungumza kwa busara na kushughulikia changamoto za jamii kwa njia bunifu na yenye maadili". Amesema Prof. Anangisye.

Aidha amesema kuwa katika Duru ya Kwanza ya Mahafali ya 55, chuo hicho kimehudhurisha wahitimu 829 wakiwemo wa shahada ya uzamivu, shahada ya umahiri, stashahada ya uzamili, shahada ya awali, stashahada na astashahada.

Kwa upande wake, Rais na Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Dkt. Akinwumi Ayodeji Adesina, ambaye alitunukiwa Shahada ya Heshima ya Sayansi, alieleza kuridhishwa na mwenendo wa uchumi wa Tanzania.

“Katika kipindi cha miaka 10 ya uongozi wangu kuanzia 2015 hadi 2025, AfDB imetoa msaada wa dola bilioni 4.73 kwa Tanzania, sawa na asilimia 53 ya mikopo yote ambayo benki yetu imetoa kwa nchi hiyo katika kipindi cha miaka 54,” alisema Dkt. Adesina.

“Kwa msukumo wa ukuaji katika kilimo, utalii, huduma za kifedha, uzalishaji viwandani, ujenzi wa madini sambamba na sera thabiti za mwenendo wa uchumi wa fedha, ukuaji halisi wa pato la taifa la Tanzania ukiongezeka kutoka asilimia 5.1 mwaka 2023 hadi asilimia 5.6 mwaka 2024 ” amesema.

Nae Mkuu wa UDSM, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete amesema pamoja na hayo, Dkt. Adesina ni mdau mkubwa wa maendeleo hasa ya miundombinu.

“Huyu tuliyemtunuku benki yake ni mdau mkubwa kwa maendeleo,” amesema Kikwete.


* Filamu 430 zapokelewa kutoka Nchi za Afrika, Ulaya……

Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

MAANDALIZI ya Tamasha la Kimataifa la Filamu la Zanzibar (ZIFF,) maarufu kama Tamasha la Nchi za Majahazi msimu wa 28 kwa mwaka 2025 yamekamilika na kuelezwa kuwa litafanyika Juni 25 hadi 29 mwaka huu Ngome Kongwe Zanzibar.

Akizungumza na waandishi wa habari leo  Katika ukumbi wa Goethe Institut jijini Dar es Salaam Mtendaji Mkuu wa ZIFF, Joseph Mwale amesema kuwa ; Maandalizi kwa ajili ya Tamasha hilo kwa mwaka huu yamekamilika na litabebwa na kauli mbiu ya ‘Tumaini Linalochipukia.’ 

Amesema Tamasha hilo ambalo limekuwa kivutio barani Afrika na duniani kwa ujumla limeendelea kuvutia watu wengi zaidi na kwa mwaka huu licha ya burudani mafunzo mbalimbali yanayohusu uandaaji wa filamu yatatolewa.

Akitangaza filamu zilizoingia katika kinyang’anyiro hicho Mkurugenzi wa tamasha la ZIFF, Hatibu Madudu amesema kuwa;  Tamasha hilo litahusisha maonesho ya filamu, warsha, na panorama.

“Mwaka huu tumepokea mwaka filamu 430 zilizotengenezwa kati ya mwaka 2024 na 2025 yaani filamu zilizotengenezwa ndani ya mwaka mmoja pekee kutoka nchi mbalimbali duniani zikihusisha bara la Afrika na Ulaya.” Amesema.

Madudu amesema kuwa, jumla ya filamu 174 zimewasilishwa kutoka ukanda wa Afrika Mashariki ambapo Kenya iliwasilisha filamu (54), Uganda filamu (52), Tanzania (49), Somalia nane (8), Rwanda 6, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo nne (4), na Burundi filamu moja.

Aidha amesema kuna filamu zilizowasilishwa kutoka Nchi 100 zaidi zikiwemo India, Brazil, Marekani, China, Ufaransa , Italia, Uturuki, Nigeria, Argentina, Spain, Poland, United Kingdom, Germany, Canada, Indonesia, Russia Federation, Qatar, Japan, United Arab Emirates, Pakistan, Tunisia, Angola, Malawi, Portugal, Belgium, Zimbabwe, Mayote, Vietnam, Reunion, Romania, Saudi Arabia, Oman, Morocco, Lebanon, Jamaica, Botswana, Burkina Faso, Ghana, Senegal, Sudan na Ethiopia.

