yaani wadau nyumbani ni nyumbani tu. mie kuliona tu hili daraja la manzese leo roho imekuwa baridiiii. yaani....we acha tu! nyumbani kutamu, nawahurumia wanaosita kurudi bongo; hawajui wanachokikosa....

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 17 mpaka sasa

  1. Duuh michu umekula rushwa na mtaarisha wa show ya ray c uholanzi umeondoa ile picha ya ray c ya uholanzi ili tusimpe ukweli huyo jamaa aliyetutalishia onyesho fake lkn pamoja na hayo hatuthudhulia tena show atakazo taalisha hadi atuombe radhi kwa kitendo alichotutendea na isipotoka ktk blog tutaamini kuwa rushwa imetembea ktk blog yako.

    ReplyDelete
  2. DARAJA HILO SALAMA MCHANA TU. LAKINI ASUBUHI NA MITAA YA JIONI HADI USIKU, HAKUPITIKI HAPO. WAKABAJI NA VIBAKA KAMA UNARIAAA VILEEE BABAKE. SIPITI HAPO PIGA, GALAGAZA, UA BORA NIVUKE BARABARA NIGONGWE NA MANGONGONGO YA BONGO.

    ReplyDelete
  3. kaka michuzi wewe kweli ni mzalendo yaani hii nchi yenye matatizo chungu nzima- umaskini,ujinga,uonevu,vibaka,maisha magumu n.k wewe unfurahia kurudi huku? ama kweli matatizo umeyazoea kaka!

    ReplyDelete
  4. Yaani wewe daraja ndio limekufanya urudi bongo...wadau bwana...wengine vichwa maji tu...utakula hilo daraja....grow up

    ReplyDelete
  5. MHESHIMIWA ISSA HABARI ZA LEO TUNASHUKURU KWA PICHA NZURI KUONYESHA DARAJA NA UBUNIFU WA KUEPUSHA AJALI KWA WATEMBEAO KWA MIGUU..INASEMEKANA HILO DARAJA"..VIBAKA.." WAMEWEKEZA NA POLISI WANAWAFAHAMU FIKA.."..PESA NI SABUNI YA ROHO.."

    ReplyDelete
  6. Huyo aliyeleta hii picha ni nzuri lakini kwa comments zake he/she is so yesterday. Kwani kilichokurudisha bongo wewe ni madaraja au roho inakusuta tu.....Inaelekea ulikua mkimbizi siku nyingi sana mbona hilo daraja halijajengwa jana?
    Acha ushamba...maendeleo sio madaraja kubwa jinga

    ReplyDelete
  7. mi nawaonea huruma zaidi wale wanaong`ang`ana Dar , hata hawakumbuki kurudi vijijini kwao .

    ReplyDelete
  8. Michuzi mbona mie sioni daraja hapo?

    ReplyDelete
  9. MICHUZI UNATUONEA HURUMA WATU AMBAO HATUTAKI KURUDI BONGO?MI NAWAONEA HURUMA WALE AMBAO WAMEMALIZA VYUO NA HAWANA KAZI NA SHIDA ZOTE ZINAZOWAKABILI,MICHUZI MAISHA MAGUMU SANA NCHI HIYO!

    ReplyDelete
  10. Kaka Michu Huyo annoy Hapo juu anayesema Haoni Daraja labda tumuulize anaona nini hapo juu?

    ReplyDelete
  11. Dar tunahiji madaraja kama hayo 15-20. Siyo mmoja tu, likolojengwa 1993!

    ReplyDelete
  12. KAKA MICHU AFDAHALI WEWE UNATUHABARISHA NA KUTUKUMBUSHA MAMBO MENGI KAMA HAYA AMBAYO KWANGU MIMI YANAJENGA MUHIMIRI WA KUWA NA KUJIVUNA KUWA MTANZANIA. Ninasema hivi kwa sababu tunapata habari zingine ambazo zinatia kichefuchefu na has kwa sababu zinatoka mahala pazito Mambo kama haya : "Sakata la mjusi wa Tanzania aliyechukuliwa na Wajerumani enzi za ukoloni, laibuliwa Bungeni"- Jamani wabunge wangekuwa wakitizama basi mabunge kama ya uingereza michango ambayo inatolewa na wabunge wenzi wao!!! Hivi mpaka lini tutakaa tusikiliza uwakilishi kama huu!!!! BUNGE ni mahala pazito jamani waendao hapo changamkeni kutoa hoja zenye usuluhishi na siyo kama hii!!! Sasa kama Wajerumani wakisema mkachuke huyu mjusi gharama za usafiri na matunzo nani atafidia!!! (KODI ZA WANANCHI) mna hakika mtapata watalii wa kutosha kulipia ghrama hizo? milifanya wapi huo utafiti? tupeni data!!! si kubwabwaja tu... (aDk)

    ReplyDelete
  13. Nadhani aliyesema haoni bridge hakukosea

    Hilo linahitajika kuitwa overpass lakini lugha yetu inageneralized vitu vingi tu...kama vile mamba- tunajua tu crocodile na kobe- tunajua tu tortoise
    Kumbe kuna alligator, crocodile etc na kuna turtle, tortoise etc.

    Kwa hiyo hilo Kiswahili ni daraja lakini kiingereza ingeitwa Overpass ilikutofautisha

    An overpass is a bridge over a freeway or railway

    A bridge a structure that allows people or vehicles to cross an obstacle such as a river or canal etc

    ReplyDelete
  14. sawa sawa anon 7;49 mie pia sioni daraja. daraja nijuavyo ni sehemu iliyo jengwa kua kivukio cha magari au watu chini yake kuna maji either ya mto ambayo yanaelekea ziwani au baharini.

    ReplyDelete
  15. Wenye ulemavu na wanaotumia baiskeli za miguu mitatu wanapitaje ktk ngazi za hilo daraja?

    ReplyDelete
  16. We anony wa August 8, 2007 7:49:00 PM EAT,acha kuchemka.Kama hujui maneno ya Kiswahili kaa kimya, si kuweka maandiko yasiyo na maana hapa. Kiswahili hakina 'generalization' km wewe unavyotaka tuamini. 'Crocodile' km unavyosema ni mamba, 'alligator' ni kenge, 'turtle' ni kasa na 'tortoise' anaitwa kobe. Upo hapo?

    ReplyDelete
  17. annoy hapo juu unatudanganya nani kakwambia wewe kenge ni aligator.....kenge ni lizard jamii ya iguana.

    wewe huyo kasa unamjua mwenyewe kweli ...waulize watu kasa ni nini kama kuna mtu anajua...na wasioona daraja hapo hawajakosea

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...