Awali Mkurugenzi wa Goethe-Institut Tanzania Mpangi Otte alieleza kuwa wanajivunia kudhamini Tamasha hilo kubwa lenye hadhi ya kimataifa.

 Otte amesema Tamasha la ZIFF limebeba thamani katika ni filamu, maono pamoja na sauti zinazosimulia

hadithi za Afrika kwa upekee uliobeba sanaa na jumbe kwa jamii na kusisitiza kuwa Goethe Institut wanaamini kuwa tamaduni sio anasa bali ni kuwaleta watu pamoja na kujifunza na kupitia ZIFF Tanzania, Afrika na dunia kwa ujumla watajifunza kupitia filamu hizo, mijadala pamoja na mafunzo mbalimbali yatakayotolewa. 

Baadhi ya waandaaji na waigizaji wa filamu zilizochaguliwa katika kinyang’anyiro hicho na filamu zao kuoneshwa katika Tamasha hilo wameeleza furaha yao ya kupata fursa hiyo na kusema kuwa kupitia kazi zao jamii itapata ujumbe ambao hauwekwi wazi katika kazi nyingi za sanaa ikiwemo afya ya akili.

Cecilia Lubango, mwongozaji wa filamu ya Tears in the Rain inayohusu afya ya akili kwa wanawake waliojifungua kwa mara ya kwanza amesema ni wakati kwa 

wasanii kutumia filamu kuweka wazi matatizo yaliyopo katika jamii.

“Ninafurahi filamu hii niliyoongoza inakwenda kuoneshwa katika jukwaa kubwa la ZIFF. Hii ni mara ya kwanza kwangu, ila niwaombe wasanii wenzangu tutumie filamu kuanika matatizo katika jamii.” Ameeleza Cecilia.

Katika hatua nyingine, Mwongoza filamu ya Ndoto Yangu, Sama Johanpow, inayohusu masuala ya elimu, amesema pamoja na kupata fursa  filamu yake kuonesha katika Tamasha la ZIFF imempa moyo na kujiona katika nafasi kubwa kwa miaka ya mbele.

Katika siku ya ufunguzi wa Tamasha hilo Juni 25 saa mbili usiku filamu itakayooneshwa ni Janani The Last Stand kutoka Uganda iliyoongozwa na Matt Bish.

Tamasha la ZIFF 2025 limedhaminiwa na Umoja wa Ulaya (EU), Azam Media Ltd, Air Tanzania na CANNEX, Serikali ya Zanzibar, Wizara ya Utalii Zanzibar, Infinity Group Zanzibar, Maru Maru Hotel, Emerson Hotel, Goethe Institut, The Box, Archipelago Restaurant na Nafasi Film Club.

Mkurugenzi wa Goethe-Institut Tanzania Mpangi Otte akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na tamasha hilo na kusema kuwa  wanajivunia kudhamini tamasha hilo kubwa lenye hadhi ya kimataifa. Leo jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa ZIFF, Joseph Mwale akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya tamasha la ZIFF 2025 na kueleza kuwa tamasha hilo lenye kauli mbiu ya  ‘Tumaini linalochipukia’ yamekamilika. Leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa ZIFF, Hatibu Madudu, akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na Tamatha la ZIFF msimu wa 28 na kueleza kuwa kwa mwaka huu wamepokea filamu 430 zilizotengenezwa kati ya mwaka 2024 na 2025 kutoka nchi mbalimbali duniani. Leo jijini Dar es Salaam.
Kutoka kushoto; Mkurugenzi wa Goethe Institut Tanzania Mpangi Otte, Mtendaji Mkuu wa ZIFF Joseph Mwale, Mkurugenzi wa ZIFF, Hatibu Madudu na Mwakilishi wa Bodi ya Wakurugenzi, wakionesha nembo itakayotumika katika maonesho ya ZIFF mwaka huu.


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa amezindua 'Albino Mobile App' ambayo ni program ya simu janja itakayowezasha usajili na ukusanyaji wa taarifa za watu wenye Ualbino na wenye Ulemavu kwa njia ya kidigitali.

Aidha, amesema Mfumo wa Albino Mobile App ni sehemu ya Mfumo wa Kitaifa wa Taarifa za Watu wenye Ulemavu (PD – MIS) utaongeza ujumuishaji wa Watu wenye Ulemavu kwenye huduna za kijamii na maendeleo.

Amesema hayo leo Juni 13, 2025 wakatu alipomuwakilisha Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye Maadhimiwho ya Siku ya Kimatqifa yw kukuza uelewa kuhusu Ualbino ambayo yamefanyika katika uwanja wa Mwanga Center, mkoani Kigoma.

Vile vile, amewaagiza Wakuu wa Mikoa kusimamia kikamilifu utekelezaji wa Mpango Kazi wa Taifa wa Haki na Ustawi kwa Watu wenye Ualbino, Mkakati wa Taifa wa Teknolojia Saidizi na Mfumo wa Kielektroniki wa Ukusanyaji wa Taarifa za Watu wenye Ulemavu (PD-MIS) katika ngazi ya Halmashauri.

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema kuwa programu hiyo janja ya ' Albino Mobile App' itarahisisha na itahakikisha usahihi wa taaarifa za usajili wa watu wenye Ualbino katika maeneo mbalimbali nchini.

“Mfumo huu utapunguza gharama za usafiri na usafirishaji wa vifaa kwa ajili ya usajili, na pia kuwezesha upatikanaji wa takwimu sahihi zinazosaidia Serikali kupanga na kutekeleza sera kwa ufanisi” amesema

Naye, Mwenyekiti wa Chama cha Watu Wenye Ualbino Tanzania (TAS), Godson Mollel amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita imeendela kuwafanyia mambo makubwa watu wenye Albino nchini ikiwemo kutenga fedha kwa ajili ya kuwezesha upatianaji wa mafuta kinga ambayo hugawiwa bure.




Katika ulimwengu wa leo unaokumbwa na changamoto nyingi za kiafya, viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Lindi wametoa wito maalum kwa vijana na wananchi wote kufanya mazoezi mara kwa mara kama njia ya kuimarisha afya na kuzuia magonjwa yasiyoambukiza. Wito huo umetolewa wakati wa maonyesho ya madini yanayoendelea katika viwanja vya madini wilayani Ruangwa.Katika ulimwengu wa leo unaokumbwa na changamoto nyingi za kiafya, viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Lindi wametoa wito maalum kwa vijana na wananchi wote kufanya mazoezi mara kwa mara kama njia ya kuimarisha afya na kuzuia magonjwa yasiyoambukiza. Wito huo umetolewa wakati wa maonyesho ya madini yanayoendelea katika viwanja vya madini wilayani Ruangwa.Katika ulimwengu wa leo unaokumbwa na changamoto nyingi za kiafya, viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Lindi wametoa wito maalum kwa vijana na wananchi wote kufanya mazoezi mara kwa mara kama njia ya kuimarisha afya na kuzuia magonjwa yasiyoambukiza. Wito huo umetolewa wakati wa maonyesho ya madini yanayoendelea katika viwanja vya madini wilayani Ruangwa.




Na Fredy Mgunda,Lindi.



Katika ulimwengu wa leo unaokumbwa na changamoto nyingi za kiafya, viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Lindi wametoa wito maalum kwa vijana na wananchi wote kufanya mazoezi mara kwa mara kama njia ya kuimarisha afya na kuzuia magonjwa yasiyoambukiza. Wito huo umetolewa wakati wa maonyesho ya madini yanayoendelea katika viwanja vya madini wilayani Ruangwa.

Viongozi hao wamebainisha kuwa afya njema siyo tu msingi wa maisha bora, bali pia ni mtaji muhimu kwa maendeleo ya mtu binafsi na taifa kwa ujumla.

“Afya bora ndiyo msingi wa maisha na maendeleo ya mtu binafsi na taifa. Tunapaswa kujenga utamaduni wa kufanya mazoezi kila wakati ili kuimarisha kinga ya mwili dhidi ya magonjwa mbalimbali,” walisisitiza viongozi hao.

Mazoezi ya mwili yameelezwa kuwa na faida lukuki ikiwa ni pamoja na kupunguza hatari ya kupata magonjwa ya moyo, kisukari, shinikizo la damu na unene uliopitiliza.

Kwa vijana, mazoezi husaidia katika kujenga miili imara, kuimarisha uwezo wa kujifunza na kujiamini, na pia kupunguza msongo wa mawazo.

Pamoja na kutoa wito wa mazoezi, viongozi hao waliwahamasisha wananchi kuendelea kujitokeza kwa wingi katika maonyesho ya madini yanayoendelea, kwani yameleta fursa nyingi za kiuchumi na kielimu kwa wakazi wa Lindi na maeneo jirani.

Maonyesho hayo yanalenga kuinua sekta ya madini kwa kuonesha teknolojia mpya, mbinu za usindikaji, pamoja na fursa za uwekezaji katika rasilimali za madini.

Kwa kuzingatia mchango mkubwa wa vijana katika maendeleo ya taifa, viongozi hao wamehimiza kuwa ni muhimu kwa vijana kuwekeza katika afya zao kupitia mazoezi na pia kutumia fursa kama hizi za maonyesho kupata maarifa yatakayowasaidia kuinua maisha yao na ya jamii kwa ujumla.

Mazoezi ya mwili ni njia rahisi na ya gharama nafuu ya kujilinda dhidi ya maradhi na kuimarisha afya. Viongozi wa Mkoa wa Lindi wameweka wazi kuwa ni wajibu wa kila mmoja, hasa vijana, kuchukua hatua na kuwa mabalozi wa afya bora kupitia mazoezi ya mara kwa mara.
Juni 13, 2025-Dar Es Salaam.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Dkt. Tausi Kida amezikutanisha Timu ya Wataalamu wa Kuandaa Mpango wa Pili wa Maboresho ya Mazingira ya Biashara na Uwekezaji (MKUMBI II) na Tume ya Rais ya Maboresho ya Kodi kwa kikao-kazi cha kubadilishana uzoefu leo Juni 13, 2025 jijini Dar es Salaam.

Akiongea, katika kikao hicho, Dkt. Kida amesema kuwa lengo kuu la kikao hicho ni kujadili namna kuhuisha mbinu za mashauriano na sekta binafsi na kupata mapendekezo yanayohusu changamoto za Kodi na sizizo za kikodi ili kuhakikisha kwamba Tanzania inakuwa na mazingira Bora ya Biashara na Uwekezaji na Mifumo imara ya kikodi.

Aidha, kikao hicho kimehudhuriwa na Mwenyekiti wa Tume ya Rais ya Maboresho ya Kodi, Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu Mheshimiwa Balozi Ombeni Sefue na Wajumbe wa Tume hiyo, na Mwenyekiti wa Wataalamu wa MKUMBI II, Prof. Faustine Kamuzora.




WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali inawathamini Watu wenye Ulemavu wakiwemo wenye ualbino na wakati wote itahakikisha inawalinda na kuwapatia fursa stahiki katika ujenzi wa Taifa.

Amesema katika kuendelea kutekeleza mpango wa uwezeshaji wananchi kiuchumi kwa kutumia mikopo inayotokana na mapato ya ndani ya Halmashauri, hadi kufikia Machi, 2025 tayari shilingi bilioni 5.48 zimetolewa kwa vikundi 891 vya Watu Wenye Ulemavu nchini.

Amesema kuwa Serikali itaendelea kuchukua hatua mahsusi za kuimarisha ustawi na utoaji huduma kwa watu wenye ualbino ikiwemo kuwatambua, kuimarisha mifumo ya kisera na kuwezesha upatikanaji wa huduma muhimu hapa nchini.

Ametoa kauli hiyo leo Ijumaa (Juni 13, 2025) wakati alipomuwakilisha Rais Dkt. Samia kwenye kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Uelewa kuhusu Ualbino yaliyofanyika katika uwanja wa Mwanga Centre, mkoani Kigoma.

Ameongeza kuwa katika mwaka 2024/2025 kiasi cha ruzuku inayotolewa kwa Vyama vya Watu wenye Ulemavu kimeongezeka hadi kufikia shilingi milioni 230 ikilinganishwa na shilingi milioni 200 zilizotolewa kwa mwaka 2023/2024.

Akizungumza kuhusu kuimarika kwa utoaji wa huduma za afya kwa watu wenye Ualbino, Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa kwa kipindi cha kuanzia Julai 2021 hadi Juni 2024 Serikali kupitia Bohari Kuu ya Dawa (MSD) ilitumia zaidi ya shilingi milioni 500 kusambaza katika mikoa yote 26 ya Tanzania mafuta kinga ya saratani ya ngozi kwa Watu wenye Ualbino.

“Kwa mwaka wa fedha 2024/2025, Serikali ilitenga shilingi bilioni 8.743 kwa ajili ya huduma za ustawi wa Jamii na shilingi 182. 8 kwa ajili ya ununuzi wa mafuta kinga ya saratani ya ngozi kwa watu wenye Ualbino.”

Aidha, Majaliwa amewaagiza Wakuu wa Mikoa wahakikishe wanasimamia kikamilifu utekelezaji wa Mpango Kazi wa Taifa wa Haki na Ustawi kwa Watu wenye Ualbino, Mkakati wa Taifa wa Teknolojia Saidizi na Mfumo wa Kielektroniki wa Ukusanyaji wa Taarifa za Watu wenye Ulemavu (PD-MIS) katika ngazi ya Halmashauri.

Kwa Upande wake, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Ridhiwani Kikwete amesema kuwa kupitia maadhimisho hayo, Serikali imezindua programu janja ‘Albino Mobile App’ ambayo itawezesha kufanya usajili na ukusanyaji wa taarifa za watu wenye ualbino kwa njia ya kidigitali.

Amesema kuwa mfumo huo utarahisisha, utaharakisha na utahakikisha usahihi katika usajili wa watu wenye ualbino na ulemavu nchini Tanzania, hususan walioko maeneo ya pembezoni.

“Mfumo huu utapunguza gharama za usafiri na usafirishaji wa vifaa kwa ajili ya usajili, na pia kuwezesha upatikanaji wa takwimu sahihi zinazosaidia Serikali kupanga na kutekeleza sera kwa ufanisi,” alisema.

Naye, Mwenyekiti wa Chama cha Watu Wenye Ualbino Tanzania (TAS) Godson Mollel Amesema kuwa Serikali imefanya mambo makubwa yenye lengo la kuwawezesha watu wenye Albino nchini ikiwemo kutoa fedha kwa ajili ya kununua mafuta kinga ambayo hugawiwa bure.

“Pia, Serikali imetoa agizo kwa halmashauri kutoa fedha kwa ajili ya kununua mafuta kinga ambayo imesaidia kupunguza uhaba wa mafuta kinga”

Pia, Godson amewataka watu wenye ulemavu kujitokeza kwa wingi kushiriki katika uchaguzi mkuu wa Rais, wabunge na madiwani utakaofanyika Oktoba 2025 “Jitokezeni kwa wingi kushiriki katika uchaguzi mkuu, mkifanya hivyo mtakuwa mmetimiza haki yenu ya kikatiba ya kuchagua au kuchaguliwa”

Katika Maadhisho hayo Mheshimiwa Majaliwa alizundua Programu janja ya usajili ya wenye ualbino ‘Albino Mobile App’. itakayowezesha kuwasajili na kuwatambua wenye ualbino.

Juni 13,2025
MKUU wa Wilaya ya Kibiti, Kanali Joseph Kolombo, ametoa onyo kwa baadhi ya watu wanaojihusisha na utoroshaji wa mazao na kusema ni ukiukaji wa sheria unaodidimiza maendeleo ya Wilaya na Mkoa.

Kolombo ameeleza hayo Juni 12, 2025 wakati akizindua rasmi mnada wa kwanza wa zao la ufuta kwa msimu wa mwaka 2025, uliofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti, mkoani Pwani.

Amewataka wakulima kuzingatia taratibu na kanuni za Serikali katika uuzaji wa mazao, akieleza kuwa ni muhimu kuyapeleka kwenye maghala rasmi ili kulinda maslahi ya wakulima na kuchochea mapato halali kwa Halmashauri.

Aidha Kolombo ameagiza taasisi za kifedha kutoa huduma kwa weledi na kurahisisha upatikanaji wa akaunti kwa wakulima ili kuimarisha mzunguko wa fedha katika maeneo ya vijijini.

Amewaasa wanunuzi wa mazao kuhakikisha wanalipa kwa wakati ili kusaidia wakulima kufidia gharama walizotumia katika uzalishaji.

Katika mnada huo wa kwanza, bei ya kilo moja ya ufuta ilifikia sh. 2,414.49, na mnada unaofuata unatarajiwa kufanyika Juni 19, 2025, katika eneo la Kingoma AMCOS, Wilaya ya Mkuranga.

Mnada huo umetajwa kuwa hatua muhimu katika kuinua uchumi wa wakulima wa Mkoa wa Pwani kupitia mfumo rasmi unaolinda haki na mapato ya pande zote.

Top News